Jumamosi, 13 Oktoba 2012

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MWANZA SACP LIBERATUS BARLOW AMEUAWA USIKU WA KUAMKIA LEO.

BREAKING NEWS: RPC MWANZA AUAWA USIKU WA KUAMKIA LEO


 SACP Liberatus Barlow 


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Kamishna Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Barlow ameuawa usiku wa kuamkia leo katika tukio linalohusishwa na ujambazi. 

Taarifa kutoka Mwanza ambazo zimethibitishwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini zinasema kuwa Kamanda Barlow aliuawa baada ya kumrudisha dada yake kutoka katika kikao cha harusi ya ndugu yao huko Kitangili mnamo saa 7.30 usiku wa kuamkia leo.
Hata hivyo, kwa mujibu wa mkuu wa operesheni wa jeshi la polisi ni kuwa habari hizo ni za kweli na amewataka wananchi wa mwanza kuwa watulivu na kuahidi wahalifu hao watapatikana.
Pole sana wanafamilia kwa kupoteza kiongozi mzuri wa jamii na familia.
Habari; ITV

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni