Jumapili, 7 Oktoba 2012

MTU MZIMA RICK ROSS AMEPANDA JUKWAANI SAA 8.15 HADI 9.00 USIKU

Mtu mzima Rick Ross kutoka nchini Marekani hivi sasa yuko jukwaani kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linalofanyika kwenye viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar salaam ,anakamua ile mbaya na mashabiki wamepagawa vyakutosha kwa kila anachowaelekeza kufuata wanafuata jamaa amefunika mbaya, hili ni onesho lake la kwanza nchini Tanzania kwa mwanamuziki huyo kufanya onesho Tanzania.
Mwanamuziki Rick Ross kabla ya kupanda jukwaani alitanguliwa na wasanii mbalimbali wa muziki wa bongofleva hapa nyumbani ambapo nao walikonga nyoyo za mashabiki waliohudhuria katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012 kwenye viwanja vya Leaders

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni