Jumanne, 8 Machi 2011

GONGOLAMBOTO

WALIOKUFA GONGOLAMBOTO KULIPWA TSH. 8.5 KILA MMOJA.

Serikali imesema ipo tayari kulipa kifuta machozi cha shilingi milioni 8.5 kwa kila aliyekufa kwa milipuko ya mabomu katika kambi ya JWTZ Gongolamboto, Dar es salaam. Idadi kamili wa waliokufa kwa sasa ni 29 baada ya watu wengine wawili kuongezeka hiyo juzi.
Kadhalika shule 10 na zahanati zilizoharibika kwa milipuko hiyo, zitaanza kujengwa na Jeshi la Kujenga Taifa ili ziendelee kutoa huduma. Kaimu Mkuu wa Mkoa amewaomba wafiwa waharakishe utaratibu wa kupata wasimamizi wa mirathi mahakamani na hatimaye walipwe kifuta machozi chao.
Shule tatu kati ya kumi zilizoharibiwa zimepata wahisani wa kuzijenga upya ambazo ni sekondari ya Pugu itakayojengwa na Taasisi ya Shree Hindu Mandal, Mamlaka ya Elimu Tanzania(TEA) shule moja na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) litajenga moja na saba zilizobaki zitajengwa na SUMA JKT.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni