Jumatano, 7 Machi 2012

ASKARI POLISI WAWILI WAFUKUZWA KAZI BAADA YA KUDAI RUSHWA.

Askari hao wamefukuzwa kazi kwa kubainika kutenda kosa ambalo ni kinyume na utendaji kazi wa jeshi hilo ambalo walidai fedha hizo kutoka kwa Jacqueline Komba ili waweze kumuonyehsa gari lake lililokuwa limeibiwa na majambazi

Askari waliofukuzwa kazi akiwemo Koplo David na Koplo Lufefe wote wa jeshi hilo na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela.

Januari 16 mwaka huu Jacqueline aliripoti katika kituo cha polisi cha Chuo Kikuuu kuibiwa gari lake aina ya Suzuki Swift lililokuwa na namba za usajili T311 BWU alikuwa ameliegesha karibu na eneo la Swimming Pool chuoni hapo.

Kamanda wa Kenyela alisema, baada ya siku moja Komba alipigiwa simu na askari mmoja kutoka kituoni hapo kumtaka atoe kiasi cha shilingi Milioni 3 ili wamuonyeshe gari lake lilipo na yeye akawaomba kuwa amepungukiwa na kuwaahidi kuwapa kiasi cha shilingi Milion 2.5 na askari hao wakakubali na kumuahidi aje siku iliyofuata yaani Januari 19 wakutane eneo la Mlimany City wakachukue fedha hizo

Jaqueline aliweza kuripoti kituo kingine cha UIrafiki na mtego uliwekwa na watuhumiwa hao waliweza kukamatwa Februari 7, mwaka huu


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni