Alhamisi, 16 Februari 2012

LIBYA IMESHINDWA KUDHIBITI WAPIGANAJI


misrata
Watu weusi ndio wanateswa zaidi

Shirika la kutetea haki za binadamu, Amnesty International linasema visa vya mateso, mauaji na watu kuzuiliwa bila kufunguliwa mashataka vimekithiri nchini Libya.
Shirika hilo linasema ukiukaji huo unatekelezwa na makundi ya wapiganji waliojihami ambao walimng'oa Muammar Gaddafi madarakan
Walioathirika zaidi ni watu wanaohofiwa kuwa wafuasi wa Gaddafi, waafrika weusi na wahamiaji walioko Libya.
Kufuatia visa hivyo makundi ya watu waliolengwa sana na visa hivyo wamehama makaazi yao.
Shirika la Amnesty international linasema serikali mpya ya Libya imeshindwa kuwachukulia hatua watu wanaotekeleza vitendo hivyo.
Kuanzia mwezi uliopita BBC imekuwa ikikusanya ushaidi wa mateso yanaoendelea miji ya Misrata, Gharyan na kusini mwa mji mkuu Tripoli.
Ijumaa hii, sherehe zitafanyika kote nchini Libya kuadhimisha mwaka mmoja tangu mapinduzi yaanze ambayo yalitarajiwa kuleta mabadiliko.
Kuna wasiwasi mkubwa sasa kuwa watu waliosaidiwa na NATO kuupindua utawala wa zamani, sasa wanahatarisha siku za baadaye za nchi hii

Maoni 1 :