Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo EDUCATION FOR ALL. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo EDUCATION FOR ALL. Onyesha machapisho yote

Ijumaa, 22 Julai 2011

WALIMU WATAKAOPANGIWA KAZI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU KULIPWA POSHO YA LAKI TANO

Waziri wa Elimu Dk. Shukuru Kawambwa.

SERIKALI mwaka huu itaanza kulipa posho ya kujikimu ya Sh. 500,000 walimu watakaopangiwa na kuripoti katika maeneo yenye mazingira magumu ikiwa ni sehemu ya motisha kwao.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, aliliambia Bunge juzi kwamba utaratibu maalumu utafanyika kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tamisemi, kuainisha na kutambua maeneo yenye mazingira magumu nchini kote.

Dk. Kawambwa aliyasema hayo wakati akijibu hoja za wabunge kabla ya kupitishwa kwa Makadirio ya Matumizi ya Wizara yake, Sh bilioni 659.29 kwa mwaka huu wa fedha; Sh. bilioni 71.76 za matumizi ya kawaida; Sh. bilioni 34.43 mishahara na Sh bilioni 37.33 matumizi mengineyo.

Chini ya mpango huo wa kutoa motisha kwa walimu, Dk Kawambwa alisema nyumba 1,200 zenye uwezo wa kuchukua familia mbili kila moja, zitajengwa katika maeneo hayo ambayo hata hivyo hakutaja vigezo vitakavyotumika kuyatambua.

Alisema lengo ni walimu hao wafikie kwenye nyumba za heshima ili wapate ari ya kufanya kazi. Majibu ya Waziri yalitokana na hoja za wabunge ambao wengi wao walizungumzia suala la maslahi ya walimu huku wengine wakiitaka Serikali itafute ufumbuzi wa tatizo la baadhi yao kukataa kuripoti katika baadhi ya maeneo.

Akiendelea kutaja mikakati ya kuboresha taaluma ya ualimu, Waziri Kawambwa alisema pia Serikali imepandisha posho ya wanavyuo vya ualimu wanaokwenda kufanya mafunzo kwa vitendo kutoka Sh. 800 hadi Sh 2,000 kwa siku. Alisema posho hiyo itaendelea kurekebishwa kulingana na mahitaji.

Katika hatua nyingine, alisema Serikali itaunda bodi itakayokuwa na mamlaka ya kusimamia taaluma ya ualimu kama ilivyo kwa taaluma zingine nchini. Alisema chombo hicho, kitawajibika kusimamia taaluma na maadili ya walimu.

Ingawa Kawambwa hakusema ni lini chombo hicho kitaanzishwa, alisema kama ilivyo kwa madaktari, wahandisi na taaluma nyingine zenye bodi maalumu za usimamizi, kwa walimu, bodi hiyo itawezesha wanataaluma hao pia kuwa chini ya chombo chao.

Akizungumzia changamoto iliyotolewa na wabunge kuhusu kuimarisha Idara ya Ukaguzi, Waziri alisema Serikali inafanyia kazi ushauri huo hususan unaotaka iwepo mamlaka au wakala anayejitegemea kwa ajili ya kuendesha kitengo hicho. Alisema wameshajadili suala hilo mara nyingi.

Ijumaa, 1 Julai 2011

WANAFUNZI WALIOSIMAMISHWA UDOM KUANZA KUREJEA KUANZIA KESHO.

CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM), kimetangaza kuwarejesha chuoni kuanzia kesho wanafunzi wote wa mwaka wa tatu wa Shule ya Sanaa na Sayansi ya Jamii waliosimamishwa masomo, huku 15 hatima yao ikisubiri taarifa binafsi kutoka mamlaka husika.
Majengo ya Chuo Kikuu cha Dodoma


Kwa mujibu wa tangazo katika tovuti ya Udom Juni 30, wanafunzi hao wanatakiwa kuripoti chuoni kesho saa nne asubuhi isipokuwa 15 wanaosubiri uamuzi wa mamlaka husika kabla ya kurejeshwa.

Aidha, katika tangazo hilo lililotolewa na Ofisi ya Makamu Mkuu wa Chuo, wanafunzi ambao wanadaiwa ada, gharama za malazi, mitihani na gharama nyingine, hawatakubaliwa kurejea.
“Kwa taarifa hii, wanajulishwa kuwa usajili utafanyika Jumamosi tarehe 02/07/2011 na Jumapili tarehe 03/07/2011 tu.

Kila mwanafunzi anatakiwa kuja na nakala halisi za vithibitisho vya malipo ya ada na gharama nyingine ambazo alikuwa anadaiwa,” ilieleza taarifa hiyo ya Makamu Mkuu wa Chuo.

Ilieleza kuwa mwanafunzi ambaye hatatimiza masharti hayo, hatapokewa chuoni; na kwamba mitihani itaanza Jumatatu.

Awali, ilikuwa ianze Juni 20 hadi Julai 14.

Taarifa hiyo iliwataja wanafunzi 15 watakaopewa taarifa zao binafsi na mamlaka husika ni Salumu Tindo, Edwin Tairo, Pascal Ngaiza, Baraka Messo, Very Melchiory, Vincent Emmanuel, Alfred Boniface, Alex Mushi, Geofrey Msangi, Samora Julius, Romano
Baradyana, Moses Goodness, Bakari Seleman, Hassan Ally na Mustafa Shaaban.

Kwa maelezo hayo, bila shaka wanafunzi hao wanasubiri maelekezo kutoka kwa Kamati ya Nidhamu juu ya ushiriki wao katika mgomo na maandamano yaliyofanyika hivi karibuni.

Aidha, taarifa hiyo ilieleza kuwa sehemu maalumu ya mapokezi na usajili, itakuwa kwenye kiwanja cha mpira wa miguu kilichoko meta 200 kutoka Ofisi za Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dodoma (Duwasa), mkabala na zinapojengwa ofisi za Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Hivi karibuni, wanafunzi hao walisimamishwa baada ya kuanzisha maandamano na vurugu kwa siku mbili wakishinikiza malipo yao ya masomo kwa vitendo.

Makamu Mkuu wa Udom, Profesa Idris Kikula, aliliambia gazeti hili mwishoni mwa wiki kwamba hata kabla ya kufukuzwa kwa wanafunzi hao, chuo kilishapanga kuwataka wanafunzi wote kulipa madeni wanayodaiwa na chuo, hivyo yeyote atakayekuwa anadaiwa hatapokewa hata kama hana hatia.

Akizungumzia jinsi ya kurudi chuoni, alisema Kamati ya Nidhamu ilikuwa inakutana na kuchambua wanaodaiwa kuhusika na wasiohusika katika mgomo.

Alisema wanafunzi wa mwaka wa tatu wasio na hatia watarudi mapema iwezekanavyo ili wafanye mitihani yao ya mwisho na kurejea kwao; wakati awamu ya pili, watarejea wa miaka mingine wasio na hatia kisha watakaogundulika kuwa na hatia, watapewa nafasi ya kujitetea ili haki itendeke kisha watarejea chuoni.

Alisema hatua hiyo pia itahusisha wanafunzi wa Shule ya Elimu ya Sayansi ya Habari (CIVE) waliofukuzwa chuoni miezi mitatu iliyopita, kwa kusababisha vurugu na maandamano.

Akizungumzia idadi ya wanafunzi waliofukuzwa, alisema kabla ya kufungwa kwa chuo hicho, wanafunzi 400 waligundulika kuwa vinara wa kuhamasisha migomo na maandamano huku wengine wakiomba kuondoka.

Alisema baada ya chuo kuwasimamisha wanafunzi hao, ndipo wengine walijichanganya na kuanza kufanya vurugu wakitaka hao wengine wasiondoke, hivyo kusababisha chuo kufungwa na wanafunzi zaidi ya 9,000 kusimamishwa masomo.

Katika hatua nyingine, uongozi wa Udom umepokea na kuidhinisha mapendekezo ya Kamati ya Menejimenti ya Rasilimaliwatu ya kupandisha vyeo watu sita wa Utawala na watatu wanataaluma.

Wanataaluma waliopandishwa vyeo ni Dk. Macheyeki kutoka Mhadhiri kuwa Mhadhiri Mwandamizi; Profesa Gesase kutoka Profesa Mshiriki kuwa Profesa kamili na Dk. Mtalikwa kutoka Mhadhiri Mwandamizi kuwa Profesa Mshiriki

Alhamisi, 28 Aprili 2011

Advantages and Disadvantages of Online Degrees

Advantages and Disadvantages of Online Degrees
Today’s lifestyle is quite busy for everybody and hence for reasons like promotion, career advancement, and for learning purpose all of us are in search of online education. Many students are choosing online education for pursuing their degrees. Almost 60 percent of the students complete their courses successfully and that is because they are aware of the advantages of online degrees. Any university that is accredited, awards online degrees to students on various fields. Online degrees are offered for almost all the subjects like Political Science, Finance, Business Administration, Law, Engineering, Accounting, Economics, Mathematics, Graphic Designing, History and Medicine too.

The only difference from an online degree and the traditional degree is the way of teaching. As an online degree student, you will attend classes, will work on projects, will ask questions and discuss with the professors and will also appear for examinations, but only through a virtual environment. Your classroom will have bulletin boards and text chats and at times you may have virtual workgroup for problem solving. Depending on your online degree program, you will have synchronous and asynchronous sessions.

Enrolment for online degrees can be done by filling the online admission forms. You will have the choice to select the cost effective university and the university with more online degree programs.

The main advantage of earning an online degree is the learning environment. Wherever you are, as long as you are connected to the Internet, your online degree follows with you. If you can properly mange your time then your online degree sessions will fit in your busy schedule. Your degree program can also be completed with your pace of study. Online degree offers you the benefit to attend classes from your home or any convenient location of yours. You can also apply to any university of any country that offers online degree programs. With these online degree programs available nobody can use excuses like unable to pursue education. Most of the online degree courses can be completed within the stipulated period or shorter than this when compared with the similar types of degree programs that are campus-based. Only you can delay your course completion, if you did not do time management properly. Even monetarily you can save a lot by opting online degree like the tuition fee will be lesser than campus-based degree and the credit hours will also be comparatively less. Most of your learning materials will be of downloading format and so you can save lot of time and money by studying online degree courses.

There are disadvantages of online education if you don’t fit as a right candidate for the online degree. You have to properly manage your time with family, work and study. Your planning for the sessions are very important and so studying on your pace will increase the duration of online degree completion. Since the learning materials will be in text and downloadable format, you should be comfortable with reading and if your choice is listening, then you have to reconsider the decision of obtaining online degree. Your discussion forums and chats are very important for communication and knowledge of using it is very essential. As the online education’s key channel of communication is Internet, it will be disadvantage to you if you don’t know its usage. You should understand the advantages of online degrees and the important factors that affect your decision in pursuing online degrees.
You can get exhaustive information on various online degree programs offered by world’s reputed institutions on http://www.counselorinternet.info/ . You can also visit http://www.onlineloanhelp.info/ for tips and sources to obtain student loans.