Jumatatu, 1 Aprili 2013

BINTI ALIYEUAWA AKITOKA DISCO HUKO NACHINGWEA AMEZIKWA KIJIJINI KWAO NAIPANGA.

Mwili wa marehemu Mariam ukiwa umehifadhiwa baada ya kugunduliwa asubuhi nje mbele ya Kanisa la Assemblies of God Nachingwea.
Bint ajulikanae kwa jina la Mariam amezikwa jumatatu iliyopita kijijini kwao Naipanga baada ya uchunguzi wa Madaktari katika Hospitali ya Nachingwea kubaini kuwa alikabwa na kusababisha kushindwa kupumua hivyo kupoteza maisha, hata hivyo kabala ya kuuawa aliingiliwa kwa kubakwa na wauaji hao na inasadikiwa marehemu alikuwa anatokea Disco katika Ukumbi wa NR ambapo mashindano ya Dansi mia mia yalikuwa yanaendelea hadi yalipohitimishwa juzi. Mkononi alikutwa na alama ya muhuri wa Ukumbi wa NR ambao wote wanaoingia hapo hupigwa muhuri huo kama alama badala ya tiketi.
Polisi wanendelea na uchunguzi wa dhahama hiyo ikiwa ni pamoja na kuwashikilia wasichana wawili ambao ni maswahiba na marehemu Mariam, Mungu aiweke pema roho ya Marehemu Mariam, Amin.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni