Jumamosi, 31 Machi 2012

WAZIRI EMMANUEL NCHIMBI KATIKA KAMPENI ZA UDIWANI KATA YA LIZABONI HUKO SONGEA JUZI.

DKT EMMANUEL NCHIMBI MBUNGE WA SONGEA MJINI NA WAZIRI WA HABARI UTAMADUNI NA MICHEZO ATINGA KAMPENI ZA UDIWANI KATA YA LIZABONI MANISPAA YA SONGEA

 Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi akimnadi mgombea wa Udiwani wa Kata ya Lizaboni, Manispaa ya Songea kupitia CCM  George Oddo aliyesimama kushoto kwenye mkutano uliofanyika kwenye ofisi za CCM kata ya Lizaboni juzi.
 Mamia ya wananchi wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi akimnadi mgombea wa Udiwani wa Kata ya Lizaboni, Manispaa ya Songea kupitia CCM  George Oddo kwenye mkutano uliofanyika kwenye ofisi za CCM kata ya Lizaboni juzi.
Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Dkt Emmanuel Nchimbi akimnadi mgombea wa Udiwani wa Kata ya Lizaboni, Manispaa ya Songea kupitia CCM  George Oddo kwenye mkutano uliofanyika kwenye ofisi za CCM kata ya Lizaboni juzi.(Habari na picha kwa hisani ya Stephano Mango)

ARSENAL YAFUNGWA 2-1 NA QPR, MAN CITY YATOKA SARE.

Arsenal hoi, Chelsea kidedea, City sare.

Manchester City walimaliza mchezo kwa mtindo wa aina yake baada ya kuwa nyuma kwa mabao 3-1 kipindi kirefu cha mchezo na kufanikiwa kusawazisha na kuwa mabao 3-3 dhidi ya Sunderland katika uwanja wa Etihad.
Mario Balotelli aliyefunga mabao mawili kwa Man City
Mario Balotelli aliyefunga mabao mawili kwa Man City

Sebastian Larsson alikuwa wa kwanza kuipatia bao Sunderland kabla Mario Balotelli hajasawazisha kwa mkwaju wa penalti kutokana na rafu aliyofanyiwa Dzeko.
Sunderland walijiimarisha kwa kupata bao la pili lililofungwa kwa kichwa na Nicklas Bendtner kabla ya mapumziko na walionekana dhahiri wangeibuka washindi baada ya bao la tatu la Larson.
Lakini Balotelli na Aleksandar Kolarov walibadili hali ya mchezo kwa kusawazsiha, ingawa Manchester City walikuwa wamepoteza rekodi yao ya kushinda uwanja wa nyumbani katika msimu huu.
Licha ya kucheza vizuri na kusawazisha, Man City wanafahamu fika iwapo Manchester United watailaza Blackburn siku ya Jumatatu, mabingwa hao mara 19 watasogea pointi tano nyuma ya City na kuendelea kushikilia usukani.
Lilikuwa pambano la kusisimua hasa dakika za mwisho ambapo Sunderland walionesha kandanda murua na kuweza kuwasumbua kwa muda mrefu wenyeji wao.
Lakini mara tu baada ya kutolewa mlinzi wa kati aliyecheza vizuri sana Matt Kilgallon na nafasi yake kuchukuliwa na Sotirios Krygiakos zikiwa zimesalia dakika 10 mpira kumalizika, wageni walionekana kuparaganyika.
QPR imefanikiwa kupata ushindi muhimu katika jitahada zao za kuepuka kushuka daraja baada ya Samba Diakite kufunga bao lake la kwanza tangu ahamie klabu hiyo na ndio lililoizamisha Arsenal na kupunguza kasi yake ya kushinda.
Adel Taarabt alikuwa wa kwanza kupata bao kwa upande wa QPR baada ya kumpita Thomas Vermaelen na kuachia mkwaju uliojaa wavuni.
Theo Walcott aliisawazishia Arsenal akiwa ndani ya sanduku la QPR na kuachia mkwaju baada ya jitahada zake za awali kugonga mwamba.
Mlinda mlango wa QPR Paddy Kenny alimnyima nafasi ya kufunga Robin van Persie wakati walipobakia wao wawili kabla ya Diakite kupachika bao la ushindi baada ya pasi kutoka kwa Jamie Mackie.
Aston Villa ikiwa nyumbani katika uwanja wao wa Villa Park ilishindwa kuhimili vishindo vya Chelsea baada ya nahodha wao Stiliyan Petrov kugundulika amekumbwa na maradhi ya saratani ya damu.
Mabao yaliyofungwa na Daniel Sturridge na Branislav Ivanovic yaliwasaidia wageni kupata ushindi wa mapema na kumiliki mpira kwa muda mrefu.
Dakika chache baadae zikawa za kuvutia baada ya James Collins kuipatia bao la kwanza Aston Villa, kabla ya Eric Lichaj kusawazisha na kufanya ubao usomeke 2-2.
Lakini sekunde 60 baadae, Ivanovic akafumua mkwaju wa karibu na kupata bao la tatu kabla Fernando Torres kumalizia kazi kwa kufunga bao la nne na la mwisho katika muda wa nyongeza.
Timu ya Everton ikiwa imeimarika ilifanikiwa kuichambua West Brom kwa mabao 2-0, kila bao likipatikana kila kipindi na hivyo kuweza kujinyanyua juu ya mahasimu wao wakubwa Liverpool katika msimamo wa Ligi Kuu ya England.
Leon Osman alikuwa wa kwanza kuifungia Everton kwa mkwaju wa yadi 20, baada ya kogongeana na Nikica Jelavic, na mpira ukamgonga Gareth McAuley wa West Bromich na kumzubaisha mlinda mlango Ben Foster.
Ni mkwaju wa chinichini wa Victor Anichebe ulizidisha furaha kwa Everton ambao wiki iliyopita waliweza kupata nafasi ya kucheza nusu fainali ya ya Kombe la FA Cup ambao kwa sasa wamejinyanyua hadi nafasi ya saba.
Nafasi nzuri waliyoipata West Brom Albion ilikuwa pale mkwaju wa chini uliopigwa na Paul Scharner ulipopanguliwa na mlinda mlango Tim Howard.
Fulham ilimaliza nuksi ya kupoteza michezo mitatu mfululizo ya ligi baada ya kujipatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Norwich City.
Alikuwa Clint Dempsey aliyeunasa mpira vizuri na kuutumukiza wavuni kabla mlinda mlango wa Norwich John Ruddy kushindwa kuzuia mkwaju wa Bryan Ruiz.
Hadi robo ya kwanza ya mchezo Fulham walikuwa tayari wameshaweka kibindoni mabao mawili.
Fulham mara mbili mikwaju yao iligonga mwamba kutokana na mashuti ya Dempsey na baadae Alex Kacaniklic - lakini mkwaju wa Aaron Wilbraham uliomgonga mchezaji wa Fulham kujaa wavuni na kuipatia Norwich bao la kufutia machozi.
Wigan imeendelea kuwa nafasi ya hatari ya kushuka daraja lakini imefanikiwa kusogea pointi tatu mbele na kuwa sawa na Blackburn nafasi ya 17 baada ya kuilaza Stoke City kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wao wa DW Stadium.
Bao la kichwa kipindi cha pili la Antolin Alcaraz liliwapatia Wigan nafasi ya kuongoza.
Ryan Shawcross alipata nafasi nzuri ya kuifungia Stoke kwa kichwa lakini mlinda mlango wa Wigan Ali Al Habsi aliokoa.
Jean Beausejour aliipotezea nafasi nzuri Wigan, kabla Victor Moses kuifungia Wigan bao la pili dakika za mwisho za mchezo.
Matokeo hayo maana yake Wigan imekusanya pointi 28, sawa na QPR pamoja na Blackburn wakiwa juu yao.
Wolves imezidi kudhoofishwa baada ya kuongoza kwa bao moja ikajikuta ikipokea kichapo kutoka kwa Bolton na kujiongezea dhiki mkiani mwa ligi.
Michael Kightly aliipatia bao la kwanza Wolves wakiwa nyuma kwa pointi sita mkiani huku michezo iliyosalia ni sita kabla msimu haujamalizika.
Lakini Martin Petrov akaisawazishia Bolton kwa mkwaju wa penalti baada ya Roger Johnson kumchezea rafu Mark Davies na baadae Marcos Alonso akaipatia Bolton bao la pili na ubao kusomeka mabao 2-1 kwa Bolton.
Kevin Davies aliifungia Bolton bao la tatu kabla Wolves kupata bao la kufutia machozi dakika za mwisho kupitia kwa Matt Jarvis.
Muda unazidi kwenda kwa kikosi cha meneja wa Wolves Terry Connor ambacho hakijashinda katika mechi zake 10 zilizopita.
Connor, bado anahitaji ushindi wake wa kwanza tangu alipochukua hatamu za umeneja. Wolves waliongoza kipindi cha kwanza lakini iliwawia shida kutumbukiza mpira wavuni

PICHA YA LEO; KABURI LA MBWA HUKO NACHINGWEA.

Hili linaloonekana hapa ni kaburi la Mbwa wa Mzungu mmoja aliyejulikana kwa jina la Phills aliyewahi kuishi hapa Tanzania wilayani Nachingwea akifanya shuguli zake za kilimo cha karanga miaka ya 1950. Kaburi hili lipo maeneo ya Boma  Airport Road hapa mjini Nachingwea na limejengewa vizuri kwa zege imara ingawa limeanza kuhujumiwa kwa kuondolea kibao cha shaba kilichokuwa kinaelezea jina la mbwa huyo na uzio mdogo kubomolewa. 
Kwa nini mbwa ajengewe kaburi zuri la kudumu kama binadamu!!?
Mbwa huyu alikuwa maarufu enzi hizo kwani alikuwa msaidizi mkubwa kwa kazi za nyumbani za Mzungu Phills ikiwemo ulinzi wa makazi pia kutumwa sehemu mbalimbali ikiwemo sokoni kununua bidhaa.
Mbwa huyo marehemu alikuwa na akili za kuweza kwenda sokoni akiwa na kikapu na pesa na maelekezo ya maandishi ya bidhaa za kununua na duka au kibanda husika cha sokoni, muuzaji husoma maelekezo na kumpatia mbwa bidhaa kwenye kikapu shingoni hata kama ni nyama na huzifikisha kwa mwenyewe aliyemtuma ambaye ni Mzungu Phills. Baada ya kifo chake mzungu alihudhunika sana na kuamua kujenga kaburi zuri la kumbukumbu ya Mbwa wake ambalo lipo hadi leo maeneo ya Kilimani Boma Nachingwea. 

Jumatano, 28 Machi 2012

TAKUKURU NACHINGWEA YAHAMASISHA WANAMICHEZO KUPAMBANA NA RUSHWA MICHEZONI.

Kaimu Kamanda wa TAKUKURU wilayani Nachingwea Nd. Zablon Ernest Ombory akiongea na viongozi wa Chama cha Mpira wa miguu wilayani Nachingwea (NAFA), wachezaji wa timu ya African Boys ya Rwangwa naTimberland almaarufu Kipande cha Ulaya ya Nachingwea pia waamuzi wa mchezo huo juu ya umuhimu wa michezo na mapambano ya rushwa michezoni kabla ya mechi kuanza katikati  ya mwezi huu.
Mgeni Rasmi akikagua wachezaji na waamuzi kabla ya mechi kuanza.

Mwenyekiti wa NAFA akiwaongoza wageni kurudi jukwaa kuu ili kuangalia burudani ya mchezo ambao uliishia kwa timu ya Timberland ya Nachingwea kuifunga African Boys 3-2. Waamuzi walikuwa Ndg. Chacha( kushoto) mwamuzi wa kati, Ndg. Ashomile na Malebo wakishika vibendera na Kamisaa toka Lindi.
Wageni jukwaani toka kushoto ni Afisa utamaduni wilaya ya Nachingwea Ndg. Mkungwi, Mweka Hazina wa NAFA Ndg. Nyoni, Kaimu Kamanda TAKUKURU Ndg. Ombory, Afisa wa TAKUKURU Ndg. Hassan na Hakimu Mfawidhi Mh. Hemela.
Wachezaji wa Timberland wakiwa mapumzikoni.

Wachezaji wa African Boys ya Rwangwa wakiwa mapumzikoni.

Jumatano, 21 Machi 2012

JIFUNZE JINSI YA KUONGEZA KIPATO KWA KUBLOG.

Zipo njia mbalimbali za kujiingizia kipato kupitia blogu au tovuti.

Njia hizo ni pamoja na kuuza vitu unavyotengeneza mwenyewe, kuuza vitabu unavyoandika, kuuza makala zako, kutoz kiasi fulani cha malipo kwa kutangaza au kuuza vitu vya watu wanaohitaji kuvitangaza/kuviuza kupitia intaneti, kutengeneza blogu/tovuti za wengine kutokana na ujuzi wako, kuweka matangazo ya makampuni (ndege, hoteli, vinywaji, michezo, benki, nk.) au asasi, chama au Serikali, kuingia mkataba wa kupata malipo kupitia mpango unaofahamika kama "affiliate program" kutoka kwa wenye tovuti wengine wanaohitaji kujitangaza kwenye blogu/tovuti yako, kupokea matangazo kupitia makampuni yanayohusika na biashara ya matangazo kama vile Google Adsense/Adword, AdBrite,  Bidvertiser, Chitika, Infolinks, Kontera, Clicksor, Oxygen, AdBull n.k.

Leo nitazungumzia AdSense ambayo maelezo kwa lugha ya kiingereza yanapatikana: 
google.com/adsense...tour

AdSense ni programu ya Google ambayo mtu yeyote mwenye blogu/tovuti anaweza kutuma maombi ya kujiunga nayo na ikiwa vigezo vitatimizwa, ataruhusiwa kujiunga na kisha kupata maelekezo kutoka kwa watu walio kwenye timu ya AdSense wanaoelekeza hatua za kufanya hadi kufanikisha kuyaweka matangazo kwenye blogu/tovuti.

Ili kujiunga na programu ya AdSense, fuata linki hii: 
google.com/adsense

Baada ya kujiunga utakuwa na fursa ya kuchagua aina ya matangazo unayotaka yaonekane kwenye tovuti yako. Mathalani tovuti yako inahusu mitindo ya mavazi na usingependa kuona habari za mambo ya siasa au dini, basi unao uchaguzi huo.

Vile vile upatapa fursa ya kuchagua ukubwa wa matangazo kulingana na ukubwa wa nafasi kwenye blogu yako. Vipo vipimo mbalimbali kama vile 600 x 200 au 300 x 250 au 120 x 120 ama 728 x 90 n.k kama vilivyoorodheshwa:  
google.com/adsense, na pia utaviona punde unapoandaa matangazo kabla ya kupata "code" kwa ajili yakuweka kwenye blogu yako. Video ya jinsi yakuandaa matangazo hayo imepachikwa hapo chini.

Kielelezo cha picha kifuatacho kinaonesha maeneo muhimu katika uso wa blogu/tovuti ambapo matangazo yakiwekwa huonekana kirahisi na wasomaji. Kielelezo hiki kimetengenezwa kutokana na utafiti uliofanyika kuona macho ya wasomaji huona na kubofya wapi zaidi wanapotembelea blogu/tovuti. Sehemu zilizoandikwa "hot" na "warm" ndizo za kuzingatia.

Pia unaweza kutizama video 
youtube.com/optimization ili kuona mfano halisi wa upangaji unaolipa zaidi.
Picture
picha toka squidoo.com
Kuna video zimeandaliwa na timu ya AdSense kwa ajili ya kukusaidia kujifunza zaidi, video mbili zimepachikwa hapo chini. Ukitaka kutizama video nyingine tumia linki hii:  youtube.com/user/InsideAdSense/videos

Baadhi ya tovuti/blogu zina 'host' ambaye amerahisisha uwezo wa kutumia matangazo ya AdSense hivyo unaweza usihitaji kutengeneza mwenyewe, ila utahitaji kujua ikiwa host wako anahitaji kupata kiasi fulani cha malipo yako kwa kuwa ana-host blogu/tovuti yako bure au kama unaweza kulipia gharama za ku-host na hivyo kumzuia asichukue malipo yako yoyote ya AdSense. Wapo host wengine hawaruhusu kabisa matangazo ya AdSense hadi utakapolipia gharma za ku-host tovuti/blogu. Maelezo hayo mwulize/utayapata kwa kusoma maelezo ya-host wako. 

Watumiaji wa Blogger/Blogspot wamerahisishiwa zoezi hili na host wao (Google Blogger/Blogspot). Baadhi ya wenye blogu kupitia blogger/blogspot tayari wanatumia matangazo haya, baadhi yao wanafahamu sababu ya uwepo wa matangazo hayo, wengine kwa kujua hawayatumii. Wengine wanajua ila kwa haipo njia ya kufanikishiwa malipo yao, wanaona haja ya kuweka Adsense; Mimi ninawashauri wasiokuwa na ufumbuzi wa jinsi ya kufanikishiwa malipo yao, basi wasiache kutangaza, bali waendelee tu na inawezekana siku moja wakapata ufumbuzi kupitia Google AdSense au kupitia rafiki/ndugu/jamaa ambaye atakuwa tayari kuingia nao ubia na kupokea fedha kwa niaba yao. Nitafafanua kuhusu hili kwenye toleo linalofuatia kuhusu malipo (usikose kuperuzi siku zijazo kulisoma).

Ikiwa una blogu na Blogger/Blogspot, tumia linki ifuatayo kufuata maelekezo:  
youtube.com/watch...blogger  
Leo nakomea hapa. Matoleo yanayofuatia nitazungumzia kuhusu mfumo wa malipo yako na miiko ya AdSense


Source: http://www.wavuti.com/

MCHEZAJI WA BOLTON WONDERERS ALIYEZIMIA UWANJANI SASA APATA FAHAMU

Muamba anatambua familia


Fabrice Muamba
Fabrice Muamba sasa anaweza kutambua familia na jamaa zake na hata kuweza kujibu maswali. Hii ni kwa mujibu wa wakuu wa kilabu yake Bolton Wonderers pamoja na madaktari.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23, pia anaweza kupumua bila usadizi wa mashine , lakini hali yake ingali mbaya kiasi cha kusalia katika chumba cha wagonjwa mahututi.
Mwamba alianguka uwanjani na kuzimia mnamo Jumamosi wakati wa mechi kati ya klabu hiyo na Spurs.
Moyo wake Ulisimama kwa masaa mawili lakini tangu hapo ameanza kuonyesha dalili za kuimarika kiafya.
Madaktari wamesisitiza kuwa hali ya Muamba sio mahututi lakini ni mbaya.
Muamba anaweza kuinua mikono yake na miguu, ingawa madaktari hawawezi kuelezea kuhusu hali yake ya baadaye kwa sasa.
Mchezaji huyo aliwahi kuchezea timu ya taifa ya Uingereza ya vijana walio chini ya umri wa miaka 21

AMINI USIAMINI,SIMBA ATIMULIWA NA SWALA MWEUSI HUKO MASAI MARA

Role reversal in Maasai Mara: Waterbuck scares off hungry lioness who was lining him up for dinner

By Jill Reilly
Sometimes no matter how loud you roar, it just isn't scary enough, as this African lioness found out in a Kenyan national reserve.
She spotted a waterbuck bathing in the cool water and deciding he was going to make an easy meal, she edged her way up to the side of the pond.
As she approached the brown, antlered animal, he looked up and surprisingly did not back away.
Time for tea: When the Africa Lioness spotted a Waterbuck bathing in the cool water, she decided he was going to make an easy meal, and edged her way up to the side of the pond
Time for tea: When the African lioness spotted a waterbuck bathing in the cool water, she decided he was going to make an easy meal, and edged her way up to the side of the pond

Bravado: A stony stand-off ensued, with both animals staring at each other, refusing to budge. The suddenly he decided to pounce and charged at the Lioness, with his lethal horns first
Bravado: A stony stand-off ensued, with both animals staring at each other, refusing to budge. The suddenly he decided to pounce and charged at the lioness, with his lethal horns first
A stony stand-off ensued, with both animals staring at each other, refusing to budge - the lioness bared her teeth, but the waterbuck put forward his horns.
Suddenly he decided to pounce and charged at the Lioness, with his lethal horns first.
 With a split-second pause, she whipped around and sprinted up the grassy bank to safety - although she was lucky not to have been caught on his antlers which can reach up to 40 inches (101cm).
The waterbuck is generally a quiet and sedentary animal, although males do compete for and hold territories as this shaggy-haired animal showed.
Despite its name, the animal is not truly aquatic and does not make tend to spend too much time in water and swamps.
It does, however, take refuge there to escape predators, which may explain why the animal was in the pond in the first place.
The bravado stand off took place in Maasai Mara National Reserve, Kenya, which lies about 270 kilometres (167 miles) from the country's capital Nairobi.
The African Lioness was a Panthera Leo and females are usually responsible for most of the hunting, while the male of the species have earned the King of the Jungle title.
They consume a wide variety of prey, from wildebeest, impala, zebra, giraffe, buffalo and wild hogs to sometimes even larger beasts such as rhinos and hippos.
Scaredy cat: With a split-second pause, she whipped around and sprinted up the grassy bank to safety - although she was lucky not to have been caught on his antlers which can reach up to 40 inches (101cm)
Scaredy cat: With a split-second pause, she whipped around and sprinted up the grassy bank to safety - although she was lucky not to have been caught on his antlers which can reach up to 40 inches (101cm)

I'll show you: The Waterbuck is generally a quiet and sedentary animal, although males do compete for and hold territories as this shaggy-haired animal showed
I'll show you: The waterbuck is generally a quiet and sedentary animal, although males do compete for and hold territories as this shaggy-haired animal showed

Standing his ground: After the African Lioness beat a hasty retreat, the Waterbuck stayed in the water
Standing his ground: After the African Lioness beat a hasty retreat, the defiant waterbuck stayed in the water


Read more: http://www.dailymail.co.uk/news/article-2117717/Role-reversal-Maasai-Mara-Waterbuck-scares-hungry-lioness-eyeing-dinner.html#ixzz1pjRsEPVW

Jumanne, 20 Machi 2012

PICHA YA LEO; MAJ. JENERALI SAMWEL NDOMBA NI MKUU MPYA WA JKT.







Mh. Rais Kikwete akiwa pamoja na Mkuu mpya wa JKT kulia Maj. Gen. Samwel Ndomba mara baada ya kumwapisha hivi karibuni, kushoto ni Mkuu wa Majeshi ya Tanzania Generali Mwamunyange.

MWAKYEMBE ASEMA AMEPONA UGONJWA ULIOMSUMBUA.


Naibu Waziri wa Ujenzi Dk. Harrison Mwakyembe, akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, muda mfupi baada ya kuingia ofisini humo kuanza kazi, kutokana na afya yake kuimarika. Mwakyembe amekuwa akitibiwa nchini India kwa muda mrefu. Picha na Zacharia Osanga
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, Dk Mwakyembe akiwa amevalia kofia ya pama alisema: “Si kwamba sijambo, bali nimepona kabisa baada ya kugundulika na maradhi hayo na kutibiwa.”


BAADA ya utata wa muda mrefu wa ama Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe amelishwa sumu au la, jana Mbunge huyo wa Kyela, aliweka hadharani ugonjwa wake akisema unafahamika kitaalamu kwa jina la Popular Scleroderma huku akisisitiza: “Sasa nimepona kabisa.”


Dk Mwakyembe amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya ngozi ambayo mwaka jana yalizidi kumtikisa na Oktoba 9, Serikali iliamua kumpeleka Hospitali ya Appolo, India kwa ajili ya matibabu na uchunguzi zaidi.


“Nimerudi juzi kutoka India na daktari wangu ameniambia nimepona, nilikuwa nasumbuliwa na maradhi ya ‘Popular Scleroderma’ iliyosababisha ‘skin disorder’ (ngozi kutokuwa katika hali ya kawaida), lakini kwa nguvu za Mungu nimepona, namshukuru Mungu.”


Kuhusu sumu
Alipoulizwa kuhusu tuhuma za kulishwa sumu, Dk Mwakyembe alikataa kuzungumzia hilo akisema anasubiri uchunguzi ulioagizwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha.


Hata hivyo, Dk Mwakyembe alisema angependa kuona uchunguzi huo unakamilika haraka na ripoti yake inatangazwa kwa umma.


Alisema yuko tayari na anasubiri tume hiyo ya uchunguzi iliyoundwa na Waziri Nahodha imhoji ili atoa kile kilichomo katika ripoti ya daktari wake.


Dk Mwakyembe alisema anachoshukuru hadi sasa ni kwamba afya yake imeimarika kutokana na shinikizo la Rais Jakaya Kikwete ambaye aliagiza Serikali kumpa kipaumbele wakati wote akiwa nchini na India hatua ambayo imemwezesha kufika hapo alipo.


Kutokana na hali hiyo, Dk Mwakyembe aliwataka wananchi wote wakiwemo wa jimboni kwake Kyela kuondoa wasiwasi akisema sasa yupo imara kwa ajili ya ujenzi wa majukumu ya taifa.


“Ninaomba wapiga kura wangu wa Kyela waache jazba, wawe na subira juu ya matatizo yangu. Wiki ijayo nitakwenda kuzungumza nao ili niweze kuwaeleza matatizo yaliyokuwa yananisumbua, lakini sasa hivi niko fit,” alisema.


Mtaalamu auzungumzia
Mtaalamu wa afya ambaye hakutaka kutajwa gazetini alisema ugonjwa huo wa ‘Popular Scleroderma’ unasababishwa na chembechembe hai nyeupe kushambulia kitu kigeni kilichoingia kwenye mwili na kusababisha magonjwa ya ngozi.


Alisema chembechembe hizo zinaweza kusababisha ngozi ya mwili kuharibika... “Ni magonjwa yanayosababishwa na chembechembe hai nyeupe kujikataa zenyewe na kusababisha ugonjwa wa ngozi na mifupa.”
Kauli hiyo ya Dk Mwakyembe kuhusu ugonjwa wake imefungua ukurasa mpya hasa baada ya baadhi ya wanasiasa kuamini kuwa hakuwa na tatizo jingine bali, amelishwa sumu. Tayari Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba ambaye alitoa ripoti akisema Naibu Waziri huyo hakulishwa sumu kama inavyodaiwa, amefanyia uchunguzi madai hayo na kukabidhi jalada lake kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma, DPP ili afungue kesi.

Kauli ya Sitta

Mmoja wa wanasiasa waliodai kuwa Dk Mwakyembe amelishwa sumu, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta alipoulizwa jana juu ya kauli hiyo mpya ya Dk Mwakyembe alisema hana cha kuzungumza.


Januari 28, mwaka huu akiwa kwenye uzinduzi wa Programu ya Neno la Hekima kutoka kwa Kiongozi iliyoanzishwa na Kanisa la Ufufuo na Uzima la Kawe, Dar es Salaam Sitta alisema Dk Mwakyembe amelishwa sumu.


Akizungumza kwa utaratibu, Sitta alisema hana mengi ya kuzungumza kuhusu ugonjwa unaomsumbua Dk Mwakyembe na kusisitiza kuwa isubiriwe ripoti kutoka India ambako alikuwa akitibiwa.


“Dk Mwakyembe si anatibiwa India?,” alihoji na kuendelea, “Nadhani umeshapata jibu, tusubiri… acha huko India waendelee na uchunguzi wao, siwezi kusema lolote zaidi ya hilo nililokuambia.”


Dk Mwakyembe alianza kuugua Oktoba 9, mwaka jana na alitibiwa Apollo hadi aliporejea Desemba 11, mwaka jana. Alirejea tena India kuendelea na matibabu hadi Ijumaa iliyopita aliporudi na kusema kuwa amepona.


Matatizo yake ya kiafya yamesababisha mvutano baina ya viongozi wa Serikali. Wakati Manumba akisema ripoti kutoka Wizara ya Afya ilionyesha hakupewa sumu, waziri mwenye dhamana na afya Dk Haji Mponda alimkana.


Pia Waziri Nahodha ambaye ana dhamana na jeshi hilo la polisi, alikana ripoti hiyo ya DCI Manumba na kutaka aulizwe mwenyewe alikoitoa huku akisema uchunguzi alioagiza bado unaendelea

MAMA NA WANAE WASAULA NGUO MBELE YA SHULE, WAKAMATWA NA POLISI.



NewsImages/6316130.jpg
Mama na wanae walipoamua kumwaga radhi shuleni
Tuesday, March 20, 2012 1:33 AMMama mmoja na wanae wa kike na wa kiume wanashikiliwa na polisi nchini Marekani baada ya kusaula nguo zao zote na kuanza kusali mbele ya shule wakiwa uchi wa mnyama.
Polisi wa kitongoji cha Upper Darby kwenye jimbo la Philadelphia nchini Marekani wanamshikilia mama mmoja na wanae kwa kusali uchi wa mnyama mbele ya shule.

Taarifa ya polisi wa Upper Darby ilisema kuwa mama huyo mwenye umri wa miaka 43 aliyejulikana kwa jina la Sara Butler akiwa na wanae wa kike Joanne mwenye umri wa miaka 23 na Bessie mwenye umri wa miaka 22 pamoja na mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka 14 walisaula nguo zao zote na kuanza kusali kwenye maegesho ya magari mbele ya shule.

Taarifa zaidi zilisema kuwa awali siku ya tukio, mama huyo na wanae walifika kwenye shule ya sekondari ya Upper Darby High School wakitaka kumuona mmoja wa wanafunzi wa kiume. Walikataliwa kukutana naye kwasababu mama huyo si mzazi wake.

Mama huyo na wanae waliondoka na kurudi baada ya lisaa limoja na kuanza kusaula nguo zao mbele ya maegesho ya magari wakisali kwa kusauti wakimtaja Yesu Kristo.

Ili waonekane vizuri mama huyo na wanae walijaribu kupanda juu ya gari walilokuja nalo lakini polisi walioitwa eneo la tukio waliwahi kuwatia nguvuni mama na wanae.

Mama huyo na wanae wanaozidi umri wa miaka 18 walifunguliwa mashtaka ya kuvunja maadili ya jamii na kujianika uchi hadharani

Ijumaa, 16 Machi 2012

MANCHESTER CITY NA UNITED ZATOLEWA NJE YA EUROPA CUP.

Miserable night for Manchester as City and United both crash out of Europe

By John Edwards
There was misery in Europe again for Manchester on Thursday night, as both United and City crashed out for the second time this season.Following their Champions League heartbreak in December, the Barclays Premier League title rivals saw their Europa League hopes end in the last-16 knockout stage.
Spanish inquisition: Rooney and Giggs can't believe it
Spanish inquisition: Rooney and Giggs can't believe it
United were always up against it at Athletic Bilbao, after being embarrassed by the Basques at Old Trafford, and went out 5-3 on aggregate after losing the return leg 2-1.
City, who trailed 1-0 to Sporting Lisbon after the first match, at least came close. Two second-half goals from Sergio Aguero and one from Mario Balotelli saw them go out on away goals after Matias Fernandez and Ricky van Wolfswinkel had scored for the away side.
City manager Roberto Mancini accepted all the blame for his side's Europa League exit.
He said: 'In the first half we didn't play, but I am the manager and it's not the players' fault, but mine - I probably made a mistake.
Crashing out: Man United
Embarrassing: United went out without a fight
'The players did everything, and fought on the pitch.
'When a manager doesn't prepare well for the game, this happens.
'When I lose a game I think about why I lost and think about where I made mistakes.
'I understand we have big players but in football every game is difficult, and in the Europa League and Champions League it is more difficult, because every team plays to win.
'Sometimes we make mistakes, but the manager is the person who always prepares the game, and I probably made some mistakes for these two games.'
City slackers: Mancini's side were 2-0 down at half-time
City slackers: Mancini's side were 2-0 down at half-time
Mancini's comments were similar to remarks he made after an unexpected Barclays Premier League defeat at Everton in January, when he blamed poor preparation.
City now only have their title challenge to concentrate on and, after losing top spot in the table last weekend, must now look to get back on track against Chelsea next Wednesday.
Mancini said: 'I am proud for the second half because we had a fantastic 45 minutes, but I am very sorry for the players and our supporters because they were fantastic in that second half.
'But I am disappointed in myself, not the players.
'For the second time this year, I hope I don't make mistakes against Chelsea

Read more: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2115557/Manchester-City-Manchester-United-crash-Europe.html#ixzz1pGznmtiT

JK ATEUA WAKUU WA MIKOA WAPYA.

WAKUU wa mikoa mipya ambayo hivi karibuni ilitangazwa katika gazeti la serikali wameteuliwa jana na wanatarajiwa kuapishwa wiki ijayo, Machi 21 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ikulu walioteuliwa ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Dk. Rajab Rutengwe ambaye sasa atakuwa mkuu wa mkoa wa Katavi na Magalula Saidi Magalula atakayekuwa mkuu wa mkoa wa Geita.

Awali Magalula alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi. Wengine ni Paschal Mabiti atakayekuwa Mkuu wa Mkoa wa SIMIYU na Asery Msangi mkoa wa Njombe.

Kabla ya hapo Mabiti alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Singida na Msangi Mkuu wa Wilaya ya Iringa.

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais imesema kwamba uteuzi huu umeanza jana Machi 15, 2012

ABIRIA WENGINE NUKSI KWELI, WANAKUZUSHIA JAMBO UTASHANGAA.

BAE KUNUNUA VITABU KWA PESA YA RADA.

BAE yanunua vitabu pesa za Rada Tanzania

Moja ya ndege za BAE, itainunulia Tanzania vitabu vya elimu kwa fedha za rada
Kampuni ya kuuza vifaa vya kijeshi ya BAE Systems itatoa takriban £29.5m kwa miradi ya elimu nchini humo kufuatia makubaliano na Taasisi ya Kupambana na ufisadi ya Uingereza (SFO).
BAE ilipigwa faini ya £500,000 mwaka 2010 kwa kushindwa kutunza rekodi zake za malipo iliyofanya kwa mshauri wake.Malipo hayo yalitolewa kununua rada ya kijeshi kwaTanzaniakwa gharama ya £28m.
Kampuni hiyo ya BAE sasa imethibitisha makubaliano ambayo yatatumika kusaidia watanzaniakamailivyoafikiwa.
Itanunua vitabu vya kiada kwa shule 16,000 vya masomo muhimu ya Kiswahli, Kiingereza, Hisabati na Sayansi.
Fedha hizo pia zitatumika kuwapatia miongozo walimu na mwongozo wa muhtasari wa masomo kwa waalimu wote 175,000 wa shule za msingi, na muhtasari yenyewe, kampuni hiyo ya ulinzi imesema.
Taasisi ya SFO ilisema makubaliano hayo yalikuwa ya kwanza na ya aina yake, lakini ilikosolewa na jaji aliyetoa uamuzi wake kwa kampuni hiyo miaka miwili iliyopita.
"Makubaliano haya ni ya kwanza kwa SFO ambayo iliratibu kutumia mfumo wa sheria za Uingereza,’ mkurugenzi wa SFO Richard Alderman alisema.
'hatma ya jambo lenyewe'
"Tumefurahi kuwa hatimaye tumefikia mahali tunaweza kutoa malipo kwa serikali yaTanzaniana kufikia tamati ya suala hili." BAE ilisema.
BAE iliafikiana na SFO mpango huo mwaka 2010. Ilikubali kulipa faini ya na gharama ya £225,000 kwa SFO – na faini ilikokotolewa kutoka £30m iliyotoa kwa watanzania kumaliza kesi hiyo.
Wakati huo jaji wa mahakama ya Southwark Crown alikosoa makubaliano hayo kati ya SFO na BAE.
"Muundo wa makubaliano hayo unaweka shinikizo la kimaadili kwa mahakama kuifanya faini hiyo iwe kwenye kiwango cha chini kwa ajili ya maandalizi ya juu. " alisema Justice Bean, aliyeongeza kuwa alikuwa kwenye shinikizo la kuiweka faini ya mahakama kuwa ya chini.
Pia alikosoa sehemu nyingine ya makubaliano ambayo alisema yalimpa mjumbe yeyote wa kampuni ya BAE Systems "kinga kwa makosa yote yaliyofanywa nyuma yawe yamewekwa wazi au la".
Kampuni hiyo ililipa £7.7m kwa kampuni mbili zinazomilikiwa na mfanyabiashara Shailesh Vithlani kabla hata ya kushinda zabuni yenyewe ya kununua rada.

Jumamosi, 10 Machi 2012

WANANCHI NA WANAHARAKATI WAPINGA MGOMO WA MADAKTARI.

DAKTARI mstaafu, Dk. Nyamaroko Khalfani, amebeza kitendo cha madaktari nchini kugoma, akisema daktari wa kweli na aliyekula kiapo cha kazi hiyo, hawezi kugoma, labda iwe kwa maslahi binafsi.

Dk. Khalfani aliyestaafu mwaka 2002 alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari wakati Kamati ya Wanaharakati Wazalendo ilipotoa tamko kuhusu maandamano yanayotarajiwa kufanyika kesho Dar es Salaam, kupinga mgomo huo.

Kutokana na kufahamu uzito wa kiapo cha madaktari, alisema anaungana na wanaharakati hao kupinga mgomo huo kwani ni kinyume na wajibu wa kitaaluma.

“Mimi ni daktari, nimefanya kazi sana Tarime Vijijini; kwa kweli si rahisi kwa taaluma yetu kugoma, ila kwa sababu ya maslahi binafsi ndiyo maana madaktari wa sasa wanagoma…daktari halisi na aliyekula kiapo cha kazi, si rahisi kugoma kama wanavyofanya hawa,” alisema.

Alisema madaktari wengi sasa ni vijana ambao wako kimaslahi zaidi kuliko kuzingatia wajibu na taaluma inavyowataka na ndiyo maana wanajiangalia badala ya kuangalia haki za wagonjwa ambao wanahitaji huduma ya tiba kutoka kwa wataalamu hao.

“Nawashutumu kwa hatua yao hiyo, kwani si jambo zuri na linaweza kuja kuvunja kabisa hali ya amani na usalama wa Taifa … jambo la msingi warudi kwanza kazini kuhudumia wagonjwa wakati madai yao yakishughulikiwa na Serikali ambayo imeshaonesha nia ya kufanya hivyo,” alisema Dk Khalfani.

Katibu wa Kamati hiyo, Salum Hapi, alisema maandamano hayo yataanzia Manzese Bakhresa hadi viwanja vya Jangwani na yatashirikisha wananchi wazalendo, wakiwamo wagonjwa.

Ijumaa, 9 Machi 2012

MAHAKAMA YA KAZI YATOA AMRI KUSITISHA MGOMO WA MADAKTARI

Kwa: Wahariri wote; TV, RADIO, MAGAZETI, BLOGU,

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, leo (Alhamisi Machi 8, 2012) imetoa uamuzi wa kusitishwa mara moja kwa mgomo wa Madaktari ulioitishwa nchi nzima tangu jana (Jumatano Machi 7, 2012).

Katika amri yake ya pili, Mahakama Kuu pia imekitaka Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari kuwatangazia wanachama wao mara moja kupitia Vyombo vya Habari kusitishwa kwa mgomo huo nchi nzima kama
walivyowatangazia wakati wanauitisha mgomo wenyewe.

Mahakama Kuu pia imeamuru pande zote mbili, yaani Serikali kwa upande mmoja na Chama cha Madaktari na Jumuiya ya Madaktari, kwa upande mwingine, kutumia fursa zilizopo katika kutatua mgogoro wa kikazi uliopo kati yao kwa
haraka.

Uamuzi huo wa Mahakama Kuu imetolewa na Jaji R.M. Rweyemamu, baada ya kusikiliza ombi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali dhidi ya Chama cha Madaktari na Jumuiya ya Madaktari kuitaka itoe zuio kwa mgomo huo.

Akitoa uamuzi huo, Jaji Rweyemamu alisema anazingatia madhara ambayo mgomo huo ungeleta kwa jamii kwa vile huduma za tiba ambazo madaktari walitaka kugoma kuzitoa ni miongoni mwa huduma muhimu zilizotajwa kwenye Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, Namba 6 ya Mwaka 2004.

Uamuzi huo, ni kama ifuatavyo:

Leo, tarehe 8, Machi 2012, Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, mbele ya Jaji R.M. Rweyemamu, baada ya kusikiliza Ombi No. 24 la 2012 lililowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Mwombaji) dhidi ya Chama cha Madaktari
Tanzania na Jumuiya ya Madaktari (Walalamikiwa), imetoa uamuzi ufuatao:

i) Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari pamoja na Wanachama wao, kusitisha Mgomo waliouanzisha rasmi tarehe 7 Machi 2012 nchi nzima na kurejea kazini mara moja kwa kuendelea na kazi zao kama kawaida, mara tu Amri hii itakapowafikia. Aidha, waombaji watatakiwa kutoa Kiapo cha kuthibitisha kwamba wamewasilisha Amri hiyo kwa Walalamikiwa na kuwasilisha Kiapo hicho Mahakama Kuu – Divisheni ya Kazi kesho tarehe 9, Mach 2012.

ii) Mara baada ya Amri hii kuwasilishwa kwa Walalamikiwa (Chama cha Madaktari Tanzania na Jumuiya ya Madaktari) watatakiwa kuwatangazia Wanachama wao kupitia Vyombo vya Habari kusitishwa kwa Mgomo huo Nchi nzima kama walivyowatangazia wakati wa kuitisha Mgomo huo;

iii) Mahakama inaamuru pande zote mbili (Serikali na Chama cha Madaktari Tanzania pamoja na Jumuiya ya Madaktari) kutumia fursa za Kisheria zilizopo katika kutatua Mgogoro wa Kikazi uliopo kati yao kwa haraka.

(mwisho)

Imetolewa na:

Ofisi ya Waziri Mkuu,
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM.

Alhamisi Machi 8, 2012

MANCHESTER UNITED YAFUNGWA 3-2 NA ATHLETIC BILBAO

Manchester United 2 Athletic Bilbao 3: Reds face the boot as sleepy Rafael nods off

By Chris Wheeler
Wake up was Sir Alex Ferguson's pre-match message to Manchester United, but his players clearly weren't listening.
Certainly not young Rafael Da Silva who may live to regret the moment he inexplicably switched off for the goal that could cost Ferguson's side a place in the quarter-finals of the Europa League.
So much for rubbing our hands in anticipation of an all-Manchester final in Bucharest in May.
Leveller: Llorente brought the visitors on terms just before half-time
Leveller: Llorente brought the visitors on terms just before half-time

MATCH FACTS

Man United: De Gea, Rafael Da Silva, Smalling (Carrick 55), Evans, Evra, Park (Anderson 61), Jones, Giggs (Nani 75), Young, Rooney, Hernandez.
Subs not used: Amos, Ferdinand, Welbeck, Fabio Da Silva.
Goals: Rooney 22, 90 pen.
Athletic Bilbao: Iraizoz, Iraola, Javi Martinez, San Jose, Aurtenetxe, Iturraspe,De Marcos, Ander Herrera (Inigo Perez 84), Susaeta, Llorente (Toquero 81), Muniain.
Subs not used: Raul, David Lopez, Koikili, Ekiza, Ibai.
Booked: San Jose.
Goals: Llorente 44,De Marcos 72,Muniain 90.
Attendance: 62,000
Referee: Florian Meyer (Germany).
Quite what the young Brazilian was thinking when he watched the ball roll away from David de Gea and towards Iker Muniain in the 89th minute, only he will know but it summed up another lamentable defensive performance from the Barclays Premier League champions.
Wayne Rooney's injury-time penalty and a string of superb saves from United's own Spaniard De Gea have given United a lifeline they barely deserve when Ferguson's side go to Basque country next week.
But this was a depressingly familiar storyline for United in Europe this season. Leading at home once again, just as they were against Basle and Ajax two weeks ago, it all went downhill as an impressive Bilbao side hit back in stunning fashion.
A second successive European defeat at home again left Ferguson searching for an explanation. He took the blame after the Ajax loss, and questions must be asked after he recalled Rafael in another unfamiliar back four.
Wayne's world: Rooney bagged the opener for United (below) after 22 minutes and celebrates (above)
Wayne's world: Rooney bagged the opener for United (below) after 22 minutes and celebrates (above)

