Jumatatu, 15 Oktoba 2012

CAPE VERDE YAIHAIBISHA CAMEROON KWENYE KUWANIA KUFUZU MASHINDANO YA MATAIFA HURU YA AFRIKA.

Cameroon yabanduliwa nje

Wachezaji wa Cameroon
Wachezaji wa Cameroon
Cameroon leo imebanduliwa nje ya fainali za kuwania kombe la mataifa huru barani Afrika zitakazo andaliwa nchini Afrika Kusini, licha ya kushinda mechi yao ya raundi ya pili kwa mabao mawili kwa moja dhidi ya Cape Verde hii leo mjini Yaunde.
Cape Verde iliilaza Cameroon kwa mabao mawili kwa bila katika mechi yao ya raundi ya kwanza.
Kabla ya mechi hiyo Cameroon ilihitaji kuishina Cape Verde kwa zaidi ya magoli mawili ili kujikatia tikiti ya kushiriki katika fainali hizo.
Cape Verde ambayo imeorodheshwa nyuma ya Cameroon katika orodha ya timu bora ulimwenguni, imeandikisha historia kwa kufuzu kwa fainali hizo za kuwania kombe la mataifa huru barani Afrika kwa mara ya kwanza baada ya kuishinda Indomitable Lions kwa jumla la magoli matatu kwa mawili.
Katika mechi nyingine ya kufuzu, Ethiopia ilivaana na Sudan ambapo Ethiopia imeibuka na ushindi wa mabao mawili kwa bila.
Katika mechi ya raundi ya kwanza Sudan ilishinda kwa mabao matano kwa matatu.
Ethiopia sasa imefuzu kupitia sheria ya goli la ugenini baada ya timu hizo kufungana jumla ya magoli matano kwa matano.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni