Alhamisi, 4 Oktoba 2012

WATANI WA JADI WATOKA SARE YA 1-1

Simba na Yanga Hakuna Mbabe, Zatoka Sare 1-1

NewsImages/6620754.jpg
Nani mbabe leo?
Mtanange wa watani wa jadi, Simba na Yanga umeisha kwa kutopatikana mbabe kati ya timu hizo mbili za jijini Dar es Salaam. Mechi imeisha Simba 1 Yanga 1.
Simba walianza kwa kujipatia goli la kuongoza dakika ya nne tu kupitia kwa Amri Kiemba aliyeunganisha krosi ya Saidi Chollo.

Yanga walisawazisha kwa njia ya penalti dakika ya 65 kupitia kwa Saidi Bahanuzi.

Dakika ya 79, Simon Msuva wa Yanga alipewa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Nyoso wa Simba.

Kikosi cha Simba kilichoanza leo:
Kaseja, Nassoro Masoud, Paul Ngalema, Shomari Kapombe, Juma Nyosso, Jonas Mkude, Mrisho Ngassa, Mwinyi Kazimoto, Felix Sunzu, Edward Christopher na Amri Kiemba. MFUMO 4-3-3


Kikosi cha Yanga kilichoanza leo:
Yaw Berko, Mbuyu Twite, Stephano Mwasika, Nadir Haroub, KelvinYondani, Athumani idd , Nizar Khalfan, Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima, Simon Msuva, Said Bahanuzi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni