Jumatano, 24 Aprili 2013

SURVIVAL FOR CASHEWNUT TRADE; WAKULIMA WA KOROSHO WILAYA YA LIWALE WAFANYA VURUGU KUBWA KUDAI MAKATO YAO YA MALIPO YA PILI YA KOROSHO HAPO JANA.

Kanisa la Katoliki Liwale(picha HansP)
Wakulima wa zao la korosho wa Wilaya ya Liwale Mkoa wa Lindi jana kuamkia leo wamefanya vurugu kubwa ya kufunga barabara kwa magogo na kuchoma moto baadhi ya ofisi za vyama vya ushirika wa mazao baada ya kufadhaishwa nakulipwa malipo pungufu katika shilingi mia sita wanazodai kama malipo ya pili kwa kila kilo ya korosho waliyouza msimu wa 2012/2013.
Madhira haya yasipodhibitiwa kwa haraka yanaweza kuhamia wilaya zingine za Kilwa, Rwangwa na Nachingwea kwa vile kuna tatizo kama hilo la Liwale. Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Lindi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilwa amefunga safari mchana huu kuelekea wilayani Liwale kujaribu kupata ufumbuzi wa tatizo hilo.
Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Lindi kinalaumiwa kufanya biashara ya kuuza korosho kwa mnada kwa bei ndogo pasipo kuwashirikisha  wadau wake ambao ni vyama vya msingi vya ushirika vilivyopo mkoani hapa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni