Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo WAVUTI. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo WAVUTI. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 14 Novemba 2012

KINANA AWA KATIBU WA SEKRETARIETI YA CCM KUANZIA LEO.

CCM safu mpya: Kinana, Nchemba, Vuai, Zakhia Meghji, Asha-Rose Migiro

Katibu Mkuu mpya wa CCM, Abdulrahaman Kinana.
  • Kwa mujibu wa taarifa kutoka Dodoma, Sekretari ya Uongozi wa CCM Taifa ni kama ifuatavyo: -
  •  Katibu Mkuu ni Abdulrahman Kinana.
  • Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara ni Mwigulu Nchemba (Mb).
  • Naibu Katibu Mkuu Zanzibar ni Vuai Alli Vuai.
  • Katibu wa Itikadi na Uenezi ni Nape Nnauye.
  • Uchumi na Fedha ni bi. Zakhia H. Meghji.
  •  Katibu wa Oganaizesheni ni Mohammed Seif Khatib.
  •  Uhusiano wa Kimataifa ni Dkt. Asha-Rose Migiro.

Ijumaa, 20 Aprili 2012

TAFSIRI YA MJENGWA JUU YA SAINI SABINI ZA WABUNGE KUMNG'OA WAZIRI MKUU.

Ndugu zangu,

Leo asubuhi wakati nikifanya ' jogging' kwenye mitaa ya Dar es Salaam niliwasikia watu wa kawaida kabisa wakijiuliza na kujadili; " inakuwaje Serikali iwalipe marehemu mishahara huku sisi tulio hai hatuna hata uhakika wa milo miwili ya siku?" Wanauliza watu wa mitaani.

Naam, nchi yetu imekumbwa na mafuriko ya habari. Kule bungeni Dodoma kuna moto unawaka. Zimeitishwa sanini 70 ili Jumatatu ipigwe kura ya kukosa imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Ndio, kuna wanaotaka Pinda ang'oke, na labda kutolewa kafara, maana, siamini kama tatizo la msingi ni Pinda, bali ni la kimfumo zaidi. Na jana kuna mbunge wa CCM kayasema makali yafuatayo;

“Mheshimiwa Naibu Spika, inashangaza na kusikitisha kuwa nchi inatafunwa. Wanaofanya haya ni mawaziri wetu. Nchi inakufa na tuelewe kuwa Tanzania sio mali ya CCM, ni ya Watanzania wote.“Mawaziri wetu wamekuwa mchwa, wanaangamiza nchi na leo nitamtaja waziri anayeongoza kwa kutafuta fedha za Watanzania. Ni Waziri wetu wa Fedha, Mustafa Mkulo. Ameuza viwanja, amelidanganya Bunge baada ya kuivunja CHC,”- Deo Filikunjombe ( CCM) Bungeni jana.

Lakini ya jana yalitanguliwa na ya juzi; Mbunge mwanadamizi wa CCM Godfrey Zambi aliyasema makali haya;

" CCM inaweza kung'olewa madarakani katika uchaguzi wa mwaka 2015 endapo kasi ya ufisadi na ubadhirifu wa fedha za umma itaendelea kama ilivyo sasa"- Godfrey Zambi ( CCM, Mbozi Mashariki).

Kauli za wabunge hao wawili wa CCM zinatoa tafsiri ya kilio cha wabunge wa CCM kuomba msaada kwa anayeweza kuwasaidia. Inatoa tafsiri pia kuwa hicho ni kilio cha wabunge wengi wa CCM. Kwamba hayo ndiyo wanayaongea hata chini chini.

Ndio, wananung'unika na wameanza kuiona adhabu wanayokwenda kuipata kutoka kwa wananchi ifikapo 2015. Wanaona pia, kuwa ' kisungura' hiki kidogo kinachopatikana kila mwaka kinavyoliwa na wajanja na wengine kuachiwa mifupa.

Wabunge wa CCM na wengine wanaona jinsi baadhi ya mawaziri wa kutoka chama chao wanavyojiangalia wenyewe kwa kujikatia zaidi kasungura hako kadogo na hata minofu mingine kuikimbizia kwenye majimbo yao badala ya kuangalia majimbo mengine pia. Hakika, Wabunge wa CCM sasa wanatoa kilio cha kuomba msaada na kilichochanganyika na hasira na hofu ya kupoteza mamlaka ya kuongoza dola ifikapo mwaka 2015. Ndio, kuna wanaokiona chama chao kikielekea kwenye kuzama 2015. Kelele wanazopiga bungeni zimegeuka kama kelele za nyikani, hazisikiki. Wameanza sasa kuwa na ujasiri wa kuzomeana wazi wazi kwenye vikao vyao badala ya kusubiri kuzomewa na wananchi hadharani. Naam, CCM ya sasa inapata tabu hata kwenye kujua namna ya kuitumia misamiati mipya ya kisiasa, maana, kuna wanaojivua gamba, wanaovuliwa magamba na sasa kuna ' wanaojinyambua' magamba wakiwa ndani ya chama- 'Political evolution' ya namna fulani.
Zitto Kabwe Bungeni 2012 kumng'oa Waziri Mkuu Pinda Mizengo
Zitto Kabwe - Bungeni Aprili 2012

Na Mtego wa Zitto Kabwe kwa CCM?

Jana Mbunge Zitto Kabwe ameitega CCM. Ni mtego wa hatari. Saini zile 70 zina maana hii;
- Kama wabunge wa CCM hawatachangamkia kutia sahihi zao zikavuka hata mia na hamsini, basi, kuna ujumbe unaopelekwa kwa umma. Kuwa wabunge wa CCM ni maneno tu, hawana dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi. Wabunge wengi wa CCM hawataiepuka adhabu ya umma inaweza kuwa inawasubiri 2015.
- Kwa wabunge wa CCM kutia sahihi zao na hata Pinda kupigiwa kura ya wabunge kukosa imani nae ina maana pia kuwa wabunge hawana imani na bwana mkubwa aliyemteua Pinda. Busara haiwataki wabunge wa CCM kufikia hapo. Hilo halina maslahi kwa taifa.

Nini kitakachotokea?


Kuna matatu;
Mosi, Mawaziri wale watano wanaotuhumiwa kwa ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma wanaweza kuepusha aibu kwa Serikali kwa wao wenyewe kutangaza kujiuzulu. Ingawa hili ni gumu kufanyika katika nchi hii, lakini, wakati mwingine kuna lazima ya kufanyika- maana, hapo watakuwa wamemnusuru Waziri Mkuu na aliyemteua.

Pili- Likishindikana la kwanza, basi, kabla ya Jumatatu, Waziri Mkuu Pinda awe ameshajiandaa kufanya maamuzi magumu. Kujiuzulu na kulinda heshima yake na ya aliyemteua. Au kutolewe ' Tamko la Serikali' litakalobadili upepo unaovuma sasa bungeni.

Tatu: La kwanza na la pili yaweza yasifanyike, na badala yake. Rais anaweza kuyaona yanayotokea sasa bungeni kama fursa ya kufanya mabadiliko makubwa Serikalini mara akitua Dar kutoka ziara ya Brazil.

Naam, yumkini pale Diamond Jubilee, kabla ya Jumatatu, kuna watakaopewa kazi ya kusafisha ukumbi na kupanga viti tayari kwa Mkuu wa Nchi kusema jambo kubwa kwa taifa kupitia kwa ' Wazee wa Darisalama'.

Na tusubiri tuone.
Maggid Mjengwa,
0788 111 765

Jumatano, 18 Aprili 2012

WABUNGE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI HAWA HAPA, KIZIGHA NA SHYROSE WAULA.

Shyrose Bhanji, Mbunge mpya wa EALA.
Waliochaguliwa kuwa Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (East Africa Legislative Assembly - EALA):

1.      Anjela Charless Kizigha - CCM

2.      Shy-Rose Saddrudin Bhanji - CCM

3.      Maryam Ussi Yahya - CCM

4.      Twaha Issa Taslima - CUF

5.      Nderakindo Perpetua Kessy – NCCR-Mageuzi

6.     Abdullah Ali Hassan Mwinyi  - CCM

7.      Adam Omar Kimbisa - CCM

8.      Bernard Musomi Murunya - CCM

9.      Charles Makongoro Nyerere  - CCM

Majina haya yanatoka kwenye orodha ya watu 33 walioteuliwa juzi
unaweza kubofya hapa kuirejea, tizama video kusikia muhtasari wa zoezi la upigaji kura na alichopata kila mshindi (shukurani ya video imwendee Mwanakijiji).
PS: Kuna mtu katika ukurasa wangu wa facebook ameaulizia 'audio' ya mtu aliyekuwa akizungumza 'lugha ya bibi' ndivyo sivyo, tafadhali tembelea bofya hapa kutembelea ukurasa wa tovuti ya Millard Ayo kusikiliza audio hiyo

Alhamisi, 2 Februari 2012

KUNANI MISRI, WATU 73 WAFARIKI KATIKA VURUGU KWENYE MECHI YA SOKA BAADA YA MAPIGANO.

 
Egyptian state TV has raised the death toll to 73 after fans of rival soccer teams rushed the field, hurling stones and sticks at each other and sparking a stampede.

State TV cited the Health Ministry and says 1,000 other people were injured in Wednesday's melee.

A medical official, speaking on condition of anonymity because he wasn't authorized to release the information, says some of the dead were security officers. Egypt's state prosecutor has ordered an immediate investigation into the causes of the deaths. Witnesses say most appeared to have occurred in a stampede after fans of the home team, Al-Masry, stormed on to the field following a rare 3-1 win against Al-Ahly, Egypt's top team. They then chased players and fans from the rival team.

Jumanne, 27 Desemba 2011

MCHUNGAJI LUSEKELO AGEUKA HAKIMU, ASEMA JAIRO NA LUHANJO HAWANA MAKOSA!!!!!!!

 
Picture
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Maombezi (GRC) lililopo Ubungo Dar es Saama, Mchungaji Antony Lusekelo, ameibuka na kusema kuwa sakata la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Bw. David Jairo, na Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Philemon Luhanjo, ni majungu na haina tatizo.

Bw. Jairo anadaiwa kuchangisha fedha za umma kwa ajili ya kugharamikia kupitisha bajeti ya wizara hiyo kinyume cha utaratibu huku Bw. Luhanjo akidaiwa kumjingia kifua.

Mchungaji Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako amesisitiza kuwa wapo viongozi wengi waliofanya kitendo sawa na ya  Jairo lakini hayajulikani hivyo kutaka Watanzania kuacha tabia ya kuchafuana.

Akizungunza na waandishi wa habari Kanisani kwake jana, Mchungaji Lusekelo alisema haiwezekani mtu mmoja kupanga kuchangisha fedha za wizara bila kuwa na mtandao na viongozi wengine na kudai kuwa kilichotokea ni siri kuvuja na si vinginevyo, "Ninachojua ni kwamba wezi wote wako mahakamani, unapoona mtu analalamikiwa kila siku wala hakamatwi ujue ni majungu tu na mambo hayo hafanyi, angefanya angekuwa selo

Ikumbukwe kwamba kuharibiana na kuchafuana kupo, mfano mimi niliwahi kuambiwa kwamba nimeenda nchini Nigeria kutafuta nguvu za giza wakati sijawai hata kuwaza kufanya kitendo cha namna hiyo,"alisema Mchungaji Lusekelo na kuendelea "Lazima tukiri kwamba watu wanachafuana na ndio maana ninasema hata kwa Bw. Jairo ni siri tu ilivuja na hawezi kufanya peke yake," alisisitiza

Alhamisi, 3 Novemba 2011

ALIYEKUTWA NA FUVU LA BINADAMU AFUNGWA MIAKA 10 JELA.

Picture
Fatma Kachingo (aliyeshikilia fuvu) akiwa chini ya ulinzi wa askari Polisi mkoani Morogogo
Fatuma Kachingo (42) ambaye anadaiwa kuwa ni mganga wa jadi katika kijiji cha Wami Dakawa wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, anayedaiwa kukutwa na fuvu pamoja na ngozi ya binadamu, amehukumiwa kwenda jela miaka 10 kufuatia kukiri kosa la kukutwa na viungo vya binadamu kinyume cha sheria.


Hukumu hiyo imetolewa na hakimu mkazi wa Mahakama ya mkoa wa Morogoro, Nuru Prudencia Nasari baada ya mshitakiwa namba moja ambaye ni mwanamke kukiri shitaka lake huku mumewe akirudishwa mahabusu baada ya kukana shitaka wakati walipofikishwa katika mahakama hiyo kwa mara ya kwanza na kusomewa shitaka hilo wote pamoja.


Hakimu Nasari akisoma hukumi hiyo kwa Fatuma Kichango alisema kuwa kosa alilokutwa nalo mtuhumu la kumiliki viungo vya binadamu ni kinyume cha sheria za nchi hivyo anatoa hukumu ya kwenda jela miaka 10 ili iwe fundisho kwa watu wenye tabia kama hiyo ambapo miaka hiyo inatokana na utetezi wa mshitakiwa kwa kuwa hajawahi kushitakiwa na kosa lolote la jinai na kwamba ana mtoto mdogo anayemtegemea kwani jambo hilo ni la kutisha katika jamii.


Nasari alisema pia mahakama imeona kuwa ni kuwa na vitu kama hivyo na kwamba ametoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa wengine ambao wanamiliki vitu kama hivyo.


Awali akisoma shitaka, Mwendesha Mashitaka wa polisi Lameck Wabi alidai kuwa washitakiwa hao kwa pamoja walikutwa na Fuvu na ngozi ya binadamu pamoja na vifaa vingine vinavyodhaniwa kuwa vya kishirikiana.

Jumamosi, 1 Oktoba 2011

MAAFISA ARDHI NDIO CHANZO CHA MIGOGORO ARDHI.

 
Picture
Mh. Ole Medeye.

Migogoro mingi ya ardhi inayotokea katika maeneo mbalimbali ya nchi inasababishwa na maafisa ardhi wanaouza ardhi mara mbili kwa watu tofauti, jambo ambalo limesababisha wananchi kugombana na kuchukiana.  Hayo yalisemwa jana na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck Ole-Medeye kwenye mkutano wa wadau wa ardhi uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Ole Madeye alisema kuwa maafisa hao wamekuwa na tabia ya kupenda fedha huku wakijua kuwa wanachokifanya ni kinyume na maadili ya kazi zao na kusababisha chuki kati yao kitendo ambacho kinachochea migogoro hiyo, jambo ambalo ni hatari na kwamba jamii inapaswa kupiga vita tabia hiyo.

“Maafisa ardhi wasio waadilifu ni hatari, kwa sababu wanachangia kuwepo kwa migogoo ya ardhi kwenye maeneo yao, jambo ambalo ni hatari katika jamii inayowazaunguka, na kwamba inachangia serikali kuonekana imeshindwa kazi, kutokana na hali hiyo tutawashughulikia kwa mujibu wa sheria,”alisema Ole Medeye.

Aliongeza, ardhi ni mali ya mwananchi na Serikali, hivyo basi kila upande unapaswa kushirikishwa wakati wa kuuza au kumtafuta mwekezaji, lakini baadhi ya maafisa hao wanashindwa kufanya hivyo badala yake wanaweka tamaa ya fedha mbele, ni tatizo kubwa.  Alisema atakayeshindwa kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa na serikali ajiondoe mwenyewe kabla ya kuondolewa kwa sababu wanarudisha nyuma maendeleo ya wananchi katika eneo husika  na kwamba wanachochea migogoro hiyo.

Alisema, kutokana na hali hiyo maafisa hao wanapaswa kubadilika na kufanya kazi kwa mujibu wa sheria ili kupunguza matatizo yaliyojitokeza ambayo yamesababisha wananchi kuijengea chuki serikali na kuonekana imeshindwa kuwajibika kwa ajili ya watu wachache.

Ole Medeye alisema, ’mteja ni mfalme’, hivyo basi wateja wa maafisa ardhi ni wananchi, kutokana na hali hiyo wanapaswa kuwashirikisha kwa kila hatua inayofikiwa,ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha, na kuwaeleza mchakato mzima wa kuendeleza ardhi au kutafuta wawekezaji ili waweze kuelewa jambo ambalo naamini linaweza kupunguza migogoro hiyo.

Hata hivyo, Ole Medeye mpaka sasa baadhi ya maafisa hao hawana takwimu sahihi za viwanja wanavyomiliki na kwamba takwimu watakazozitoa katika kipindi hiki siyo za ukweli, hii inatokana na uzembe katika kutimiza wajibu wao, kutokana na hali hiyo wanapaswa kutimiza wajibu wao ikiwa ni pamoja na kubaini viwanja vilivyopimwa, vilivyouzwa pamoja na viwanja vinavyotakiwa kupimwa ili waweze kukusanya kodi ipasavyo.

“Maafisa hawa hawana takwimu sahihi ya viwanja wanavyovimiliki, hii inatokana na kushindwa kuwajibika ipasavyo, jambo ambalo limesababisha kupotea kwa kodi ya ardhi, kutokana na hali hiyo wanapaswa kubadilika ili tuweze kukusanya mapato yetu stahiki,” aliongeza. Alibainisha, ikiwa watafanya hivyo, wataweza kushirikiana na wananchi ili kuondoa migogoro hiyo pamoja na kufuata taratibu zinazotakiwa katika kuendeleza kazi zao

Ijumaa, 9 Septemba 2011

MCHUNGAJI MTIKILA ALILIA JENGO LA MAHAKAMA YA RUFAA LISIUZWE.

Mch. Mtikila.

 
Mwenyekiti wa Democratic Party, DP, Mchungaji Christopher Mtikila, amefungua kesi akipinga kuuzwa jengo la Mahakama ya Rufani Tanzania.

Mtikila alifungua kesi hiyo leo Septemba 9, 2011 katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, ambayo imepewa namba 23/2011 na walalamikiwa katika kesi hiyo ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Waziri wa Katiba na Sheria na Jaji Mkuu wa Tanzania.

Kwa mujibu wa hati ya madai, Mtikila anadai jengo la mahakama hiyo ni miongoni mwa majengo ya kumbukumbu na historia, ambayo yanapaswa kuhifadhiwa. Anadai jengo hilo licha ya kuwa la kihistoria na utamaduni, pia ni urithi wa vizazi vijavyo na ni kosa kulifanyia mabadiliko yoyote.

Mtikila anadai jengo hilo lilipokabidhiwa kwa Idara ya Mahakama, Serikali ililifanyia ukarabati uliogharimu shilingi bilioni mbili ili likidhi mahitaji ya kuwa Mahakama ya Rufani. Anadai hilo lilitokana na kuongezeka kwa shughuli za mahakama, anadai kutokana na hilo, lilijengwa jengo lingine la ghorofa mbili nyuma ya jengo la zamani, kwa gharama ya sh. bilioni 1.3. Pia  ilikubaliwa kujengwa sanamu ya Jaji Mkuu wa kwanza, hayati Augustino Said kama kumbukumbu yake.
Anaiomba Mahakama itamke kuwa, walalamikiwa wana wajibu wa kulihifadhi jengo hilo kulingana na sheria za uhifadhi wa mali za kale; Pia iwazuie walalamikiwa kulitoa na kulivunja jengo hilo, badala yake lihifadhiwe kulingana na sheria ya mali za kale.

Jumatatu, 8 Agosti 2011

TAMWA, TGNP MPO!? MWANAUME AJINYONGA KUTOKANA NA MATESO YA MKE, HATARI!!!!!

Mkazi mmoja katika Mtaa wa NHC katika Mji wa Mugumu wilaya ya Serengeti wilayani Mara, Samson Kitoshi (32) amejinyonga hadi kufariki dunia kwa kamba chumbani kwake kwa kile alichodai kuwa: “Amechoka kupigwa na mkewe kila wakati.”
Mkurugenzi wa TAMWA Bi. Ananilea Nkya.
Tukio hilo lililovuta umati mkubwa wa watu, linadaiwa kutokea jana saa tano asubuhi. Akisimulia mkasa huo, mtoto wa marehemu (jina tunalihifadhi) alisema kabla ya kutokea kwa tukio hilo, mama yao alimpa Shilingi 1,000 akanunue sukari na vitafunwa, lakini asimpe baba yao chai... "Mama aliaga kuwa anakwenda Hospitali DDH kwa kuwa anaumwa. Baba akasema hatakunywa chai hiyo na kutuambia kuwa hatutamwona tena anatuaga na tusiingie ndani."

Marehemu baada ya kuingia chumbani kwake anadaiwa kuwa alifunga kamba juu ya dari na kujining'iniza hadi alipokata roho. Mtoto huyo wa darasa la tatu ambaye ana umri wa miaka 10 alisema hawakuweza kuingia ndani kama walivyoambiwa na baba yao, lakini baadaye aliamua kumwamsha akidhani kuwa amelala ili anywe chai ndipo alipokuta amening'inia. Alipiga kelele kuomba msaada.

"Baba alikuwa amevua shati akawa amening'inia chini kuna meza nikaweka stuli ili nifungue kamba sikuweza nikapiga yowe majirani wakafika wakasema ameshakufa," alisema.

Kuhusu migogoro ya ndani, mtoto huyo alisema kumekuwa na ugomvi wa mara kwa mara hasa ukisababishwa na mama yao ambaye anauza pombe ya kienyeji ya wanzuki anaporudi akiwa amelewa kwani humfanyia vurugu baba yao.

"Hivi karibuni baba alifikia hatua ya kumtaka mama aondoke amechoka na mateso anayomfanyia, lakini mama alikataa kuwa hawezi kutoka na kudai yeye ndiye atakayetoka," alisema. Ndugu wa Kitoshi ambaye anaishi katika Kijiji cha Morotonga alisema kuwa marehemu aliyekuwa akifanya kazi ya kusaga nafaka alikuwa akilalamika kupigwa na mkewe mara kwa mara.

"Huyu ni ndugu yangu hata leo amefika kwangu na akanikosa na kurudi nadhani alitaka kuniambia kitu. Baada ya muda nikapigiwa simu kuwa amekufa kwa kujinyonga, amechoshwa na kupigwa," alisema.

Kamanda wa Polisi Wilaya ya Serengeti, Paulo Mng'ong'o alijaribu kumtafuta mwanamke huyo kwa simu lakini mara baada ya kujitambulisha kuwa yeye ni OCD, mama huyo alikata simu.

Baada ya muda mama huyo alifika nyumbani na kumkuta mume wake akining'inia kwenye kamba. Huko alipokewa kwa maneno makali kutoka kwa wanawake wenzake waliokuwa na hasira baadhi wakisema: “Ulitaka afe ujitawale sasa amekufa tanua... unadanganya ulikuwa hospitali mbona umelewa..."

Maneno hayo makali yalimwingia mwanamke huyo kwani alikaa chini kisha akalala chali na kupoteza fahamu. Hakuweza kunyanyuka hadi alipopakiwa kwenye gari la polisi pamoja na mwili wa mumewe na kupelekwa hospitali.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda Mng'ong'o alisema polisi inalifanyia uchunguzi na kwamba itatoa taarifa kwa umma. Alisema wangefanya mahojiano na mke huyo wa marehemu baada ya kuzinduka kujua chanzo cha kifo hicho.Mwenyekiti wa Mtaa wa NHC, Elias Nyamraba alisema kuwa wanasubiri ndugu wa marehemu kwa ajili ya hatua nyingine ikiwemo ya mipango ya mazishi akisema Kitoshi ni mzaliwa wa Kijiji cha Issenye


source:wavuti.com

Jumatatu, 6 Juni 2011

VIJANA U-23 WAIFUNGA NIGERIA, TAIFA STARS HOI.

 
Timu ya Taifa ya soka kwa wanaume wa umri wa chini ya miaka 23 (U23) imeshinda katika mpambano wao wa kwanza dhidi ya Nigeria katika mchezo wa kusaka nafasi ya kushiriki mashindano ya Olympic.

Tanzania imeshinda bao 1 lililofungwa na Thomas Ulimwengu katika dakika ya 81 na kuwaacha Nigeria waliokuwa wakicheza kwa kuzuia zaidi wakibaki na nyavu zao.

Kwa matokeo hayo, Tanzania inahitaji sare yoyote katika marudiano yatakayofanyika wiki mbili toka sasa ili iweze kusonga katika ngazi zinazofuata za michuano hiyo.

Kwa mechi ya African Nations Cup, mambo yaliingia shubiri huko mjini Bangue kwani timu ya Central African Republic iliibangua 2:1 timu ya Tanzania.

Matukio muhimu kama yalivyorekodiwa na tovuti ya BBC ni:

1315GMT: So we are learning that the CAR v Tanzania game will kick-off at 1500GMT - the head of the Taifa Stars delegation, Samwel Nyala, has told a local radio that the pitch in Bangui is bumpy but the Tanzanian team is in top mood.

1538GMT: In Bangui its approaching half-time and it's still goalless between Central African Republic and visiting Tanzania.

1550GMT HALF-TIME CAR 1-0 TANZANIA: The hosts, who have been dominating, score on the stroke of half-time.

1610GMT: Back playing in Bangui where hosts CAR lead 1-0 over Tanzania.

1636GMT: Tanzania are fighting back and Athuman Machupa is one of several Taifa Stars who has failed to convert good chances against the CAR.

1640GMT GOAL! CAR 1-1 Tanzania. Star striker Mbwana Samata, who has come on as a second-half substitute, equalises for Tanzania.

1646GMT GOAL! CAR 2-1 Tanzania. The hosts score what should be a winner in the last few minutes of the game.

1659GMT: FINAL SCORE CAR 2-1 Tanzania: That result means CAR are second in the group behind Morocco on goal difference - both teams have seven points. Tanzania are third now ahead of Algeria on goal difference.

Matokeo mengine ya mechi zilizochezwa siku ya leo, Jumapili 5, 2011 hadi chapisho hili linapotoka ni:
  • Group E: Mauritius 1-2 DR Congo - Result
  • Group C: Comoros 1-1 Libya - Result
  • Group K: Botswana 0-0 Malawi - Result
  • Group A: Zimbabwe 2-1 Mali - Result
  • Group B: Ethiopia 2-2 Nigeria - Result
  • Group H: Benin 2-6 Ivory Coast - Result
  • Group I: Swaziland 1-2 Sudan - Result
  • Group H: Burundi 3-1 Rwanda - Result
  • Group D: Central African Republic 2-1 Tanzania - Result
  • Group J: Angola 1-0 Kenya - Result
  • Group A: Liberia 1-0 Cape Verde (Latest)
  • Group B: Guinea v Madagascar
  • Group K: Tunisia 2-0 Chad (Latest)
  • Group G: Egypt v South Africa (1830GMT)

ZAIDI YA WATU 20 WAJERUIWA KATIKA MLIPUKO HUKO NAIROBI KENYA, MMOJA AHOFIWA KUFA.

 
At least 1 person died leaving at least 28 others injured on Sunday, when an explosion went off in downtown Nairobi and set a gas station on fire.

“One person has died from this explosion 28 others are still receiving treatment in hospitals around the city, the number of casualties might rise because businessmen and their customers were caught unaware,” Police Spokesman Erick Kiraithe told journalist late on Sunday.

AFP photographer said the blast went off around 11 a.m. local time near Nairobi's Kirinyaga Road injuring dozens of people and sending ambulances and police rushing to the scene. The injured were taken to a local hospital, where several were being treated for serious burns.

Omar Alwiya, a bus conductor, said he was sleeping at around 11 a.m. when he heard an explosion that shook the room he was in and filled it with dust. He rushed to the scene and found two shipping containers overturned, several cars destroyed and a fire at a gas station.

Prime Minister Raila Odinga visited the scene of the blast and said in a brief statement to reporters that at least 28 people had been injured.Dr. Peter Kamau Wanyoike said 29 people were admitted to Kenyatta National Hospital. Nine had burns on 60 percent of their body. Others were injured by falling glass or minor burns.

Authorities have not ruled whether the explosion was accidental or set on purpose,  “It is still too early to ascertain the cause but we have our team of the anti terrorism police, our bomb experts and the officers from the Criminal Investigations Department on the ground,” the Spokesman added.

Kenya has experienced bombings in the past, most recently in December on a bus that was set to travel to the Ugandan capital, Kampala. At least two people died in that attack.

The Somali militant group al-Shabab which controls vast swathes of neighbouring Somalia,has repeatedly threatened to attack Kenya because of its support for the U.N.-backed Somali government in Mogadishu.