Jumatano, 18 Julai 2012

AJALI NYINGINE YA MELI KUZAMA IMETOKEA ZANZIBAR LEO MCHANA. NI MV SKAGIT SEAGUL, SMZ IMETANGAZA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO.

 

Wakazi wa Zanzibar wakiwa wamekusanyika katika Bandari ya Malindi mjini Unguja Zanzibar jioni ya leo wakati miili ya baadhi ya abiria wa Boti ya Kampuni ya Seagull "MV Skagit" wakitolewa baada ya boti hiyo kuzama na kupoteza maisha ya watu zaidi ya 200 hii leo ikitokea jijini Dar es Salaam.
Askari wa JWTZ wakiwa wamejipanga wakati wa zoezi la kupokea maiti.
Moja ya maiti ikiwa imebebwa na askari

Maiti ingine ikiwa imebebwa...
Ni hali ya huzuni Visiwani humo na jijini Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla. Ajali hii imetokea ikiwa imepita miezi kadhaa baada ya meli nyingine ya Abiria kupoteza uhai wa watu visiwani humo.
Meli ya Mv Skagit iliyokuwa safarini kutoka Dar kuelekea Zanzibar imezama majira ya saa nane mchana hii leo katika maeneo Pungume na Chumbe baada ya kukumbwa na upepo mkali.

Meli hiyo inayosadikiwa kuwa na abiria 250 inasemekana imepindukia upande mmoja na huku abiria wengi wakiweza kuokolewa kutokana na jitihada mbali mbali kupitia vile vile msaada wa boti za Mv Kilimanjaro, Tug ya Bandari na vyombo vyengine.

Mpaka tunaandika taarifa hizi ni maiti tatu zilikwishapatikana na kiasi cha abiria 150 wameokolewa na waliojeruhiwa wanatibiwa katika Hospitali ya Mnazimmoja.

Taarifa zinaeleza kwamba kulikuwa na watoto takriban 30 na Watalii kutoka nchi mbali mbali wafikao kumi.

Wazamiaji kutoka Kikosi cha KMKM pamoja na Jeshi tayari wapo eneo la ajali kusaidia kuokoa maisha ya wananchi waliokumbwa na maafa haya

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni