Jumapili, 29 Julai 2012

HATARI JAMANI, WABUNGE WALA RUSHWA, TUTAENDELEA KWELI NCHI HII!!!?

SPIKA AVUNJA KAMATI YA NISHATI, WAZIRI AELEZA WALIVYOITAFUNA TANESCO
Kizitto Noya na Boniface Meena, Dodoma
WAKATI wabunge wakitoa tuhuma nzito dhidi ya wenzao wanaodaiwa kujihusisha na ufisadi ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), imebainishwa kuwa wabunge wenye tabia hiyo ni watano, watatu kutoka chama tawala CCM na wawili upinzani.

Habari zilizopatikana jana mjini Dodoma zimeeleza kuwa baadhi ya wabunge hao wanatoka katika Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, huku wengine wakitoka Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma. 

Kwa mujibu wa taarifa hizo, wabunge hao wamedaiwa kuwa wamekuwa wakitumia nafasi zao za ubunge na ujumbe wa kamati kufanya biashara na Tanesco na kutetea mafisadi ndani ya shirika hilo la umma.

Gazeti hili limefanikiwa kupata majina ya wabunge hao, ambayo leo hatutayataja kwa sababu za kitaaluma. 

Baadhi ya wabunge waliochangia hoja hiyo bungeni juzi na jana walisema kuwa, wanawafahamu wabunge hao kwa majina, lakini hawapendi kuwataja kwa kuwa siyo wakati mwafaka.

Moto wa kutaka kutajwa kwa majina ya wabunge hao ulikolezwa jana na Mbunge Vita Kawawa wa Namtumbo(CCM) aliyeomba Mwongozo wa Spika, akitaka jambo hili lijadiliwe na Bunge na kupendekeza kuwa, Kamati za Bunge zinazotuhumiwa kwa rushwa zivunjwe.

 “Waheshimiwa wabunge wamejadili suala hili kwenye wizara, lakini kwa mujibu wa kifungu cha 55 (3)f  mbunge au waziri anaweza kutoa hoja ili jambo fulani lijadiliwe. Sasa naomba kutoa hoja ya kujadili suala hilo," Kawawa alisema.

Aliliomba pia Bunge likubali kuivunja na kuiunda upya Kamati ya Nishati na Madini na kamati nyingine zilizolalamikiwa kwa rushwa. Hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge. 

Baada ya hoja hiyo kuungwa mkono Spika wa Bunge, Anne Makinda alisimama na kukubali hoja hiyo ya Kawawa na kutangaza kuivunja Kamati ya Nishati na Madini.

Spika Makinda alisema ameiagiza Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge kutengeneza kanuni za kuwadhibiti wabunge wenye tabia hiyo ya kupokea rushwa kutoka kwa watu mbalimbali ili kutimiza matakwa yao binafsi.

"Ninakubali kuivunja Kamati ya Nishati na Madini na zingine ambazo zitatajwa kwenye tuhuma hizo. Nalipeleka pia suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, halafu kama ni kutajwa (wabunge hao), basi tutapata mwongozo wa kamati hiyo." alisema Spika Makinda na kuongeza:

"Nasema kwa dhati kabisa, kitendo hiki hakikubaliki ndani ya Bunge hili. Wabunge mkae vizuri. Kama kuna baadhi yetu wanaenda huku na huku kujitafutia masilahi binafsi, tutawezaje kuisimamia Serikali?"

Mbunge Zedi
Baada ya Spika kutangaza kuvunja Kamati ya Nishati na Madini, Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Seleman Zedi alisema kuwa ameshtushwa na uamuzi huo na anasubiri uamuzi wa Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge. 

"Nimeshtushwa sana na uamuzi huo, lakini tusubiri Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge," alisema Zedi.

Waziri Muhongo
Akihitimisha hoja ya wizara yake bungeni jana, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema kuwa baadhi ya wabunge ambao wanashiriki kwenye vikao vya uamuzi vya Tanesco kama wajumbe, wamekuwa wakilihujumu shirika hilo kwa njia mbalimbali ikiwamo kufanya nalo biashara.

"Shirika liliwahi kulipa Pauni za Uingereza 50,000 kwa ajili ya kununua vipuri, lakini kilicholetwa nchini ni masanduku ya misumari,” alisema Profesa Muhongo na kuongeza;

“Hata katika nguzo za umeme kuna biashara inaendelea. Tunajua kuwa nguzo hizo zinazalishwa Iringa na kupelekwa Mombasa kisha kurudishwa nchini kwa maelezo kwamba zimetoka Afrika Kusini." 

Waziri Muhongo alisema kuwa mbali na ufisadi huo, baadhi ya wabunge ambao ni wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini wamewahi kuliuzia shirika hilo matairi ya magari kwa bei kubwa, bidhaa ambayo hata hivyo alisema haina ubora unaokubalika.

"Baadhi ya wabunge wanafanya biashara na Tanesco; niseme tu kuwa, hii siyo sahihi. Lakini niombe kwamba mjadala huu tuufunge kwa sababu, tayari tumekabidhi suala hilo kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)" alisema Waziri Muhongo.

Waziri Muhongo pia alizungumzia jinsi baadhi ya watu na kampuni zinavyoiibia Tanesco kupitia mita za Luku ambapo aliwataja  watu hao kuwa ni pamoja na Shule za St. Mary's zinazodaiwa Sh10.5 milioni, Access Bank, Tawi la Tabata Matumbi Sh13.8 milioni na Hoteli ya Akudo Paradaise ya Kariakoo inayodaiwa Sh25.5 milioni.

Alisema kuwa baada ya kubainika kwa wadaiwa hao hutumia umeme kinyume na utaratibu,wahusika  wote walikamatwa na kufikishwa kituo cha polisi baada ya kufanyika kwa uchunguzi.

“Baada ya kufanya uchunguzi na kubaini kuwapo kwa watu wanaotumia umeme bila kulipia na kuisababishia Tanesco hasara, tumeamua kuwachukulia hatua ikiwamo kuwafikisha polisi,” alisema Profesa Muhongo na kuongeza:

“Inaonyesha wazi kwamba wizi wa umeme wa Luku umekuwa ukifanyika mara kwa mara na kwamba baada ya kuwakamata hawa, uchunguzi utaendelea na wengine watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.”

Jenista Mhagama

Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama alisema kuwa, amepokea kwa masikitiko taarifa hizo za wabunge wa CCM kuingia katika tuhuma hizo, lakini akasema namna nzuri ya kushughulikia tatizo hilo ni vyombo vya dola kufanya uchunguzi makini ili kujiridhisha na kisha hatua za kisheria kufuatwa.

"Ni taarifa mbaya kwa kweli, lakini mimi niiombe Serikali itusaidie kufanya uchunguzi ili ukweli ubainike na hatua zichukuliwe," alisema Mhagama.

YANGA BINGWA WA KOMBE LA KAGAME KWA MARA NYINGINE TENA.



Timu ya Yanga yaibuka bingwa wa kombe la Kagame yaifunga Azam kwa bao 2-0

Jumamosi, 28 Julai 2012

BEI YA KUUNGANISHA UMEME IMESHUSHWA NA SERIKALI

NI KWA WALE WASIOHITAJI NGUZO, WA NGUZO MBILI KUTOZWA SH 800,000, WAZIRI MUHONGO, ASEMA MGAWO SAFARI HII HAUKUBALIKIBoniface Meena, Dodoma
 
SERIKALI imetangaza kushusha gharama za kuunganisha umeme kwa wananchi wanaohitaji huduma hiyo kwa viwango ambavyo ni kati ya asilimia 60 na 77 kwa wakazi wa vijijini na kati ya asilimia 29 na 65 kwa wananchi waishio sehemu za mijini.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo aliliambia Bunge jana kuwa gharama za kuunganishiwa umeme kwa wateja walioko kwenye umbali usiozidi meta 30 (single phase) ambao hawahitaji nguzo sasa zitakuwa Sh177,000 kwa wateja wa vijijini na mijini itakuwa Sh320,960 badala ya Sh455,108 ambazo zilikuwa zikilipwa awali bila kujali mteja aliko.

Akiwasilisha hotuba ya makadirio ya matumizi ya wizara yake ya 2012/2013 bungeni Dodoma jana, waziri huyo alisema punguzo hilo ni sawa na asilimia 61.11 kwa wateja waishio vijijini na asilimia 29.48 kwa wateja waishio mijini.

Profesa Muhongo alisema pia Serikali imeshusha gharama za uunganishaji wa umeme kwa wateja watakaojengewa njia moja (single phase) na kuwekewa nguzo moja katika maeneo ya vijijini ambao sasa watalipa Sh337,740 na mijini Sh515,618 badala ya Sh1,351,884 zilizokuwa zikilipwa awali.
“Punguzo hilo la pili ni sawa na asilimia 75.02 kwa wateja wa vijijini na asilimia 61.86 kwa wateja waishio mijini,” alisema Profesa Muhongo.

Alisema kwa wateja watakaojengewa njia moja na kuwekewa nguzo mbili katika maeneo ya vijijini watalipa Sh454,654 na mijini watalipa Sh696,670 badala ya Sh2.001 milioni zilizokuwa zikilipwa awali.

“Punguzo hili ni sawa na asilimia 77.28 kwa wateja waishio vijijini na asilimia 65.19 kwa wateja waishio mijini,” alisema Profesa Muhongo na kuongeza. “Viwango hivyo vya gharama vitaanza kutumika Januari mwakani bila kisingizio.”

Chimbuko la Punguzo
Hatua ya kushushwa kwa gharama za kuunganishiwa umeme zimekuja zaidi ya mwaka mmoja tangu Rais Jakaya Kikwete alipolilekeza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kupunguza gharama hizo ili kupata wateja wengi zaidi.

Machi 18 mwaka jana, Rais Kikwete aliitaka Tanesco, kupunguza gharama za kuunganisha umeme kwa wananchi ili wengi wapate huduma hiyo sambamba na kuongeza wateja wanaotumia umeme kwa asilimia 30 ifikapo mwaka 2015.

Akizungumza na wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini, Rais Kikwete alisema gharama hiyo ikipunguza, itaiwezesha Tanesco kupata wateja wengi ikilinganishwa na sasa.
Kauli ya Rais ilitokana na maelezo ya Mkurugenzi wa Shirika hilo, William Mhando (ambaye sasa amesimamishwa kazi) kuwa Tanesco ilikuwa ikifanya mazungumzo na Benki za Akiba na Azania ili zitoe mikopo kwa wateja kwa ajili ya kuunganishiwa umeme.

Kadhalika Mei 16 mwaka huu, akizungumza na Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt Profesa Muhongo alisema: “Kipaumbele cha wizara kwa sasa ni kupata umeme wa uhakika wa bei nafuu na unaotabirika. Ni muhimu kuongeza watumiaji wa umeme kwa kuwa kwa sasa kwa takwimu za Tanesco ni asilimia 18.4 tu ya Watanzania wanaopata huduma hii.”

Wizi Tanesco Profesa Muhongo aliwataka wezi wa umeme kujisalimisha kabla hawajakamatwa kwani hata wakijificha watakamatwa tu. Alisema upotevu wa umeme unafanywa na baadhi ya wananchi wanaoshirikiana na wafanyakazi wa Tanesco kwa kushirikiana na vishoka. “Kuna rushwa iliyokithiri Tanesco, kuna wezi wanaowaunganishia watu umeme na kuliibia shirika, wakae chonjo kwani watakamatwa tu,” alisema Profesa Muhongo. kuhusu wizara hiyo, alisema mambo mengi yatafanyika kwa uwazi na haoni sababu za kila jambo kuwa ni siri. “Mnakaribishwa wizarani kila mtakapoona mambo yanakwenda ndivyo sivyo, hatutakuwa na mambo ya kuficha tutakuwa wawazi,” alisema Profesa Muhongo.

Mgawo wa Umeme
Kuhusu suala la mgawo wa umeme, alisema hautakuwepo tena na haukubaliki kamwe.
“Waheshimiwa wabunge, suala la mgawo haliwezekani na halikubaliki,” alisema Profesa Muhongo. Alisema katika mwaka 2011/12, wizara iliendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme nchini. Profesa Muhongo alisema hadi Juni, 2012 uwezo wa mitambo ya kufua umeme (installed capacity) ulikua megawati 1,375.74 (gesi asilia ikiwa ni asilimia 40, maji asilimia 41 na mafuta asilimia 19).

“Uwezo huo ni ongezeko la megawati 367 sawa na asilimia 36 ikilinganishwa na uwezo wa megawati 1,013.74 uliokuwepo Juni, 2011. Mahitaji ya juu ya umeme kwa mwaka 2011/12 yalifikia wastani wa MW 820.35 ikilinganishwa na MW 730 kwa mwaka 2010/11,” alisema.

Alisema Julai, 2011 wakati wa Bajeti ya wizara hiyo ilipowasilishwa, nchi ilikuwa katika mgawo wa umeme... “Mgawo huo ulitokana na upungufu wa umeme wa takriban megawati 300 uliosababishwa na upungufu wa maji katika mabwawa kwenye vituo vya kufua umeme. Kutokana na hali hiyo, Serikali ililazimika kuandaa mpango wa dharura wa kuondoa mgawo wa umeme nchini ulioridhiwa na bunge.” Alisema katika mpango huo, megawati 572 zilipangwa kuzalishwa na kuingizwa kwenye gridi ya taifa. Alisema hadi kufikia Juni, mwaka huu uwezo wa ufuaji wa umeme kutokana na mpango huo wa dharura ulifikia megawati 422.

“Mitambo hiyo inajumuisha Symbion megawati 137, Aggreko megawati 100, IPTL megawati 100 na mtambo wa gesi asili wa Ubungo megawati 150," alisema. Alisema kutofikiwa kwa kiwango kilichokusudiwa,  kunatokana na kukosekana kwa mitambo ya megawati 150 ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) iliyokadiriwa kugharimu Dola za Marekani 162 milioni sawa na Sh256.20 bilioni. Alisema hadi kufikia mwishoni mwa Juni, mwaka huu lengo la kuondoa mgawo wa umeme lilifikiwa kwa asilimia 100.

WAJUA HISTORIA YA MCHEZO WA OLIMPIKI!!?

Michezo ya Olimpiki

Bendera ya Olimpiki yaonyesha pete tano

Michezo ya Olimpiki ni mashindano ya michezo makubwa duniani inayofanyika kila baada ya miaka minne.
Michezo ya Olimpiki imekuwa na historia ndefu katika vipindi viwili:
  • Michezo ya Olimpiki ya Kisasa ya kwanza ilitokea mwaka 1896 mjini Athens (Ugiriki). Mwanzishilishaji alikuwa Mfaransa Pierre de Coubertin alitaka kutumia kielelezo cha michezo ya kale kwa kujenga uhusiano mzuri kati ya vijana wa nchi mbalimbali na kuwapatia nafasi ya kushindana kwenye uwanja wa michezo badala ya uwanja wa vita. Coubertin alianzisha Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (International Olympic Committee - IOC).
Michezo hii ya kisasa imeendelea kila baada ya miaka minne isipokuwa 1916, 1940 na 1944 kwa sababu ya Vita Kuu ya Kwanza na ya Pili ya Dunia.
Michezo ya kisasa hufanyika katika mji mwingine kila safari. Michezo ya 2004 ilifanyika Athens, ya 2008 huko Beijing na ya 2012 itafanyika London.
Kuna tofauti kati ya michezo ya kiangazi na michezo ya majira ya baridi.
Washindi watatu wa kwanza wa kila mashindano hupewa medali ya dhahabu, fedha au shaba.

Ijumaa, 27 Julai 2012

AZAM FC NA YANGA KUKUMBANA KIPUTE CHA FAINALI KAGAME CUP JUMAMOSI HII.

YANGA SC YAILAZA APR, YATINGA FAINALI KOMBE LA KAGAME


Kikosi cha Yanga kilichoanza mechi ya leo.
TIMU ya Yanga SC imefanikiwa kuingia Fainali ya Michuano ya Kombe la Kagame leo baada ya kuilaza timu ya APR ya Rwanda bao 1-0 kwenye mchezo wa Nusu Fainali uliochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Bao la Yanga limefungwa na mchezaji Hamis Kiiza katika muda wa nyongeza baada ya dakika 90 kumalizika 0-0. Kwa matokeo haya, Yanga itakutana na Azam FC katika fainali itayochezwa Jumamosi Julai 28, 2012 katika Uwanja wa Taifa.

Jumatano, 25 Julai 2012

LEO NI SIKU YA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WETU MBALIMBALI WALIOTETEA TAIFA HILI, SHEREHE ZAADHIMISHWA SEHEMU MBALIMBALI TANZANIA.

MAADHIMISHO YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 Rais Dkt. Jakaya Kikwete, akiweka Ngao  na Mkuki kwenye Mnara wa Mashujaa, wakati wa maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa, iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo.
Mkuu wa Majeshi, Davis Mwamunyange akitoka kuweka silaha ya jadi kwenye Mnara wa Mashujaa, wakati wa maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa, iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo, kuhudhuria sherehe za maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa, leo.
 Kutoka (kushoto) Rais Dkt. Jakaya Kikwete, Mkuu wa Majeshi, Davis Mwamunyange, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Idd, Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi,  Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Pandu Ameir Kificho....., Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Said Meck Sadiq,  wakiwa katika viwanja vya Mnazi  Mmoja wakihudhuria sherehe za maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa, leo.
 Sehemu ya wageni waalikwa na Mabalozi wa nchi mbalimbali waliohudhuria maadhimisho hayo.
 Askari wa Jeshi wakishiriki katika maadhimisho hayo, hapa wakiweka silaha begani.
 Ni ishara ya kutoa heshima kwa Mashujaa wapiganaji.
 Rais Dkt. Jakaya Kikwete, akisalimiana na baadhi ya wazee waliopigana vita mbalimbali vya ukombozi wa nchi ya Tanzania, waliohudhuria katika maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa, iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya wazee waliopigana vita mbalimbali vya ukombozi wa nchi ya Tanzania, waliohudhuria katika maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa, iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, leo.
 Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, akiomba dua kwa niaba ya waislam wakati wa maadhimisho hayo leo.
 Kiongozi wa dini ya kikristo, Mchungaji Kamoyo, akiomba sala kwa niaba ya wakristo wakati wa maadhimisho hayo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, wakati akiondoka kwenye uwanja wa Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo baada ya kuhudhuria sherehe za maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa.
SHEREHE ZA SIKU YA KUWAKUMBUKA MASHUJAA ZA FANA MKOANI RUVUMA
Jeshi la Wananchi JWTZ wakipita mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Sabit Mwambungu Kutoa heshima katika Kuadhimisha siku ya Mashujaa kakaka Viwanja vya Maenge Manspaa ya Songea
Gwaride la JWTZ likitoka Nje baada ya Kumaliza shuguli za Siku ya Kuwa kumbuka mashujaa walio kufa wakati wa vita na mashujaa walio nyongwa na wajerumani na kuzikwa katika kaburi moja watu 27 .
Picha ya Askari wa Vita vya Nduli Iddi Amini Dada ikiwa ni ukumbusho kwa asikari walio enda Uganda kuwa komboa waganda pamoja na kuokoa eneo lililo tekwa na Iddi Amini Dada
Askari wa Mawasiliano JWTZ wakiwaburudisha waliofika viwanja vya Mashujaa kuadhimisha siku ya Mashujaa
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma akiwa na Bregedia wa kanda ya kusini katika siku ya kuwa kumbuka Mashujaa viwanja vya Mashujaa Mahenge
Meya wa Manispaa ya Songea Charles Mhagama wa pili kutoka kushoto akiwa mmoja wawatu walio hudhuria siku ya Mashujaa
Mkuu wa wilaya ya Songea Joseph Joseph Mkirikiti akiwa katika Viwanja vya Mashujaa Mahenge wakwanza Kulia

MARANDA NA FALIJALA WAFUNGWA MIAKA MITATU JELA KWA KESI YA EPA

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, imemhukumu kifungo cha miaka 18 jela Kada wa CCM, Rajabu Maranda na binamu yake, Farijala Hussein katika kesi ya tuhuma za kuchota Sh2.2 bilioni za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Rajab Maranda na binamu yake Farjala Hussein(mwenye jezi ya bluu)
Mahakimu wawili katika jopo la waliokuwa wakisikiliza kesi hiyo waliwatia hatiani watuhumiwa kwa makosa sita kati ya saba yaliyokuwa yakiwakabili na kuwahukumu kifungo cha miaka mitatu jela kwa kila kosa.

Kwa upande wake kiongozi wa jopo hilo, Jaji Fatuma Masengi aliwaachia huru washtakiwa hao kwa maelezo kwamba upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha mashtaka yote saba yaliyokuwa yanawakabili.

Hata hivyo, hukumu hiyo haikuweza kuwaokoa watuhumiwa na hasa Farijala na Maranda watatumikia adhabu yao kwa miaka mitatu jela kwa kuwa adhabu zote walizopewa zitakwenda kwa wakati mmoja.

Tayari Maranda na Farijala wanatumikia kifungo kingine cha miaka mitano jela, baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa Sh1.8 bilioni za EPA, ambapo walihukumiwa na mahakama hiyo Mei 23, 2011.

Jopo lagawanyika
Jopo la mahakimu watatu lililokuwa likisoma hukumu hiyo liligawanyika na kusoma hukumu mbili tofauti, ambapo hukumu moja iliyoandaliwa na kusomwa na kiongozi wa jopo hilo, Jaji Masengi aliyewaachia huru washtakiwa.

Hata hivyo, katika hukumu ya pili, iliyoandaliwa na Hakimu Projestus Kahyoza na mwenzake Catherine Revocate iliwatia hatiani washtakiwa katika makosa sita kati ya saba yaliyokuwa yakiwakabili, na kuwahukumu kifungo cha miaka mitatu kwa kila kosa.

Hata hivyo, wakati wakisoma hukumu hiyo, mahakimu hao walisema badala ya washtakiwa kutumikia kifungo cha miaka 18, hukumu yao itaenda sambamba hivyo watatumikia kifungo cha miaka mitatu jela.

Kabla ya hukumu
Kabla ya hukumu hiyo kutolewa, hakimu Kahyoza na mwenzake walipitia ushahidi uliotolewa na mashahidi sita wa upande wa  mashtaka  akiwamo mtaalamu wa maandishi, Joseph Mgendi ambaye aliweza kuangalia saini katika nyaraka halisi na zinazodaiwa kughushiwa,  ikiwamo hati ya usajili  ambapo alibainisha kuwa zilikuwa zimeghushiwa.

Pia walipitia utetezi uliotolewa wa mshtakiwa Maranda, ambaye aliyakana mashtaka yote saba yanayowakabili na kwamba, alikataa katakata kuwa hakuwahi kula njama na kughushi hati ya usajili wa Kampuni ya Money Planners & Consultant.

Hakimu Kahyoza alisema, Maranda alidai kuwa yeye hakuwahi kwenda Brela kusajili kampuni hiyo na kwamba, aliyewahi kwenda kusajili kampuni ni binamu yake, Farijala.

Hakimu Kahyoza alisema, Maranda katika utetezi wake alisema yeye hakuwahi kughushi hati yoyote hivyo, haikuwa rahisi kwake kutoa hati iliyoghushiwa pia, hakuwahi kuiba fedha BoT na wala hakuwahi kujipatia fedha yoyote kwa njia ya udanganyifu.

Kahyoza alifafanua kwamba, Maranda alidai mfumo uliotumika kuwaingizia fedha kwenye akaunti yao iliyopo katika Benki ya CBA uliendeshwa kihalali ndiyo maana, BoT hawakuwahi kulalamika hivyo, aliiomba mahakama imuone hana hatia.

Akisoma utetezi uliotelewa na Farijala, Hakimu Kahyoza alisema, Farijala naye alikataa  madai ya kughushi, kuwasilisha nyaraka bandia benki, kuiba fedha yoyote na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na aliiomba mahakama imwachie huru kwa sababu hana hatia.

Yasiyo na utata
Hakimu Kahyoza alisema kuwa mahakama ilibaini kuwapo kwa masuala yasiyokuwa na utata ambayo ni pamoja na kwamba Maranda na Farijala ni ndugu, waliwahi kufanya biashara pamoja na waliingiziwa fedha kwenye akaunti namba 0101379004 ya United Bank of Africa ambazo ni kiasi cha Sh2.2 bilioni.

“Baada ya kuweka msingi huo, mahakama ilijiuliza je, washtakiwa walikula njama ya kuiibia  BoT, walighushi hati ya usajili wa kampuni namba 150731, walighushi hati ya mkataba kati ya Kampuni ya Money Planners & Consultant  na Kampuni ya B. Grancel ya nchini Ujerumani, waliwasilisha nyaraka za kughushi benki, waliibia BoT na kwamba je, walijipatia fedha kwa njia ya udanganyifu,” alihoji Kahyoza.

Hakimu huyo alisema kwa kuzingatia ushahidi uliotolewa,  hakuna utata kuwa hakuna mahali panapoonyesha washtakiwa ndiyo walikuwa wamiliki wa kwanza wa kampuni hiyo Money Planners & Consultant na kwamba majina yanayodaiwa kuwa ni wamiliki wa kampuni  hiyo ya Thobias  Kitunga na Paulo  ni majina ya uongo na ya kufikirika.

Alisema licha ya majina hayo kuwa ya kufikirika, mabadiliko ya kampuni hiyo ya Money Planners & Consultant hayakuwahi kufanyika na hata Brela hakuna kumbukumbu, hivyo saini zilizopo katika nyaraka za kampuni hiyo ikiwamo hati ya usajili ni za kughushi.

Alisema sababu ya kuthibitisha hilo ni kwamba, ofisi ni ileile iliyopo Magomeni Mapipa, Mtaa wa Iramba nyumba namba 7 hata baada ya mabadiliko.

“Hati hizo za usajili hazikusainiwa na Msajili wa Biashara toka Brela, Noel Shani bali zilisainiwa na washtakiwa wenyewe. Hivyo, kwa mujibu wa kifungu cha 333 na 335 (c) (e) vimetufanya tufikie hitimisho kuwa  washtakiwa walighushi nyaraka hizo,” alisema Hakimu Kahyoza.

MASHINDANO YA OLYMPIC YANAANZA IJUMAA HII, MJI WA LONDON WAKUMBWA NA MSONGAMANO WA MAGARI BAADA YA NJIA ZINGINE KUTENGWA KWA MATUMIZI YA WANAMICHEZO TU..

Motorists faced widespread gridlock this morning as drivers were excluded from 30 miles of controversial reserved VIP ‘Games Lanes’ in the capital - and the threat of a £130 fine if they go into them.
As Olympic planners prepared for Friday's opening ceremony, 'Games Lanes' came into force across London, causing inevitable traffic chaos on already busy road networks, as well as delays on the London Underground as those trying to escape queues opted for public transport.
Police warned that London's roads are already 'at capacity', while motorists told of rush-hour gridlock, including queues of cars travelling at just 10mph along the eastbound stretch of the M4 from Heathrow into London.
There were a number of heavily-congested hot spots around London during the rush-hour, with the M4 and A4 approach in west London twice as busy as normal according to traffic analysts.
Standstill: Road networks in London already creaking under rush-hour traffic saw even more queue chaos as the Games Lanes went live
Standstill: Road networks in London already creaking under rush-hour traffic saw even more queue chaos as the Games Lanes went live
Sign of things to come: As the Olympic Games Lane officially opened around London this morning, there was predictable traffic gridlock, including on this stretch of the M4 near Hammersmith, west London
Sign of things to come: As the Olympic Games Lane officially opened around London this morning, there was predictable traffic gridlock, including on this stretch of the A4 near Hammersmith, west London
Aside from the occasional errant motorist, the majority of road users decided not to risk a fine in the Games Lanes, sitting instead in gridlocked traffic
Aside from the occasional errant motorist, the majority of road users decided not to risk a fine in the Games Lanes, sitting instead in gridlocked traffic


Later estimates by the AA put the rush-hour tailbacks at around 12 miles on the western approach into London.
There were also hold-ups for motorists on the A12 at the Lea Interchange in east London and at the A13 Canning Town Flyover.
 

The A40 around Ealing and at Westway in west London was also congested, while Grosvenor Place in Victoria in central London and the Hyde Park Corner Junction were also busy.
Other areas of London where there were rush-hour jams included Tower Bridge and Baker Street.
On the Tube, there were severe rush-hour delays today on three Underground lines, two days before the start of the Olympics.
One of the affected lines was the Metropolitan which will carry thousands of people to Wembley Stadium for Olympic football matches.
Confusion: In some areas of London, it appeared unclear as to whether the Games Lanes were operational, with some motorists risking a fine by straying into them to beat the traffic
Confusion: In some areas of London, it appeared unclear as to whether the Games Lanes were operational, with some motorists risking a fine by straying into them to beat the traffic

Chaotic: Even official Olympic vehivles found themselves struggling into central London this morning as rush hour and the Games Lanes combined to give motorists headaches
Chaotic: Even official Olympic vehivles found themselves struggling into central London this morning as rush hour and the Games Lanes combined to give motorists headaches
 
Jammed: An AA Roadwatch image from around 8.45am today shows the extent of the traffic problems, with the M4 from Heathrow being particularly chaotic
The Cabinet minister responsible, Jeremy Hunt, admitted: ‘The next 48 hours are absolutely critical.’
But despite pleas by the Prime Minister for ministers not to use the lanes he also did not rule out taking advantage of them himself – though only when on official business and for ‘operational and security’ reasons, he insisted: ‘It might happen from time to time.’
Culture, Media, Sport and Olympics Secretary Mr Hunt denied this was a ‘cop-out’ and stressed that if going to the Games purely for the ‘enjoyment’ of watching the sport he would use public transport like everyone else.
Across the capital in east London, motorists queued along the A12 near Leyton, as the Games Lane remained completely clear
Across the capital in east London, motorists queued along the A12 near Leyton, as the Games Lane remained completely clear

Speaking on BBC News 24, Transport Secretary Justine Greening said it was not surprising there had been some disruption to traffic on the day the lanes became operational.
'There will be a lot of disruption and London is a congested city anyway.'

The AA said the Games Lanes will make traffic in London 'pretty hectic', adding that the best way for motorists to keep ahead of delays is to watch temporary signs which show when the lanes are live and inactive.
Despite the reported lengthy delays, Locog claimed there was minimal disruption.
Debbie Jevans, Locog's director of sport, said: 'The traffic has moved, the Olympic lanes have worked well this morning and athletes have gone to the venues and are training as they have been for a week now.
Speaking at the Olympic Park, Jackie Brock-Doyle, Locog's director of communications, added: 'London is moving well this morning.'
Commuters have also had to contend with the hot weather this week, as soaring temperatures led to speed restrictions on rail services.
Yesterday, the ultra-hot weather led to speed restrictions on Greater Anglia services which meant some trains did not stop at Stratford, the closest station to the Olympic Park in east London.
Today, speed restrictions were in place on First Great Western services in and out of Paddington station in London. Trains were not running between Paddington and Greenford in west London.
 
Going live: The occasional motorist was spotted in the Games Lane, while left, a cyclist on the Marylebone Road in central London took his chances Going live: The occasional motorist was spotted in the Games Lane, while left, a cyclist on the Marylebone Road in central London took his chances
Motorists will be told which roads have active Games Lanes through 150 temporary signs placed around the capital.
Londoners and road users took to Twitter this morning to describe the condition of the roads as the Games Lanes opened.
One user, James Shrager, said: 'The #gameslane on the m4 is an embarrassing joke. There isn't one on the elevated section and it's a car park. Poor athletes.'
The lanes have been nicknamed ‘Zil lanes’ after the limousines used to ferry communist leaders in specially reserved lanes from the Kremlin during the Soviet era in Russia.
One of the most notorious symbols of Whitehall’s  war on the motorist - the controversial M4 Bus lane – sprang back to life a week ago as the first ‘Games Lane’ ferrying VIPs from Heathrow Airport to the Olympic village and the capital’s top hotels.
A Downing Street spokesman said: ‘Ministers will be using public transport to get to the Games wherever possible, unless particular operational or security reasons mean that cars are required.
Warning: Drivers now face a £130 fine if they stray into the designated Games Lanes from now on
Warning: Drivers now face a £130 fine if they stray into the designated Games Lanes from now on

Jumatatu, 23 Julai 2012

RAIS JAKAYA KIKWETE AMEZINDUA MRADI MKUBWA WA MAJI JIJI LA MBEYA, NI MSAADA TOKA JUMUIYA YA ULAYA.

MAJISAFI ALIYOZINDUA RAIS KIKWETE MBEYA YANASAFISHWA NA MCHANGA KUTOKA NJE YA NCHI

RAIS JAKAYA KIKWETE AKIWA ANAKATA UTEPE KWA FURAHA IKIWA NI ISHARA YA KUZINDUA MRADI WA MAJI ENEO LA SWAYA JIJINI MBEYA LEO, MRADI HUO UMEGAHRIBU ZAIDI YA SH.BILIONI 75.5. KULIA AKISHUHUDIWA NA WAZIRI WA MAJI PROF.MAGHEMBE, MKUU WA MKOA WA MBEYA ABBAS KANDORO NA WENGINE

MH. RAIS AKISALIMIANA NA BAADHI YA WAWAKILISHI WA JUMUIYA YA ULAYA

HILI NI MOJA YA ENEO LA MRADI

Jumapili, 22 Julai 2012

Alhamisi, 19 Julai 2012

ASKARI 3,000 KUAJIRIWA NA JESHI LA POLISI MWAKA HUU WA FEDHA.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akiwasilisa bungeni makadirio na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2012/2013, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi
Waandishi Wetu
JESHI la Polisi litaajiri askari wapya 3,000 wengi wao wakiwa wasomi kutoka taasisi za elimu ya juu.
Akiwasilisha makadirio ya Bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2012/13 katika kikao cha Bunge, Dodoma jana, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi alisema:


“Sehemu ya waajiriwa itapatikana kutoka katika shule na vyuo vya elimu ya juu na idadi nyingine kutoka vijana wa JKT (Jeshi la Kujenga Taifa). Utaratibu huu unalenga kuwa na askari wenye sifa stahiki na waaminifu kwa kazi ya Polisi.”


Alisema polisi wataendelea kuongeza ufanisi katika upelelezi wa makosa ya jinai na kwamba mwaka 2012/2013 litatumia vyuo vyake vya Dar es Salaam na Kidatu kutoa mafunzo kwa askari wa kufanya kazi hiyo.


Dk Nchimbi alisema mafunzo hayo ya ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa za kiintelijensia na mbinu za kisasa za upelelezi, zitatolewa kwa maofisa, wakaguzi na askari wapatao 1,000.


Wakimbizi kurejeshwa makwao
Waziri huyo alisema Serikali inakamilisha taratibu za kuwarejesha makwao wakimbizi wapatao 40,000, wengi wao kutoka Burundi, ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.


Hadi kufikia Aprili 30, mwaka huu, Tanzania ilikuwa na wakimbizi 112,645 wakiwamo Warundi 48,195, Wakongo 62,632, Wasomali 1,548 na wakimbizi wa mataifa mengine 270.


Hatua ya kuwarejesha makwao wakimbizi itawezesha kufungwa kwa Kambi ya Mtabila, Kigoma yenye wakimbizi 38,800, ambayo inapaswa kuwa imefungwa ifikapo Desemba 31, mwaka huu.
“Katika mwaka 2011/12, idadi ya wakimbizi wa Burundi kutoka kambi hiyo waliorejea kwao ni 155 tu, hali iliyosababisha kambi hiyo kutofungwa,” alisema Dk Nchimbi na kuongeza:


“Mkakati mpya wa kufunga kambi hiyo ni kwamba limefanyika zoezi la mahojiano ya kina na wakimbizi hao kwa lengo la kubaini kama wapo wakimbizi wenye sababu za msingi za kuendelea kuwepo nchini.”
Alisema mahojiano hayo yalifanyika kati ya Septemba na Desemba mwaka jana na kwamba matokeo yanaonyesha kwamba 33,705 hawana sababu za msingi za kuendelea kuwa wakimbizi na wengine 2,045 walionekana kuwa na sababu za msingi.


Malumbano yaendelea
Malumbano yameendelea kulitikisa Bunge baada ya jana Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Utaratibu na Bunge), William Lukuvi kukatisha hotuba ya Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Vicent Nyerere akidai  inazungumzia mambo ambayo yako Mahakamani.


Nyerere alisoma bajeti yake baada ya ile iliyosomwa na Waziri Nchimbi lakini, wakati akiendelea, Lukuvi aliomba mwongozo wa Spika, Anne Makinda na kisha kuomba hotuba hiyo isitishwe.
Kitendo hicho kilisababisha mabishano ya kikanuni huku wabunge wakitunishiana misuli na kushindana kwa utaalamu wa kujua vifungu vya sheria na kanuni za Bunge.


Hii ni mara ya pili kwa Serikali kuzuia hotuba za wizara hiyo kutoka Kambi ya Upinzani. Mara ya kwanza ilikuwa katika hotuba ya Makadirio ya Mwaka jana (2011/12) ambapo aliyekuwa Waziri Kivuli wa Wizara hiyo, Godbless Lema alizuiwa kusoma hotuba yote.


Jana, baada ya Waziri Lukuvi kuwasilisha ombi lake, alisimama Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu ambaye alisema haikuwa haki kwa Serikali kukatisha hotuba hiyo kivuli na kwamba kitendo hicho kinakwenda kinyume cha utamaduni wa Bunge.


“Kama ambavyo Serikali imeachwa ikasoma hotuba yake yote, msemaji wa kambi ya upinzani Bungeni naye aachwe asome na aeleze kile ambacho ni maoni ya kambi, tangu kuanza kwa Bunge hili na mabunge yaliyopita, si utamaduni kukatisha hotuba ya upinzani,” alisema Lissu.


Lissu alisema wapinzani wamekuwa wakinyanyaswa na kwamba kuzuiwa kwa hotuba yao mara kadhaa, ni mbinu za kuwafanya wasieleze kwa Watanzania uovu unaofanywa na Serikali.


Baada ya hapo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema alisimama na kueleza kuwa anaunga mkono hoja ya Lukuvi kwa kuwa maelezo yaliyoko katika ukurasa wa nne wa hotuba ya upinzani yalitakiwa yakasemwe polisi.


“Mheshimiwa Spika, nasikitika kusema kwamba humu ndani ukurasa wa tatu kuna jambo ambalo jana (juzi) jioni ulitolea uamuzi kwa kutumia Kanuni ya 48 na nina imani kuwa waheshimiwa wabunge ambao wanajua hizi kanuni za kwenye vitabu watakubali kuwa hili jambo si la kujadili kwenye hotuba,” alisema Werema.


Alisema suala jingine ni la Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Peter Msigwa na kwamba liko mahakamani na hata suala la Dk Steven Ulimboka nalo liko mahakamani.
“Naunga mkono hoja ya Waziri wa Nchi kwamba maneno haya yasiingie naomba kutoa hoja,” alisema Werema, huku akisema kuwa Lissu ni mtovu wa nidhamu.


“Yaliyoko mahakamani nasema hapana na ninasisitiza yote yaliyoko mahakamani kweli hapana. Yaliyoko mahakamani hapana. Waheshimiwa wabunge naomba tuwe na heshima lakini yaliyoko mahakamani nasema hapana.” alisisitiza Jaji Werema.


Baadaye alisimama Spika Makinda na kusema yale yote ambayo yako mahakamani hatayaruhusu yajadiliwe hivyo yatolewe. Alitaka yatajwe ili yasijadiliwe... “Sijui ni yapi yako mahakamani kwa hiyo naomba mniambie ili niyajue.”


Lukuvi alisimama na kuyataja kuwa ni suala la Msigwa, Dk Ulimboka na lile lililojitokeza hivi karibuni huko Iramba Magharibi ambako mtu mmoja aliuawa katika vurugu zilizotokea kwenye mkutano wa hadhara wa Chadema.


Baadaye Mbunge wa Nyamagana (Chadema), Ezekiah Wenje alisimama na kusema pamoja na kuwa yeye si mwanasheria, kanuni zinasema hairuhusiwi kuzungumzia mwenendo wa mahakama hivyo, kinachozungumziwa ni maelezo ya kesi zilizopo mahakamani.


“Spika naomba uelewe na unisikilize kwa makini ili uelewe, sehemu ambazo Werema na Lukuvi wamezisoma wamezitafsiri kwa mitizamo yao, naweza kusema wako guided by narrow interpretation (wanaongozwa na tafsiri finyu),”alisema Wenje.


Malumbano hayo yalimsimamisha pia Mbunge wa Bariadi Mashariki (UDP), John Cheyo akitumia Kanuni ya 76(1) na (2) akitaka hoja hiyo isitishwe ili jambo hilo liangaliwe na kujua mambo yapi yako mahakamani.


“Spika mimi nadhani watu wanataka haki itendeke, ubishi uliopo hivi sasa unaweza ukaahirishwa na kwamba tukaahirisha hoja hii ili kuangalia ni mambo gani yaliyopo mahakamani,” alisema.
Hata hivyo, Makinda alisema mvutano haukuwa umefikia hatua ya kuahirisha Bunge na badala yake, aliitaka Kamati ya Maadili na Madaraka ya Bunge kukutana na kulitolea uamuzi jambo hilo kama maneno yaliyoandikwa na upinzani yako mahakamani basi hayatasomwa lakini, kama hayako mahakamani watarudia kuyasoma.


Ataka Waziri, Naibu waonje rumande


Katika hatua nyingine, Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe alipendekeza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi na Naibu Wake, Pereira Ame Silima wawekwe rumande walau kwa miezi sita ili waonje adha ya hali mbaya katika mahabusu nchini.


“Bunge hili lipitishe uamuzi, waziri na naibu wake wakae jela hata miezi sita tu pengine wataweza kufahamu hali ilivyo mbaya katika mahabusu zetu. Hali ni mbaya kwelikweli na tunaposema tunamaanisha wala hatutanii,” alisema Filikunjombe.


Aliitaka Serikali kuongeza fedha zaidi ili kuliwezesha Jeshi la Polisi kununua silaha za kisasa: “Polisi hawana silaha zozote kuwawezesha kupambana na uhalifu na badala yake limeachiwa virungu ambavyo huvitumia kupigia wanafunzi, wakati wa migomo na maandamano ya Chadema,” alisema Filikunjombe.


Mbunge huyo alipendekeza kuwa ni bora jeshi hilo likasukwa upya na kupunguza ukubwa wake, ili kuliwezesha kuwa dogo lakini lenye silaha za kisasa zaidi kuliko kuwa na jeshi kubwa lenye silaha za kizamani.


Habari hii imeandikwa na Neville Meena, Boniface Meena na Habel Chidawali, Dodoma

Jumatano, 18 Julai 2012

AJALI NYINGINE YA MELI KUZAMA IMETOKEA ZANZIBAR LEO MCHANA. NI MV SKAGIT SEAGUL, SMZ IMETANGAZA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO.

 

Wakazi wa Zanzibar wakiwa wamekusanyika katika Bandari ya Malindi mjini Unguja Zanzibar jioni ya leo wakati miili ya baadhi ya abiria wa Boti ya Kampuni ya Seagull "MV Skagit" wakitolewa baada ya boti hiyo kuzama na kupoteza maisha ya watu zaidi ya 200 hii leo ikitokea jijini Dar es Salaam.
Askari wa JWTZ wakiwa wamejipanga wakati wa zoezi la kupokea maiti.
Moja ya maiti ikiwa imebebwa na askari

Maiti ingine ikiwa imebebwa...
Ni hali ya huzuni Visiwani humo na jijini Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla. Ajali hii imetokea ikiwa imepita miezi kadhaa baada ya meli nyingine ya Abiria kupoteza uhai wa watu visiwani humo.
Meli ya Mv Skagit iliyokuwa safarini kutoka Dar kuelekea Zanzibar imezama majira ya saa nane mchana hii leo katika maeneo Pungume na Chumbe baada ya kukumbwa na upepo mkali.

Meli hiyo inayosadikiwa kuwa na abiria 250 inasemekana imepindukia upande mmoja na huku abiria wengi wakiweza kuokolewa kutokana na jitihada mbali mbali kupitia vile vile msaada wa boti za Mv Kilimanjaro, Tug ya Bandari na vyombo vyengine.

Mpaka tunaandika taarifa hizi ni maiti tatu zilikwishapatikana na kiasi cha abiria 150 wameokolewa na waliojeruhiwa wanatibiwa katika Hospitali ya Mnazimmoja.

Taarifa zinaeleza kwamba kulikuwa na watoto takriban 30 na Watalii kutoka nchi mbali mbali wafikao kumi.

Wazamiaji kutoka Kikosi cha KMKM pamoja na Jeshi tayari wapo eneo la ajali kusaidia kuokoa maisha ya wananchi waliokumbwa na maafa haya

Jumapili, 15 Julai 2012

PICHA YA LEO; MWANAMAPINDUZI HALISI WA UCHUMI, HIVI KUPIGA KISHOKA ENZI ZILE ILIKUWA LAZIMA!!!?

Mwalimu J K Nyerere enzi hizo akiwa katika ziara ya kikazi wilayani Mafia, Land Rover 109 ndio ilikuwa gari imara inayopendekezwa kwa matumizi ya Serikali, tumetoka mbali.

Jumamosi, 14 Julai 2012

ALIYEMTEKA NA KUMJERUHI DK. ULIMBOKA AFIKISHWA MAHAKAMANI.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Suleiman Kova

ADAIWA KUWA NI RAIA WA KENYA, ALIKODIWA
Waandishi Wetu,

RAIA wa Kenya, Joshua Mulundi (21) amekamatwa na polisi jijini Dar es Salaam na kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za kumteka na kufanya jaribio la kumuua Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk Steven Ulimboka. Mtuhumiwa huyo alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana alasiri na kusomewa mashtaka mawili na Wakili wa Serikali, Ladslaus Komanya.

Wakili Komanya alidai mahakamani hapo kuwa Mulundi ambaye makazi yake ni Murang'a nchini Kenya kuwa, mnamo Juni 26, mwaka huu akiwa eneo la Leaders Club, jijini Dar es Salaam alimteka Dk Ulimboka.

Hata hivyo, kumetokea utata wa jina, umri wake na makazi ya mtuhumiwa huyo, kwani wakati hati ya mashtaka mahakamani inasema ni Joshua Mulundi mwenye umri wa miaka 21 na mkazi wa Murang’a nchini Kenya, taarifa ya Jeshi la Polisi imesema anaitwa Joshua Mahindi mwenye miaka 31 na mkazi wa Namanga nchini Kenya.

Katika shtaka la pili, Wakili Komanya alidai kuwa tarehe hiyohiyo mshtakiwa alifanya jaribio la kumsababishia kifo Dk Ulimboka kwa kumpiga katika eneo la Msitu wa Pande eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam, kinyume cha sheria.

Hata hivyo, mshtakiwa huyo alikana mashtaka hayo akidai kuwa makosa aliyoshtakiwa nayo siyo sahihi.

Hakimu Mkazi, Agnes Mchome alimwambia kuwa hatakiwi kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo, isipokuwa Mahakama Kuu pekee.

Hakimu Mchome aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 5,2012 itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Taarifa ya Polisi
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi mshtakiwa huyo anajulikana kwa jina la Joshua Muhindi (31), mkazi wa Namanga nchini Kenya. Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Suleiman Kova aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mshtakiwa huyo alikamatwa Juni 29 mwaka huu katika Kanisa la Ufufuo na Uzima lililoko Kawe baada ya taarifa kutoka kwa wasamaria wema.

Alisema raia huyo mwenye kitambulisho cha utaifa namba 29166938 kilichotolewa Oktoba 11, 2010 katika Wilaya ya Nyeri nchini Kenya, pia anamiliki hati ya dharura ya kusafiria yenye namba 0123431 iliyotolewa Juni 14, mwaka huu Namanga Kenya.
Kwa mujibu wa Kova, baada ya kuhojiwa na polisi, raia huyo alisema alikuja nchini Juni 23, mwaka huu kwa ajili ya kufanya tukio lililotokea Juni 25 mwaka huu na kwamba alijulishwa kuwa yeye na wenzake 12 ndiyo walipangwa kutekeleza tukio hilo.

Alisema raia huyo na wenzake walikuja nchini kwa ajili ya kumdhuru Dk Ulimboka, baada ya kukodiwa na mtu ambaye hakumtaja jina ambaye anaamini ni mtumishi wa Serikali.

“Baada ya kuhojiwa alidai kuwa yeye ndiye aliyehusika kumteka Dk Ulimboka na wenzake na baada ya utekaji huo wenzake waliondoka,” alisema Kova na kuongeza:

“Alisema walikuja kutekeleza tukio hilo kwa lengo la kujua ni nani anayemshawishi Dk Ulimboka na alipelekwa na mwenyeji wake asiyemtambua hadi katika hoteli moja katikati ya jiji.”

Alisema mtuhumiwa huyo na wenzake 12 wako kwenye kikundi kijulikanacho kama Gun Star chenye makao yake Iwiru Wilaya ya Thika nchini Kenya na kwamba kinaongozwa na mtu mmoja ajulikanaye kama Silencer akisaidiwa na Paft.
Alisema pia, mtuhumiwa huyo alidai kuwa, wamekuwa wakijihusisha na matumizi ya silaha na kwamba wamekuwa wakifanya matukio mengi ya kihalifu nchini Kenya.

Alisema baada ya utekaji huo, Juni 29 mwaka huu raia huyo alikwenda katika Kanisa la Ufufuo na Uzima lililoko Kawe kwa nia ya kutaka kuonana na kiongozi wa kanisa hilo Mchungaji Gwajima, lakini hakufanikiwa badala yake alionana na msaidizi wake ajulikanaye kama Joseph Marwa Kiriba.

“Alipoonana naye alimweleza kuwa yeye ni mwanachama wa Kikundi cha ‘Umafia’ na kwamba hukodiwa kufanya matukio ya kihalifu Kenya na nje ya mipaka,” Kamanda Kova alisema.

“Alikwenda katika kanisa hilo kwa ajili ya kufanya toba maana aliona alifanya kitendo cha kinyama hivyo aliona arudi ili akapate toba,” alisema.

Alisema jeshi hilo bado linaendelea na uchunguzi kwa ajili ya kuwatafuta watu wengine waliohusika na utekaji huo.
Katika hatua nyingine, jeshi hilo pia limewakamata watu wanane ambao wanadaiwa kuhusika na uvamizi wa mashamba katika eneo la Kawe.

Maandamano ya madaktari yazuia
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limepiga marufuku maandamano ya madaktari yaliyopangwa kufanyika Jumatatu ijayo kushinikiza mambo kadhaa ikiwamo kuundwa tume huru ya kuchunguza kutekwa, kuteswa na kutupwa katika Msitu wa Pande kwa Kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dk Steven Ulimboka.

Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Suleman Kova aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa maandamano hayo hayatafanyika kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo za kiusalama.

Alisema wamesitisha maandamano hayo kwa sababu madai ya madaktari tayari yameshashughulikiwa na Serikali.
“Tumesitisha maandamano kwa sababu tunahofia kunaweza kutokea uvunjifu wa amani maana Waislamu nao walipanga kuandamana kesho (leo),” alisema Kova.

Msimamo wa madaktari

Kauli hiyo ya Kova ilitolewa saa chache baada ya kikao cha zaidi ya madaktari 400 waliokutana katika mkutano wa dharura ulioitishwa na Chama cha Madaktari (MAT), ambako waliridhia kufanyika kwa maandamano hayo.
Katibu wa (MAT) Dk Rodrick Kabangila alisema katika kikao hicho, madaktari hao walipokea taarifa ya MAT iliyoeleza hatua zilizochukuliwa na Serikali dhidi ya wenzao waliofukuzwa.

“Madaktari wamepokea taarifa za wenzao kufanyiwa vitendo vya unyanyasaji, ikiwamo kufukuzwa katika makazi yao kwa kutumia Polisi wa Kutuliza Ghasia (FFU), kunyimwa chakula, posho na kuelezea kuwa vitendo hivyo ni vya unyanyasaji na uonevu dhidi ya taalamu na udaktari wenyewe,” alisema Dk Kabangila.

Dk Kabangila alisema kuwa, kufuatia hatua hiyo madaktari hao wamepitisha azimio la kufanya maandamano ya amani ambayo yanatarajia kushirikisha madaktari zaidi ya 800 hadi 1,000 na kutoa wito kwa wananchi wenye mapenzi mema na taaluma hiyo, kushiriki wakiwa na vitambaa vyeupe.

Akizungumzia msimamo wa polisi kuyazuia maandamano hayo, Dk Kabangila alisema uongozi wa madaktari utakutana kujadili tamko hilo la polisi.

“Tumepata barua inayozuia maandamano yetu. Barua hii imetoa sababu ambazo ni tofauti na sisi tulichoomba. Sisi (MAT) ndio tulioomba maandamano kwa ajili ya kuonyesha hisia zetu juu ya vitendo wanavyofanyiwa madaktari,” alisema Dk Kabangila.
Habari hii imeandaliwa na Geofrey Nyang’oro, Nora Damian na James Magai


JOHN TERRY ASHINDA KESI YA UBAGUZI KWA KUKOSEKANA USHAHIDI USIO NA SHAKA, KUKABILIANA NA KIBANO TOKA FA.

IT'S IMPOSSIBLE TO KNOW WHAT WAS SAID': CHIEF MAGISTRATE SAYS THERE WAS TOO MUCH DOUBT TO CONVICT FOOTBALLER OF RACIAL ABUSE

 
Fresh charges: Following the conclusion of the court case the FA is set to reopen its own inquiry to decide whether Terry and Ferdinand should face charges of bringing the game into disrepute

Howard Riddle's judgment:
'The prosecution has presented a strong case. There is no doubt that John Terry uttered the words 'f****** black c***' at Anton Ferdinand.
'When he did so he was angry. Mr Ferdinand says that he did not precipitate this comment by himself accusing Mr Terry of calling him a black c***. 
'Even with all the help the court has received from television footage, expert lip readers, witnesses and indeed counsel, it is impossible to be sure exactly what were the words spoken by Mr Terry at the relevant time.
'It is impossible to be sure exactly what was said to him at the relevant time by Mr Ferdinand. It is not only that all of this happened in a matter of seconds.
'For a small part of the relevant time, the camera's view of Mr Terry was obstructed. We do not have a clear camera view of Mr Ferdinand, sufficient to pick up exactly what he said.
'No matter how serious the incident looks now, and how crucial the exact wording is now, at the time it was secondary to the key witnesses. They are professional footballers in the final minutes of a game where the result mattered to them both.
'They would naturally concentrate on the game more than on exactly what had been said to them or by them. I have assessed John Terry as a credible witness.
'Weighing all the evidence together, I think it is highly unlikely that Mr Ferdinand accused Mr Terry on the pitch of calling him a black c***.
'However I accept that it is possible that Mr Terry believed at the time, and believes now, that such an accusation was made. The prosecution evidence as to what was said by Mr Ferdinand at this point is not strong.
'In those circumstances, there being a doubt, the only verdict the court can record is one of not guilty.'
Edited version. For the full transcript, click here. Warning strong language

Key moment: Terry and QPR's Anton Ferdinand clash during the Barclays Premier League match at Loftus Road
Key moment: Terry and QPR's Anton Ferdinand clash during the Barclays Premier League match at Loftus Road
Shell-shocked: Anton Ferdinand's mother, Janice (right), looks stunned as she leaves court after the ruling
Shell-shocked: Anton Ferdinand's mother, Janice (right), looks stunned as she leaves court after the ruling