Jumatatu, 2 Julai 2012

RAIS KIKWETE ATOA MSIMAMO KUHUSU MADAKTARI.


'Daktari Asiyeweza Kazi Aachie Ngazi ' - JK


NewsImages/6503146.jpg
Rais Jakaya Kikwete
RAIS Kikwete amesema serikali haina uwezo wa kulipa kiwango cha mshahara cha Sh.Mi.3.5 wanachokitaka kulipwa madaktari
Na kuwataka madaktari ambao hawataridhika na kiwango kilichowekwa waachie ngazi na wakatafute mwajiri atakayekuwa na uwezo wa kuwalipa kiasi hicho

Rais Kikwete aliyasema hayo pia katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi kupitia vyombo vya habari

Rais Kikwete amesema, Serikali kwa sasa haiwezi kuwaahidi madaktari kima hicho kwani ikifanya hivyo malipo ya daktari anayeanza kazi yatakuwa ShMil. 7.7 kwa mwezi kitu ambacho hakiwezekani.

Mwisho alimalizia kwa kusema “nawasihi madaktari kuacha mgomo warejea kazini, kwani Watanzania wanateseka na kupoteza maisha kwa kukosa maatibabu”.

Wakati huohuo,Uongozi wa Taasisi ya Mifupa (MOI) umebandika tangazo linalosema na kuwataka madaktari wanaotaka kuendelea na kazi wakajisajili kwa Mkurugenzi wa Tiba

Tangazo hilo lilifanua kuwa madaktari watakaotaka kuendelea na kazi kujisajili ni mwisho leo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni