Jumanne, 14 Julai 2015

PASTOR KALU ATANGAZA NIA MBIO ZA UBUNGE MBEYA VIJIJINI KUPITIA CCM...


MWANDISHI WA HABARI KALULUNGA AJITOSA MBIO ZA UBUNGE MBEYA VIJIJINI‏

Mwandishi wa Habari, Gordon Kalulunga akizungumza katika viwanja vya mahubiri alipokuwa akitangaza nia ya kugombea Ubunge jimbo la Mbeya vijijini.

Kalulunga akitaja vipaumbele vyake

Katibu wa Umoja wa Vijana Wilaya ya  Mbeya vijijini, Siulanga  akiwaasa Vijana kumuunga mkono kijana mwenzao.

Kalulunga akisalimiana na mmoja wa wazee waliojitokeza kumsikiliza alipokua akitangaza nia

Baadhi ya wanachama wapya wakikabidhiwa Kadi

Vijana wakiserebuka

Burudani zikiendelea
Wananchi wakimsikiliza Kalulunga

MWANDISHI wa habari wa gazeti la Mtanzania kutoka Mbeya, Gordon Kalulunga amejitosa kuingia kwenye kinyang’anyiro cha Ubunge katika Jimbo la Mbeya vijijini kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi(CCM).

Kalulunga alitangaza kuingia kwenye mchakato wa kugombea kuteuliwa na Chama ili aweze kupeperusha bendara katika uchaguzi mkuu ujao katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jana kwenye viwanja vya mahubiri Mbalizi mkoani Mbeya.

Mtia nia huyo alisema endapo Chama chake kitampitisha na hatimaye kushinda Ubunge katika Jimbo hilo atahakikisha wananchi wote wanajiunga na mfuko wa bima ya afya kwa ajili ya matibabu kwa kila kaya kuchangia ili kupunguza adha na gharama kubwa za matibabu.

Aliongeza kuwa akifaniiwa kuukwaa Ubunge pia atasimamia kuhakikisha Jimbo hilo linapata Chuo cha aina yoyote kikiwemo Chuo cha ufundi kwa ajili ya vijana kupata elimu jambo lilatalopunguza wimbi la ukosefu wa ajira kwa vijana.

Kalulunga alisema kipaumbele kingine atakachoshughulikia ni pamoja na kupigania ujenzi wa ofisi za makao makuu ya Wilaya hiyo katika eneo husika ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi tofauti na ilivyosasa ambapo Ofisi za Wilaya ya Mbeya zipo katikati ya Jiji la Mbeya.

Awali Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Mbeya vijijini, Japheti Siulanga aliwataka vijana wote kuungana ili kumuunga mkono kijana mwenzao aliyejitokeza na kuonesha nia ya kutaka kuongoza akiwa Mbunge wa jimbo hilo.

Aidha katika mkutano huo vijana zaidi ya 26 walijiunga na Chama cha mapinduzi na kukabidhiwa kadi za umoja wa Vijana.
CREDITS;MBEYA YETU BLOG

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni