YANGA SC YAILAZA APR, YATINGA FAINALI KOMBE LA KAGAME

Kikosi cha Yanga kilichoanza mechi ya leo.
TIMU ya Yanga SC imefanikiwa kuingia Fainali ya Michuano ya Kombe la Kagame leo baada ya kuilaza timu ya APR ya Rwanda bao 1-0 kwenye mchezo wa Nusu Fainali uliochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Bao la Yanga limefungwa na mchezaji Hamis Kiiza katika muda wa nyongeza baada ya dakika 90 kumalizika 0-0. Kwa matokeo haya, Yanga itakutana na Azam FC katika fainali itayochezwa Jumamosi Julai 28, 2012 katika Uwanja wa Taifa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni