Alhamisi, 18 Aprili 2013

VIJEMBE TOKA BUNGENI JANA;MH. RAGE AMWAMBIA MH. LISSU AKASOME UPYA SHAHADA YAKE YA SHERIA NI BAADA YA KUKATAA TAARIFA YA LISSU JUU YA UHURU WA MAJADILIANO BUNGENI.

(Picha Maktaba)
Mh. Lissu jana alitolewa nje ya Bunge kwa nguvu kwa amri ya Naibu Spika Mh. Job Ndugai alipoonekana kuingilia Hotuba ya Mh. Mwigulu Nchemba jana aliyekuwa anashangaa habari ya udini imetoka wapi siku hizi baada ya miaka mingi ya utulivu chini ya utawala wa CCM!!!? Kiujumla hali ya utovu wa nidhamu imeendelea kutawala Bunge letu licha ya meza kuu kujitahidi kuidhibiti hali hiyo bila mafanikio, ni wakati wa wananchi kujitahidi kufuatilia matangazo ya vipindi vya Bunge ili tuchambue busara za Wabunge wetu hasa tukiangalia wapo kwa maslahi ya Watanzania au ya kwao binafsi!!?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni