Jumamosi, 9 Novemba 2013

JAMANI TUNAKWISHA, AJALI ZA PIKIPIKI ZIMERIPOTIWA SANA JUMA HILI, TUELIMISHANE NA KUKUMBUSHANA KUCHUKUA TAHADHARI.

 
Toyota Land Cruiser linalodaiwa kumgonga muendesha pikipiki aliyetambulika kwa jina moja la Huweso.
 

...Askari wa usalama wa barabarani akichukua maelezo katika eneo la tukio, alielala chini ni Huweso baada ya kupata ajali.

Picha mbili za juu zinaonesha ajali iliyotokea juzi Ihumwa Dodoma ikisababisha vifo vya vijana wawili Ramadhan Lesso na George Lwandala ambao walikuwa wanafunzi wa CBE Dodoma, chanzo cha ajali ni mwendokasi na lori kupaki bila alama zozote kando ya barabara kuu ya Morogoro-Dodoma. Wanafunzi hao waliligonga lori kwa nyuma na kufariki papo hapo.


Ajali nyingine ya pikipiki imetokea juzi huko Geita ikihusisha mwendesha bodaboda na abiria wake wa kike ambao hawakufahamika majina yao kuanguka katikati ya barabara na baadae kukanyagwa na gari aina ya Noah waliyokuwa wanapishana nayo.
RAI
Kila mtu kwa nafasi yake ajaribu kufanya wajibu wake ikiwa ni kuelimisha waendesha bodaboda kwenda kwa mwendo wa tahadhari na wastani ili ikitokea tatizo la ghafla waweze kudhibiti, wenye magari waheshimu wenye vyombo vidogo barabarani kama bajaj na pikipiki pia abiria wajaribu kuwadhibiti madreva wao wanapoona wanaenda kwa kasi sana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni