Ijumaa, 19 Oktoba 2012

ASKARI POLISI AUAWA KIKATILI HUKO ZANZIBAR, KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR AZUNGUMZA NA WAANDISHI

 

Kamishna
wa Polisi Mussa Ali Mussa akifafanua jambo katika Mkutano na Waandishi
wa Habari akielezea juu ya Fujo na Ghasia zilizotokea katika Mkoa wa
Mjini Magharibi na kupelekea kifo cha Askari Mmoja,Mkutano huo
umefanyika katika Makao Makuu ya Polisi Ziwani Mjini Zanzibar.

 PICHA NA MAKAME MSHENGA-MAELEZO ZANZIBAR
Askari huyo Nd. Abdelhman alifikwa na umauti juzi usiku akiwa njiani akitokea kazini kwenda nyumbani majira ya saa 6.00 usiku ndipo alipovamiwa na kupigwa mapanga hadi kufa . Tukio hili linahusishwa na vurugu zilizofanywa na baadhi ya wafuasi wa UAMSHO tangu juzi mchana baada ya habari kuzagaa kuwa kiongozi wao Sheikh Hadi ametekwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni