Jumatano, 12 Februari 2014

MAAFISA WAWILI WA TBA WAHUKUMIWA JELA MIAKA TISA KILA MMOJA.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo (TBA) na mwenzie wamehukumiwa kifungo cha miaka tisa jela au kulipa faini ya shilingi milioni kumi na tano kila mmoja na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu juzi baada ya kupatikana na hatia ya matumizi mabaya ya ofisi kinyume na kifungu cha 31 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa ya 2007. Watuhumiwa hao wanadaiwa kwa nyadhifa zao waliidhinisha ujenzi wa jengo la ghorofa 18 katika eneo ambalo mipango miji inaonesha inaruhusiwa kujenga majengo yasiyozidi ghorofa saba tu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni