Jumatatu, 25 Februari 2013

MANCHESTER CITY WAIFUNGA CHELSEA 2-0

Man City yailemea Chelsea 

Wachezaji wa Manchester City
Mabingwa watetezi wa kombe hilo Manchester City wameandikisha ushindi mkubwa dhidi ya mabingwa wa ulaya Chelsea na hivyo kufufua matumaini yao ya kuhifadhi kombe hilo kwa mwaka wa pili, licha ya kukabiliwa na upinzani mkali kutoka wa vinara wa ligi hiyo kwa sasa Manchester United.
Mechi hiyo iliyokuwa na mashambulizi na kila aina ya vivutio baina ya timu hizo zinazomilikiwa na matajiri wawili tofauti,imemalizika kwa ushindi wa Man City wa mabao mawili kwa bila.
Mabao ya kipindi cha pili ya Yaya Toure na Carlos Tevez yalitosha kuizamisha Chelsea, na kufufua matumaini ya Man City, kutetea taji lao ambalo sasa linaonekana kuwa mikononi mwa majirani zao Manchster United wanaoongoza ligi wakiwa na tofauti ya point 12.
Mapema kipindi cha pili, Chelsea, walipata penati baada ya Demba BA, kuangushwa katika eneo la hatari na mlinda mlango wa Man City, Joe Hart, lakini penati iliyopigwa na nahodha wa Chelsea, Frank Lampard, ilipanguliwa Joe Hart na kuamsha mashambulizi zaidi ya Manchester City.
Wachezaji wa Newcastle
Yaya Toure kunako dakika ya 63 alipenyeza shuti la wastani pembeni mwa lango la Chelsea na kuwafanya Manchester City, kuongoza kwa bao moja kabla Chelsea, kufanya juhudi za kutaka kusawazisha lakini wakajikuta wanoangezwa bao la pili maraidadi kabisa lililofungwa na Carlos Tevez ambaye aliingia akitokea benchi,huku likiwa bao lake la kwanza baada ya mechi sita alizocheza bila kuifungia timu yake.
Kwingineko,katika mchezo mwingine wa leo, Newcastle wakiwa nyumbani,walitoka nyuma baada ya kufungwa bao la mapema na kuchomoza na ushindi wa mabao manne kwa mawili dhidi ya Southampton.
Mabao wa Newcastle yamefungwa na Musa Sisoko,Papis Demba Cisse,Yohan Cabaye aliyefungwa kwa mkwaju wa penati huku bao la nne watakatifu au Southampton wakijifunga.
Mabao ya Southampton yalifungwa na Morgan Scheneiderlin dakika tatu tu baada ya mchezo kuanza huku bao la pili likifungwa na Rickie Lambert.

Jumatatu, 11 Februari 2013

NIGERIA NDIO MIAMBA WAPYA WA KOMBE LA MATAIFA HURU YA AFRIKA(CAN)

Nigeria 1 Burkina Faso 0: Mba's fine strike ends 19 years of hurt as Super Eagles win third Africa Cup of Nations title

By David Kent
Nigeria claimed their third African Nations Cup title with a dominant performance over Burkina Faso in Johannesburg.
Sunday Mba fired the Super Eagles ahead with a superb volley five minutes before the break after a period of pressure saw Burkina Faso, competing in their first final, succumb to Stephen Keshi's side.
Cup of joy: A jubilant Nigeria squad hoist the Africa Cup of Nations trophy aloft for the third time
Cup of joy: A jubilant Nigeria squad hoist the Africa Cup of Nations trophy aloft for the third time
Always in control: Sunday Mba flicked the ball over a defender with his right, before firing home the only goal of the final with his other foot
Always in control: Sunday Mba flicked the ball over a defender with his right, before firing home the only goal of the final with his other foot, sparking gleeful celebrations (below)
Winner: Sunday Mba is congratulated by Nigeria team-mates after firing the only goal of the game

Wilfried Sanou came close to levelling for the Stallions midway through the second half but his brief flash of brilliance was extinguished by a top-drawer save by Vincent Enyeama.
It was Nigeria's first final since 2000 but they were hot favourites ahead of the match against the minnows from west Africa due to their 12-game unbeaten record.
Fancy seeing you again: Nigeria coach Stephen Keshi grabs the Africa Cup of Nations trophy after winning the competition as a player in 1994
Fancy seeing you again: Nigeria coach Stephen Keshi grabs the Africa Cup of Nations trophy after winning the competition as a player in 1994
Safe hands? Vincent Enyeama clings on despite pressure from Prejuce Nakoulma
Safe hands: Vincent Enyeama clings on despite pressure from Prejuce Nakoulma

MABADILIKO YA HALI YA HEWA; MAREKANI KASKAZINI YAKABILIWA NA BARAFU INAYOFIKIA SM 100, MAGARI YAFUNIKWA.


Snow-covered vehicles sit on Commonwealth Avenue in the Brighton neighborhood of Boston on Saturday.
Hiyo milima inayoonekana ni magari yaliyofunikwa na theluji katika moja ya mitaa ya mji wa Boston huko Marekani jana.

Jumapili, 10 Februari 2013

KOMBE LA MATAIFA HURU YA AFRIKA(CAN); MALI YACHUKUA NAFASI YA TATU BAADA YA KUIBUGIZA GHANA 3-1

Mali 3 Ghana 1: Eagles repeat 2012 third-place playoff win against Black Stars

By Andy James
Mali defeated Ghana 3-1 to finish third in the Africa Cup of Nations on Saturday, overcoming the Black Stars for the second consecutive year in the consolation match. 
Striker Mahamadou Samassa opened the scoring with a header in the 21st minute, captain Seydou Keita added to the lead with a close-range shot in the 48th, and Sigamary Diarra sealed the victory in stoppage time, ending Mali's emotional campaign. 
Kwadwo Asamoah scored for Ghana in the 82nd minute. Ghana striker Wakaso Mubarak missed a penalty early in the second half.

MATCH FACTS

Mali: Soumaila Diakite, Diawara, Salif Coulibaly, Adama Coulibaly, Tamboura, Ousmane Coulibaly, Kalilou Traore, Mahamane Traore, Mahamadou Samassa (Sigamary Diarra 78), Keita, Diabate.
Subs Not Used: Mamadou Samassa, N'Diaye, Wague, Maiga, Sissoko, Idrissa Coulibaly, Cheick Diarra, Yatabare, Sow, Samba Diakite, Yirango.
Booked: Tamboura.
Goals: Mahamadou Samassa 21, Keita 48, Sigamary Diarra 90.
Ghana: Dauda, Richard Boateng, Vorsah, Boye (Mensah 46), Afful, Wakaso, Awal, Asamoah, Asante, Atsu (Adomah 70), Gyan (Clottey 75).
Subs Not Used: Agyei, Pantsil, Annan, Agyemang-Badu, Derek Boateng, Rabiu, Akaminko, Boakye, Kwarasey.
Booked: Wakaso, Vorsah, Asante.
Goals: Asamoah 82.
Att: 6,000
Ref: Eric Otogo-Castane (Gabon).
Latest Africa Cup of Nations results, fixtures and stats
Last year, Mali beat Ghana 2-0 in the third-place playoff. They entered this year's tournament with players saying they were motivated to bring joy to fans enduring political instability and fighting back home.
Saturday's loss at the Nelson Mandela Bay Stadium added even more disappointment for Ghana, after they reached the semi-finals for the fourth straight time but left without the title once again. 
Ghana were consigned to the third-place match after losing the semi-final to Burkina Faso on penalties. The Black Stars won the last of their four titles in 1982. 
Mali were trying to make it to the final for the first time in more than 30 years but their hopes of a first title ended after a 4-1 defeat to Nigeria in the semis.
The Malians dedicated this latest uplifting campaign to their conflict-torn home country, where French troops are fighting Islamist extremists. 
Samassa scored with a diving header from near the penalty spot after a breakaway down the left, and former Barcelona player Keita netted his third goal of the tournament with an easy finish from close range after a cross from the right. 
Keita scored again in the 72nd minute but the goal was ruled because the offside flag was up. 
Ghana pulled a goal back near the end with a long-range left-footed shot that curled to fool Mali goalkeeper Soumaila Diakite, who was his team's hero in the penalty shootout against host South Africa in the quarter-finals.
Cruising: Former Barcelona midfielder Seydou Keita doubled Mali's lead just after half-time
Cruising: Former Barcelona midfielder Seydou Keita doubled Mali's lead just after half-time

Ijumaa, 8 Februari 2013

MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI APUNGUZWA SPIDI. NI KWA SHERIA MPYA ILIYOPITISHWA NA BUNGE.

 
SERIKALI imewasilisha bungeni mapendekezo ya mabadiliko katika Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Umma ya 2008, huku ikiongeza vifungu ambavyo vinapunguza nguvu ya Bunge katika kushughulikia taarifa ya Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Marekebisho hayo yamo kwenye Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Sheria, namba 3 ya mwaka 2012 (The Written Laws - Miscellaneous Amendments Bill) uliowasilishwa bungeni jana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema.
Kwa mujibu wa Ibara ya 143 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, CAG anawajibika kuwasilisha taarifa yake kwa Rais ambaye baada ya kuipokea atawaagiza watu wanaohusika wawasilishe taarifa hiyo kwenye kikao cha Bunge kilicho karibu.
Taarifa hiyo inabidi iwasilishwe katika kikao hicho kabla ya kupita siku saba tangu siku ile kilipoanza kikao hicho.
Sheria ilivyo sasa inaelekeza kuwa baada ya ripoti hiyo kuwa silishwa bungeni itajadiliwa katika kamati tatu zinazosimamia Hesabu za Serikali kwa ajili ya kuifanyia uchambuzi, kisha kuwasilisha taarifa zake bungeni katika muda zitakazopangiwa.
Kamati hizo za Bunge ni zile za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na Hesabu za Serikali Kuu (PAC) ambazo hufanya uchambuzi kisha kusoma taarifa zake ndani ya Bunge kwa hatua zaidi.
Hata hivyo, marekebisho yaliyowasilishwa Bungeni jana na Jaji Werema yanapendekeza kubadili utaratibu mzima wa kushughulikia taarifa hiyo, kwani yanaongeza vipengele, “vinavyoliwajibisha Bunge kwa Serikali” badala ya kinyume chake.
Serikali imeongeza vipengele vya ziada ambavyo vinazitaka kamati za Bunge zinapofanya uchambuzi wa ripoti ya CAG, kupeleka maazimio yake kwa Serikali ili “yatafutiwe majawabu” badala ya utaratibu wa sasa wa kupeleka hesabu zake bungeni.
Kimsingi Kamati za Bunge hufanya kazi kwa niaba ya Bunge, hivyo taarifa zake husomwa Bungeni na siyo kwingineko kama ambavyo marekebisho ya sheria yanataka kuelekeza.
Jaji Werema alisema: “Marekebisho haya yamefanywa ili kumwezesha Waziri wa Fedha kuwasilisha taarifa ya majibu ya Serikali ya hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali”.
Ikiwa Bunge litapitisha marekebisho hayo ni dhahiri kwamba Bunge halitakuwa tena na uwezo wa kuwawajibisha watendaji wa Serikali ambao watabainika kuhusika na upotevu wa fedha au kufuja fedha za umma, hivyo kupunguza uzito wa mjadala na uwezo wa wabunge kuhoji.
Kadhalika taarifa za LAAC, POAC na PAC kuhusu taarifa ya CAG na mapendekezo ya kamati hizo, yatajadiliwa sambamba na majibu ya Serikali. Hivyo hakutakuwa na nafasi ya Bunge kutekeleza wajibu wake wa kuisimamia Serikali kama inavyoainishwa katika Katiba.
Hatua hiyo ni sawa na kulifunga Bunge mikono kutokutekeleza wajibu wake kuhusu ripoti ya CAG, kwani kwa mujibu wa sheria halitaweza kujadili chochote hadi Serikali kupitia kwa Mlipaji Mkuu (Paymaster General) atakapokuwa ametoa majibu ya utetezi kuhusu kasoro katika ripoti hiyo.
Chanzo; Gazeti la Mwananchi

Jumapili, 3 Februari 2013

MOHAMMED MORSI RAIS WA MISRI ASHINDWA KUFAIDI MATUNDA YA MAPINDUZI, IKULU YALINDWA DHIDI YA WAANDAMANAJI.

Askari wa kupambana na fujo wa Misri wamewekwa kwa wingi nje ya ikulu ya rais mjini Cairo baada ya mapambano ya Ijumaa usiku baina ya wanajeshi na waandamanaji waliowatupia mabomu ya petroli.

Walinzi nje ya ikulu ya rais mjini Cairo

Muandamanaji mmoja alikufa baada ya kupigwa risasi na zaidi ya 50 walijeruhiwa.
Maandamano hayo ambayo piya yalifanywa katika miji mengine kadha ya Misri, ndio ya karibuni kabisa katika mfulululizo wa maandamano ya kumpinga Rais Mohammed Morsi wa chama cha Muslim Brotherhood.
Upinzani unamlaumu kuwa amepindukia madaraka yake.
Televisheni imeonesha matokeo ya maandamano ya jana usiku, mawe na takataka zimejaa mabarabarani