Jumapili, 3 Juni 2012

NAPE NNAUYE ATIKISA SONGEA LEO


Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo kimeiteka Songea baada ya umati wa wananchi wa mji huo kujitokeza katika mkutano wa hadhara wa CCM uliohutubiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye  kwenye Uwanja wa Zimanimoto mjini Songea mkoani Ruvuma. Pichani, Nape akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili kwenye uwanja huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Cornel Msuha. Pia alipata fursa ya kuongea na Jumuiya za wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu vilivyopo mjini Songea. (Picha na  Bashir Nkoromo)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni