Jumatatu, 6 Julai 2015

WALUGULU WAPATA CHIFU MPYA, NI KUNGALU WA 15. NI BAADA YA KINGALU WA 14 KUFARIKI DUNIA TAREHE 1/7/2015 NA KUZIKWA TAREHE 2/7/2015 KIJIJINI KINOLE MOROGORO.


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia kusimikwa kwa Kiongozi mpya wa kabila la Waluguru Chifu Kingalu wa 15 katika kijijini Kinole mkoani Morogoro Alhamisi Julai 3, 2015 kufuatia kifo cha Chifu Kingalu wa 14 aliyefariki Jumatano jijini Dar es salaam na kuzikwa siku ya pili kijijini hapo.
Kiongozi mpya wa kabila la Waluguru Chifu Kingalu wa 15 akitolewa nje baada ya kusimikwa rasmi kuwa kiongozi wa kabla hilo kijijini Kinole mkoani Morogoro Alhamisi Julai 3, 2015 kufuatia kifo cha Chifu Kingalu wa 14 aliyefariki  Jumatano jijini Dar es salaam na kuzikwa kijijini hapo.

Kiongozi mpya wa kabila la Waluguru Chifu Kingalu wa 15 akichomeka fimbo yake ya Uchifu kabla ya kuketi  meza Kuu na Rais Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kusimikwa rasmi kuwa kiongozi wa kabila hilo kijijini Kinole mkoani Morogoro Alhamisi Julai 2, 2015 kufuatia kifo cha Chifu Kingalu wa 14 aliyefariki jana Jumatano jijini Dar es salaam na kuzikwa  kijijini hapo.Picha na IKULU

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni