KWA kipindi kirefu sasa, usimamizi wa makaburi ya Sinza, Dar es Salaam umekuwa chini ya mikono ya mateja (watumiaji wa mihadarati) wanaoendesha biashara haramu ya maeneo ya makaburi yaliyokwishatumika ili kujipatia kipato.

Picha ya Maktaba; Msiba wa Dokta Remmy.
Kwa sababu ya kukosa utu na ufukara uliopitiliza, mateja hao wasiopungua 15 wamekuwa wakiendesha biashara hiyo waziwazi kwa miaka nenda rudi na hivyo kufanya wazoeleke kwa baadhi ya wakazi wa maeneo jirani na makaburi hayo, pamoja na wateja wanaofika kutafuta huduma ya maziko.
Kutokana na kuzoeleka huko na kwa sababu ya kutokuwa na tabia ya kukwapua vya watu kama wafanyavyo mateja wengine katika vituo vya mabasi na kwingineko, wa kwenye makaburi hayo wanapewa ushirikiano na watu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulipwa dau wanalolitaja na hivyo kuligeuza eneo hilo kuwa lao la kudumu kibiashara.
Uchunguzi wa gazeti hili uliothibitishwa na baadhi ya mateja hao, wakazi wa eneo hilo, viongozi wa mitaa na watu waliopotelewa na makaburi walimozikwa ndugu zao, umethibitisha kuwapo uozo mkubwa katika makaburi hayo ‘yanayomilikiwa’ na genge hilo kama sehemu ya kujiingizia kipato isivyo halali.
Aidha, imethibitika kuwa mateja hao wasio na tabia ya kuibia mtu wala kudhuru wanaoingia na kutoka kwenye makaburi hayo kusaka huduma ya maziko, hufukua makaburi ya waliozikwa kuanzia miaka miwili iliyopita kurudi nyuma na kuzika maiti wapya huku wakifahamu kuwa eneo hilo limejaa na linastahili kuachwa huru.
Kwa maelezo ya mateja waliozungumza na HABARILEO, wafu wanaowafukua zaidi ili kupata
makaburi ya wazi ni watoto wachanga bila kujali walizikwa lini pamoja na watu wazima waliozikwa kwa zaidi ya miaka miwili iliyopita.
Mateja walonga
Kwa masharti ya kutotajwa gazetini, baadhi ya mateja waliozungumza na HABARILEO kwa nyakati tofauti makaburini hapo, walidai kuishangaa Serikali kwa kusahau kuwapelekea vifaa vya afya kwa kuwa kazi wanayoifanya ni ya hatari kiafya.
Picha ya Maktaba; Msiba wa Dokta Remmy.
Kwa sababu ya kukosa utu na ufukara uliopitiliza, mateja hao wasiopungua 15 wamekuwa wakiendesha biashara hiyo waziwazi kwa miaka nenda rudi na hivyo kufanya wazoeleke kwa baadhi ya wakazi wa maeneo jirani na makaburi hayo, pamoja na wateja wanaofika kutafuta huduma ya maziko.
Kutokana na kuzoeleka huko na kwa sababu ya kutokuwa na tabia ya kukwapua vya watu kama wafanyavyo mateja wengine katika vituo vya mabasi na kwingineko, wa kwenye makaburi hayo wanapewa ushirikiano na watu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulipwa dau wanalolitaja na hivyo kuligeuza eneo hilo kuwa lao la kudumu kibiashara.
Uchunguzi wa gazeti hili uliothibitishwa na baadhi ya mateja hao, wakazi wa eneo hilo, viongozi wa mitaa na watu waliopotelewa na makaburi walimozikwa ndugu zao, umethibitisha kuwapo uozo mkubwa katika makaburi hayo ‘yanayomilikiwa’ na genge hilo kama sehemu ya kujiingizia kipato isivyo halali.
Aidha, imethibitika kuwa mateja hao wasio na tabia ya kuibia mtu wala kudhuru wanaoingia na kutoka kwenye makaburi hayo kusaka huduma ya maziko, hufukua makaburi ya waliozikwa kuanzia miaka miwili iliyopita kurudi nyuma na kuzika maiti wapya huku wakifahamu kuwa eneo hilo limejaa na linastahili kuachwa huru.
Kwa maelezo ya mateja waliozungumza na HABARILEO, wafu wanaowafukua zaidi ili kupata
makaburi ya wazi ni watoto wachanga bila kujali walizikwa lini pamoja na watu wazima waliozikwa kwa zaidi ya miaka miwili iliyopita.
Mateja walonga
Kwa masharti ya kutotajwa gazetini, baadhi ya mateja waliozungumza na HABARILEO kwa nyakati tofauti makaburini hapo, walidai kuishangaa Serikali kwa kusahau kuwapelekea vifaa vya afya kwa kuwa kazi wanayoifanya ni ya hatari kiafya.















