Jumapili, 9 Septemba 2012

FAINALI ZA AFRIKA 2013; ZAMBIA YAIFUNGA UGANDA 1-0.

Chipolopolo yailipua Cranes

Nahodha Christopher Katongo asherehekea goli.
Mabingwa wa Afrika Zambia wamewafunga Uganda bao 1-0 katika mechi iliyochezwa uwanja wa Levy Mwanawasa , mjini Ndola ,zambia, Jumamosi.
Hii ilikuwa mechi ya kuwania kufuzu kucheza fainali za kombe la Afrika za mwaka 2013, Afrika kusini.
Nahodha wa Chipolopolo Christopher Katongo alifunga goli kutokea katikati ya uwanja kipindi cha kwanza cha mchezo.
Mchezaji huyo anayesakata soka ya kulipwa nchini China alitumia mwanya wa kuzubaa kwa mabeki wa The Cranes kunasa mpira wa kurusha wa Davies Nkausu na kufurahisha mashabiki wapatao 40,000 waliohudhuria mechi hiyo.
Uganda, inasaka nafasi kwa mara ya kwanza kucheza fainali za kombe la Afrika (AFCON) tangu mwaka 1978 ilipomaliza mshindi wa pili nyuma ya wenyeji Ghana.
Timu hizo mbili zitarudiana nchini Uganda katikati ya mwezi Oktoba, mwaka huu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni