Jumatano, 28 Machi 2012

TAKUKURU NACHINGWEA YAHAMASISHA WANAMICHEZO KUPAMBANA NA RUSHWA MICHEZONI.

Kaimu Kamanda wa TAKUKURU wilayani Nachingwea Nd. Zablon Ernest Ombory akiongea na viongozi wa Chama cha Mpira wa miguu wilayani Nachingwea (NAFA), wachezaji wa timu ya African Boys ya Rwangwa naTimberland almaarufu Kipande cha Ulaya ya Nachingwea pia waamuzi wa mchezo huo juu ya umuhimu wa michezo na mapambano ya rushwa michezoni kabla ya mechi kuanza katikati  ya mwezi huu.
Mgeni Rasmi akikagua wachezaji na waamuzi kabla ya mechi kuanza.

Mwenyekiti wa NAFA akiwaongoza wageni kurudi jukwaa kuu ili kuangalia burudani ya mchezo ambao uliishia kwa timu ya Timberland ya Nachingwea kuifunga African Boys 3-2. Waamuzi walikuwa Ndg. Chacha( kushoto) mwamuzi wa kati, Ndg. Ashomile na Malebo wakishika vibendera na Kamisaa toka Lindi.
Wageni jukwaani toka kushoto ni Afisa utamaduni wilaya ya Nachingwea Ndg. Mkungwi, Mweka Hazina wa NAFA Ndg. Nyoni, Kaimu Kamanda TAKUKURU Ndg. Ombory, Afisa wa TAKUKURU Ndg. Hassan na Hakimu Mfawidhi Mh. Hemela.
Wachezaji wa Timberland wakiwa mapumzikoni.

Wachezaji wa African Boys ya Rwangwa wakiwa mapumzikoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni