Jumanne, 5 Juni 2012

KILELE CHA MAADHIMISHO YA DIAMOND JUBILEE YA MALKIA WA UINGEREZA IMEFIKIA LEO.

Malkia Elizabeth wa Uingereza
Sherehe za Kuadhimisha miaka sitini ya utawala wa malikia Elizabeth zimefikia kilele hii leo Mjini London, Maelfu ya Watu walimshangilia wakati alipojitokeza kwenye Roshani (Balkoni) ya Kasri QASRI ya Buckingham, huku Ndege za Jeshi la ANGA zikipta Angani.
Mapema leo malkia Elizabeth alihudhuria Ibada Maalum ya Kutoa Shukurani katika Kanisa la St. Paul mjini London.Wanasiasa, Mabalozi na Viongozi wa Kigeni pia walihudhuria Ibada hio.
Kwenye hutuba yake kwa Waumini, Kiongozi Kanisa la Ki-Anglikana, Askofu Mkuu Rowan Williams, alimsifu Malkia Elizabeth kwa kujitolea kwake kwa Uingereza.
Baadaye Malkia alihudhuria dhifa ya chakula cha mchana iliyoandaliwa katika ukumbi wa Westminster ambapo baadaye alikwenda kwenye roshani ya nyumba ya Kifalme ya Malkia wa Uingereza ambapo alikuwa akisubiriwa kwa hamu kubwa na umati wa watu.
Maelfu ya watu walijipanga kando ya barabara kumuona Malkia akisindikizwa na walinzi wake.
Hii ndio kilele cha sherehe za kuadhimisha utawala wa miaka sitini wa Malkia. Wanasiasa, mabalozi na viongozi wa kigeni pia walihudhuria.
Kwenye hotuba yake kwa waumini, kiongozi wa ngazi ya juu zaidi katika kanisa la ki-Anglikana, Askofu mkuu Rowan Williams, alimsifu Malkia Elizabeth kwa kujitolea kutumikia raia wa Uingereza: Baadaye kidogo kwaya ilimuimbia Malkia wimbo huu.
Rais wa Marekani Barack Obama alituma pongezi kwa Malkia na raia wa Uingereza kwa siku hii

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni