Ijumaa, 2 Machi 2012

MWANAJESHI WA MAREKANI ANYONYWA ULIMI HADHARANI,AIBU YA DUNIA.

Aibu ya Mwanajeshi wa Marekani Apakatwa, Anyonywa Ndimi na Mwanaume Mwenzake
  

  
Mwanajeshi huyo mwenye cheo cha Sajenti aliyejulikana kwa jina la Brandon Morgan aliruka na kutua kwenye kifua cha mpenzi wake mwanaume mwenzake na kumkumbatia na kuanza kunyonyana ndimi live live bila chenga.

Tukio hilo lilitokea nchini Marekani wakati wa sherehe za kuwakaribisha nyumbani wanajeshi wa Marekani waliokuwa wakipagana vita dhidi ya Taliban nchini Afghanistan.

Picha ya sajenti Morgan akiwa amemdandia mpenzi wake wa kiume akinyonyana naye ndimi imekuwa gumzo kubwa sana duniani.

Sajenti Morgan ambaye ni mkazi wa California hajakasirishwa na kusambaa kwa picha hiyo na badala yake amewashukuru baadhi ya watu waliompongeza na kuwatakia maisha mema yeye na mpenzi wake wa kiume.

Sheria ya Marekani ya kupiga vita ushoga na usagaji ilifutwa miezi mitano iliyopita hivyo kuwapa nafasi mashoga na wasagaji kujitangaza wazi bila woga.

Angalia picha ya sajenti Morgan akinyonyana ndimi na mpenzi wake ambaye ni mwanaume mwenzake

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni