Jumapili, 17 Juni 2012

MWENGE WAKIMBIZWA HUKO NACHINGWEA MKOANI LINDI.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea Bi. Mrindoko akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati Mwenge wa Uhuru ulipokimbizwa wilayani humu juma lililopita.


Mwenge ulishikwa na baadhi ya wafanyakazi na wananchi wengine wilayani Nachingwea.


Ujumbe wa Mwenge ni Hamasa juu ya zoezi la sensa mwaka 2012, pia vita dhidi ya ukimwi, madawa ya kulevya na rushwa.


Watoto wakiangalia machapisho mbalimbali katika Banda la TAKUKURU wilaya ya Nachingwea ambao nao walikuwepo kufikisha ujumbe juu ya mapambano dhidi ya Rushwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni