Jumanne, 20 Machi 2012

MAMA NA WANAE WASAULA NGUO MBELE YA SHULE, WAKAMATWA NA POLISI.



NewsImages/6316130.jpg
Mama na wanae walipoamua kumwaga radhi shuleni
Tuesday, March 20, 2012 1:33 AMMama mmoja na wanae wa kike na wa kiume wanashikiliwa na polisi nchini Marekani baada ya kusaula nguo zao zote na kuanza kusali mbele ya shule wakiwa uchi wa mnyama.
Polisi wa kitongoji cha Upper Darby kwenye jimbo la Philadelphia nchini Marekani wanamshikilia mama mmoja na wanae kwa kusali uchi wa mnyama mbele ya shule.

Taarifa ya polisi wa Upper Darby ilisema kuwa mama huyo mwenye umri wa miaka 43 aliyejulikana kwa jina la Sara Butler akiwa na wanae wa kike Joanne mwenye umri wa miaka 23 na Bessie mwenye umri wa miaka 22 pamoja na mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka 14 walisaula nguo zao zote na kuanza kusali kwenye maegesho ya magari mbele ya shule.

Taarifa zaidi zilisema kuwa awali siku ya tukio, mama huyo na wanae walifika kwenye shule ya sekondari ya Upper Darby High School wakitaka kumuona mmoja wa wanafunzi wa kiume. Walikataliwa kukutana naye kwasababu mama huyo si mzazi wake.

Mama huyo na wanae waliondoka na kurudi baada ya lisaa limoja na kuanza kusaula nguo zao mbele ya maegesho ya magari wakisali kwa kusauti wakimtaja Yesu Kristo.

Ili waonekane vizuri mama huyo na wanae walijaribu kupanda juu ya gari walilokuja nalo lakini polisi walioitwa eneo la tukio waliwahi kuwatia nguvuni mama na wanae.

Mama huyo na wanae wanaozidi umri wa miaka 18 walifunguliwa mashtaka ya kuvunja maadili ya jamii na kujianika uchi hadharani

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni