Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo GADAFFI. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo GADAFFI. Onyesha machapisho yote

Jumanne, 28 Juni 2011

MAHAKAMA YA KIMATAIFA YATOA HATI YA KUKAMATWA GADDAFFI, IS IT A FAIR COURT OF LAW!?

Waziri wa sheria nchini Libya Mohammed al Qamoodi amesema hati za mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita za kutaka Kanali Muammar Gaddafi akamatwe zimelenga kuficha uhalifu wa Nato.
Kanali Muammar Gaddafi


Akizungumza mjini Tripoli, Bw Qamoodi amesema operesheni za Nato zinazoendelea nchini humo ni uhalifu wa kivita dhidi ya raia wa Libya lakini ICC imezifungia jicho.
Waziri huyo ameongeza kuwa wanajeshi wa Nato sasa wamepata kisingizio cha kumuua kiongozi wao Kanali Gaddafi.
Hata hivyo ametangaza kuwa Libya imepata fursa ya kufungulia Nato mashtaka ya uhalifu wanaoendeleza nchini Libya.
Mahakama hiyo imemtuhumu Gaddafi kwa uhalifu dhidi ya binadamu na kuamuru mashambulio kwa raia baada ya machafuko dhidi yake kuanza kati kati ya mwezi Februari.
Mahakama hiyo iliyopo the Hague pia imetoa hati ya kukamatwa kwa mtoto wake wa kiume Saif al-Islam na mkuu wa idara ya ujasusi Abdullah al-Sanussi.
Hatua hio imeendelea kuzua hisia tofauti.
Mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mashauri ya nchi za kigeni nchini Urusi, Konstatin Kosachev amesema kuwa uamuzi wa jaji hao sasa utavuruga juhudi za kutafuta suluhu ya mzozo huo.
Bw Kosachev amesema nia kuu ya jumuiya ya kimtaifa ni kuwa Kanali Gaddafi ajiuzulu na atoke nchini humo lakini sasa hilo huenda lisifanyike.
Badala yake, Kosachev amesema huenda kiongozi huyo atafanya kila juhudi kushinda vita hivyo na hii sio habari njema kwa Libya.
Lakini kwa upande wao, wapinzani wamekaribisha uamuzi huo.
Msemaji wao Ibrahim Dabbashi amesema sasa jukumu lipo kwa washirika wa Gaddafi kuelewa kuwa wanafanya kazi na mhalifu na wamshauri aondoke madarakani.
Maelfu ya watu wanaaminiwa kufariki dunia kwenye ghasia hizo.

Alhamisi, 19 Mei 2011

Jumatano, 23 Machi 2011

VIONGOZI AFRIKA WALAANI UVAMIZI MAGHARIBI LIBYA

Marais wa Uganda, Zimbabwe na Afrika ya Kusini kwa nyakati tofauti wamelaani uvamizi wa kijeshi wa Marekani na marafiki zake kwa Libya na kusema kuwa mashambulizi hayo ni undumilakuwili wa mataifa hayo yanayoacha baadhi ya mambo yaendelee katika mataifa mengine vibaraka kwao na kuishupalia Libya. Mugabe na Museveni wamesema nchi hizo zimevamia Libya wakiwa na nia ya kujipatia mafuta kibabe huku Zuma wa Afrika ya Kusini akiona ni siasa zisizofaa za mataifa hayo kujichagulia viongozi vibaraka kwao. Umoja wa Nchi za Afrika umeyataka mataifa hayo kusitisha mashambulizi hayo mara moja.