Wayne's world: Rooney bagged the opener for United (below) after 22 minutes and celebrates (above)

But surely his players have to hold their hands up this time. Bilbao were as brilliant as United were bad, and as vibrant as their 6,000 army of fans, even though it must be said that questions remain over two of their three goals.
Indeed, by the time United broke the deadlock in the 22nd minute it was the Spanish side who were looking most likely to open the scoring, with Fernando Llorente making a real nuisance of himself.
But they were caught unawares when Rooney was fouled just over the halfway line and took a quick free-kick to Ryan Giggs. The United veteran surged forward and exchanged a series of passes with Javier Hernandez, who checked back inside two defenders and tried his luck with a low left-foot shot.
Heads up: Llorente nodded the Spaniards' first goal of the evening
Heads up: Llorente nodded the Spaniards' first goal of the evening - much to the delight of the travelling fans (below)

Heads up: Llorente nodded the Spaniards' first goal of the evening - much to the delight of the travelling fans (below)
Goalkeeper Gorka Iraizoz got down to push it away but only as far as Rooney, who turned the ball into the empty net from close range. The England striker will score more difficult goals this season but credit to him for making up ground after starting the move.
Bilbao pressed forward undeterred and were certainly deserving of Llorente's equaliser in the 44th minute. Muniain was allowed to break forward from deep and feed the ball into 6ft 5in Spain striker Llorente, who knocked it on to Andoni Iraola.
He played it out to Markel Susaeta, whose first-time cross picked out Llorente's charging run as he burst between Rafael and Chris Smalling to plant a powerful header past De Gea


Read more: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2112331/Manchester-United-2-Athletic-Bilbao-3-Sir-Alex-facing-Euro-exit-home-woe.html#ixzz1ocGb4BcF

Jumatano, 7 Machi 2012

WAFANYAKAZI WA TAZARA WAGOMA

Mwl. Julius Nyerere na Rais kaunda wa Zambia wakati wa uzinduzi wa Reli ya TAZARA miaka ya 70.
WAFANYAKAZI wa Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA ), jana waligoma kuendelea na kazi.


Wamekitishia kusimamisha huduma ya usafiri wa garimoshi kwa kushinikiza kulipwa mshahara wao wa miezi miwili ya Januari na Februari; anaripoti Lucy Lyatuu.


Hata hivyo, Menejimenti ya Tazara imesema, tayari mshahara wa wafanyakazi hao wa Januari ulishalipwa na uliobakia utalipwa katika ya mwezi huu na hali hiyo inatokana na kushuka kwa uzalishaji wa shirika.


Akizungumza na wafanyakazi wa shirika hilo waliokusanyika katika eneo la kuondokea abiria jijini Dar es Saalam, Mwenyekiti wa Tawi la Chama cha Wafanyakazi wa Reli (TRAWU), Yassin Mleke alisema wafanyakazi wamechukua hatua hiyo kutokana na kutosikilizwa

ASKARI POLISI WAWILI WAFUKUZWA KAZI BAADA YA KUDAI RUSHWA.

Askari hao wamefukuzwa kazi kwa kubainika kutenda kosa ambalo ni kinyume na utendaji kazi wa jeshi hilo ambalo walidai fedha hizo kutoka kwa Jacqueline Komba ili waweze kumuonyehsa gari lake lililokuwa limeibiwa na majambazi

Askari waliofukuzwa kazi akiwemo Koplo David na Koplo Lufefe wote wa jeshi hilo na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela.

Januari 16 mwaka huu Jacqueline aliripoti katika kituo cha polisi cha Chuo Kikuuu kuibiwa gari lake aina ya Suzuki Swift lililokuwa na namba za usajili T311 BWU alikuwa ameliegesha karibu na eneo la Swimming Pool chuoni hapo.

Kamanda wa Kenyela alisema, baada ya siku moja Komba alipigiwa simu na askari mmoja kutoka kituoni hapo kumtaka atoe kiasi cha shilingi Milioni 3 ili wamuonyeshe gari lake lilipo na yeye akawaomba kuwa amepungukiwa na kuwaahidi kuwapa kiasi cha shilingi Milion 2.5 na askari hao wakakubali na kumuahidi aje siku iliyofuata yaani Januari 19 wakutane eneo la Mlimany City wakachukue fedha hizo

Jaqueline aliweza kuripoti kituo kingine cha UIrafiki na mtego uliwekwa na watuhumiwa hao waliweza kukamatwa Februari 7, mwaka huu


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela. 

Jumanne, 6 Machi 2012

CORRUPTION ALLEGATIONS HIT WWF IN TANZANIA.


By Kizito Makoye

DAR ES SALAAM (AlertNet) – The World Wide Fund for Nature (WWF) in Tanzania is embroiled in a corruption scandal over the alleged misappropriation of Norwegian aid aimed at helping civil society organisations build capacity, Norwegian and WWF officials said.

When Norway’s government learned of the irregularities it immediately suspended its funding to that project and to another $2.5-million REDD+ readiness project aimed at enhancing Tanzania’s capacity to deliver data on forest carbon stocks, said Naess Inger, the Norwegian embassy counselor on environmental issues.

The Tanzania country director of the well-known conservation group has since resigned.

An external auditing firm, Ernest & Young, has been brought in to carry out an investigation into the problems, WWF officials said.

The auditing firm’s initial report, seen by AlertNet Climate, suggests that a share of NOK 25million (approximately $1.3 million) injected by Norway into a project called ‘Strengthening Capacity of Environmental Civil Society Organizations’ has disappeared.

REDD - Reducing Emissions from Deforestation and Forest Degradation – is a U.N.-backed effort to protect tropical forests by having developed countries pay poorer countries to protect forest, in exchange for the richer countries receiving carbon emission reduction credits. REDD+ is a version of the effort that focuses on ensuring forest communities gain from such payments.

PAYMENTS SUSPENDED

“We have suspended all further disbursements to the two projects while awaiting receipt of the probe report by Ernst& Young … further decisions in line with our policy of zero tolerance of corruption will follow later,” Inger said.

According to Inger, the four-year capacity building programme, which started in 2008, was  aimed at empowering civil society organisations to help improve the contribution of fisheries, forestry and wildlife to national economic growth, poverty reduction and people’s livelihoods.

She said investigations are ongoing to determine how a large sum of money disappeared and to assess whether internal controls in the WWF system should be improved.

A final report from the auditor is expected to be completed soon, she said.

The director of WWF-Norway, Rasmus Hansson, confirmed that “per diem” expenses are central to the auditor’s investigation.

The allegations of fraud have emerged as part of an internal process, but stem from several sources, Hansson said in an email interview with AlertNet Climate. Suspicions were routinely reported on to the Norwegian Foreign Ministry's corruption unit, he said.

WWF-Norway has funded various types of training for Tanzanian environmentalists, including on lobbying political authorities. The courses offered have been organised by WWF-Tanzania, which was required to report back to WWF-Norway.

In December, the Norwegian Ambassador in Tanzania, Ingunn Klepsvikse, visited WWF-Tanzania to ask for documented evidence on the use of Norwegian taxpayers’ money. During this visit, the envoy expressed concern about the management of the Norwegian support and reported that the financial books she was shown were not in order, Inger said.

According to Inger, the largest expense items in the capacity building program have been for external lecturers, event expenses at hotels and various allowances for seminar participants, as well as grants to activities of organisations and youth groups.

She said WWF will take responsibility for paying back to the government of Norway any funds that have disappeared, but insisted the setback will not stop REDD projects in Tanzania or elsewhere.

"Norway is committed to assisting countries like Tanzania to prepare for a future international REDD+ mechanism and (we) expect all our partners to demonstrate good levels of governance in the management of programmes (and) projects," Inger said in a statement, adding that, “while this kind of incident is regrettable, it should not prevent the many other valuable initiatives from progressing for the overall benefit of Tanzanians.”

RESIGNATION AND FIRINGS

Amid mounting pressure, WWF’s Tanzania country director, Stephen Mariki, resigned on Feb. 14.

Sources in Dar es Salaam said a high-level delegation from the WWF regional office in Nairobi visited the WWF Tanzania office and pressed Mariki to resign.

“I have not done anything wrong myself but since this scandal happened under my leadership there was no option than to step aside” Mariki said in an interview with AlertNet Climate, shortly after his resignation.

“I have taken the right decision for the sake of my own respect.”

He blamed WWF-Norway for what he termed “blowing the issue out of proportion” while defending his record on fighting corruption as being in line with organisation policy.

According to Kimunya Mugo, the WWF Eastern and Southern Africa director of communications, the group has terminated the employment of eight people in connection with the fraud charges.

Kizito Makoye is a journalist based in Dar es Salaam, Tanzania
Source:
http://www.wavuti.com

Ijumaa, 2 Machi 2012

'ASKOFU' AKAMATWA KWA RUSHWA ARUSHA

Thomas Mollel almaarufu Askofu.
WAKATI mwanachama wa CCM, Siyoi Sumari, akitangazwa mshindi katika mzunguko wa pili wa kura ya maoni Arumeru Mashariki, mfanyabiashara maarufu mkoani hapa anayechimba, kuuza na kununua madini aina ya tanzanite, Thomas Mollel ‘Askofu’ amekamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za kutoa rushwa kwa madiwani.

Askofu huyo ambaye pia ni Diwani wa Mbuguni, Arumeru, alikamatwa usiku wa manane wa kuamkia jana kwa tuhuma hizo zinazohusiana na kura ya maoni ambayo ilipigwa jana na kumpa Siyoi ushindi wa kura 761 dhidi ya William Sarakikya ambaye alipata kura 361.

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, iliagiza kurudiwa kwa kura ya maoni ikihusisha wagombea hao baada yao na wengine waliojitokeza kutofikisha zaidi ya nusu ya kura za wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Jimbo la Arumeru Mashariki.

Katika kura hizo, Siyoi aliongoza kwa kupata kura 361 akifuatiwa na Sarakikya aliyepata kura 259. Kamati Kuu ilifanya uamuzi huo ili kupata mgombea ambaye atapata asilimia 50 au zaidi ya hapo.

Matokeo ya jana yalitangazwa na Msimamizi, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa. Wajumbe waliopiga kura walikuwa 1,124 ambapo kura mbili ziliharibika.

Askofu akamatwa Kuhusu Askofu kukamatwa, ilidaiwa kwamba alikutwa kikaoni akishawishi madiwani kwa rushwa ili wampigie kura ya maoni Siyoi, ili apate ridhaa ya CCM kugombea ubunge katika uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki.

Kamanda wa Takukuru wa Mkoa wa Arusha, Mbengwa Kasomambuto, alidai kwamba hadi jana walishamkamata Askofu na watuhumiwa wengine wawili.

Kasomambuto alidai kuwapo mtandao wa kutoa rushwa na kwamba Askofu alikabidhiwa kazi ya kushawishi kundi la madiwani hao na juzi juzi kukutana na baadhi yao kwenye kikao ambacho hakikuwa rasmi wala halali.

Aliwataja wengine waliokamatwa, kuwa ni Elirehema Kaaya ambaye awali aligombea katika mzunguko wa kwanza wa kura hiyo lakini alishindwa kwa kupata kura 205.

Ilidaiwa kuwa naye alihusika kushawishi waliompigia kura awali, ili wampigie Siyoi katika uchaguzi wa marudio uliofanyika jana. Mwingine ni Ezekiel Mollel, ambaye ni Katibu wa Jumuiya ya Vijana ya CCM Wilaya ya Monduli.

“Wote watatu tunawashikilia na wako kwa uchunguzi zaidi na ukikamilika wote watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka ya rushwa,” alisema Kamanda huyo.

Aliongeza kuwa Elirehema ni Katibu Mwenezi wa CCM Nyamagana ambaye alishika nafasi ya tatu katika uchaguzi huo. Alidai kwamba mtuhumiwa huyo baada ya kuhojiwa, alikutwa na tuhuma za kupewa jukumu la kushawishi kwa rushwa wajumbe waliompigia kura katika uchaguzi wa awali wapatao 205 ili wahamishie kura zao kwa Siyoi.

PICHA YA LEO; POOL TABLE ISIYO YA GHARAMA KUBWA YABUNIWA NA WATOTO WA KIJIJINI

Jamaa wakiendelea na mchezo maarufu wa pool baada ya kazi ngumu za kilimo.

TANGAZO LA KUCHELEWA KWA MSHAHARA WA FEBRUARI 2012 DUCE, JAMANI KUWENI MAKINI MSIKALIE HAKI ZA WATU. HAPO KAZI ZINAFANYIKA KWELI!!!?

 

MWANAJESHI WA MAREKANI ANYONYWA ULIMI HADHARANI,AIBU YA DUNIA.

Aibu ya Mwanajeshi wa Marekani Apakatwa, Anyonywa Ndimi na Mwanaume Mwenzake
  

  
Mwanajeshi huyo mwenye cheo cha Sajenti aliyejulikana kwa jina la Brandon Morgan aliruka na kutua kwenye kifua cha mpenzi wake mwanaume mwenzake na kumkumbatia na kuanza kunyonyana ndimi live live bila chenga.

Tukio hilo lilitokea nchini Marekani wakati wa sherehe za kuwakaribisha nyumbani wanajeshi wa Marekani waliokuwa wakipagana vita dhidi ya Taliban nchini Afghanistan.

Picha ya sajenti Morgan akiwa amemdandia mpenzi wake wa kiume akinyonyana naye ndimi imekuwa gumzo kubwa sana duniani.

Sajenti Morgan ambaye ni mkazi wa California hajakasirishwa na kusambaa kwa picha hiyo na badala yake amewashukuru baadhi ya watu waliompongeza na kuwatakia maisha mema yeye na mpenzi wake wa kiume.

Sheria ya Marekani ya kupiga vita ushoga na usagaji ilifutwa miezi mitano iliyopita hivyo kuwapa nafasi mashoga na wasagaji kujitangaza wazi bila woga.

Angalia picha ya sajenti Morgan akinyonyana ndimi na mpenzi wake ambaye ni mwanaume mwenzake