Jumatatu, 31 Oktoba 2011

OKWI AANGUSHIWA JUMBA BOVU MSIMBAZI, MWAPE ASEMA NI BAO LA MUNGU TU

SIMBA WAWEWESEKA KWA KIPIGO CHA JUZI.

Hivi ndivyo mshambuliaji wa Yanga, Davies Mwape alivyofunga bao pekee dhidi ya Simba. Picha na Jube Tranquilino



Ibrahim Bakari
MUUAJI wa Simba, Davis Mwape amesema ni Mungu tu aliyemwezesha afunge katika mechi yao ya watani iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa juzi ikiwa ni mchezo wa Ligi Kuu.


Mwape alifunga bao pekee katika mchezo huo na kuifanya Yanga kufikisha pointi 24 nyuma ya Simba inayoongoza kwa pointi tatu.


Akizungumza katika mahojiano maalum baada ya mchezo juzi, Mwape alisema: "Ni Mungu kanipa nguvu za ajabu, kufunga katika mechi ngumu ni kazi yake, sikutarajia na wala sikuwa nafikiria kufunga.


"Nasema ni Mungu tu, Mungu amenisaidia sana,


namshukuru na nashukuru pia mashabiki na viongozi wangu na wao kwa kunipa nguvu...," alisema Mwape.


Mwape raia wa Zambia, alisema: "Naamini kile ninachokifanya uwanjani, najua nimecheza vizuri na ndiyo maana nikafunga najitahidi kufanya zaidi ili kufanya maajabu zaidi

NIMEIPENDA HOJA HII, NIMEIKUTA KWA MJENGWABLOG.

Hoja Yangu; Lay Man Ni Nani?

Madaktari wakifanya upasuaji mkubwa. Huwaita wote wasio na taaluma ya udaktari LAY MEN
Wanasheria wakiwa mahakamani. nao huwaita wote wasio wanasheria, LAY MEN
Mapadre na watu wa wakfu.huitwa wenye daraja, na wote wasio na daraja takatifu huitwa LAY MEN.


Wadau nimeshangazwa na madai a makundi haya kwenye jamii.ukitoa maoni kwenye masuala ya kisheria wakati wewe siyo mwanasheria, unaitwa Lay man na wenye fani yao.madaktari nao huwaita wasio madktari kuwa ni lay men, kadhalika na mapadre na watu wenye wakfu huwaita waamini wasio na wakfu lay men.sasa mimi najiuliza, LAY MAN ni nani? na kwa nini hizi profession tatu pekee ndizo zinaita wengine lay men. karibu tujadili
Na Mdau wa Mjengwablog
MAONI YANGU ni kuwa si taaluma hizo tatu tu kuwa huwaita wenzao Lay men, hata ukienda jeshi lolote leo hii eti wanatuita sisi tusio wanajeshi RAIA au Civillian utafikiri wao sio raia wa nchi hii, ukipita Chuo Kikuu kwenye Makongamano yao ndio kabisaa wanajiita WANATAALUMA utafikiri wewe husiye na digrii huna taaluma yoyote, hivyo nakubaliana na mbwembwe zote hizo haina shida, sababu ni kuwa wao ni marafiki wasomi(learned friends) na wamesota kuzipata sifa hizo, hivyo LAY MAN si tusi, ni mtu tu asiye na utaalamu wa kutosha juu ya fani fulani. Naomba kuwasilisha, ni maoni yangu tu Mkuu.

Jumamosi, 29 Oktoba 2011

YANGA YAIFUNGA SIMBA 1-0

Tegete wa Yanga.
Juma K Juma wa Simba.

Leo Simba imeshindwa kuunguruma mbele ya kandambili Yanga toka mitaa ya Twiga na Jangwani, mbele ya mashabiki kibao Simba imejikuta ikiloa kwa goli hilo moja katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom jioni hii ya leo, pole kwa watani wao wa jadi, ndio mpira huo, unadunda.


WAZIRI MKUU AMTEMBELEA ZITTO MUHIMBILI KABLA YA KUSAFIRISHWA INDIA JANA.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akimjulia hali mgonjwa Mh. Zitto Kabwe kabla ya kusafirishwa India kwa matibabu zaidi jana, hali ya Mheshimiwa Zitto si mbaya sana kwani alionekana akitembea mwenyewe kuelekea chumba cha VIP pale uwanja wa ndege wa Julius Nyerere wakati akisubiri kusafiri. Tunamuombea afya njema.

Ijumaa, 28 Oktoba 2011

SAIF AL ISLAM YUPO NIGER.

Colonel Gaddafi’s son Saif al-Islam has crossed the Libyan border into Niger, a senior official in the National Transitional Council said last night (Thur).
The official, who declined to be named for safety reasons, said: ‘There is a contact with Mali and with South Africa and with another neighbouring country to organise his exit.
‘He hasn’t got confirmation yet, he’s still waiting.’
After days of speculation the NTC has confirmed Said al-Islam has fled to Niger
After days of speculation the NTC has confirmed Said al-Islam has fled to Niger
Conflicting reports have arisen on an almost daily basis about his exact whereabouts, but this appears to be confirmation he has left Libya as many suspected he had.

A source with the NTC told Reuters the two surviving indictees were together, protected by Tuareg nomads.
Tuaregs were recruited by Gaddafi to fight as hired guns in Libya in the final months of the conflict.
'Saif is concerned about his safety,' the source said. 'He believes handing himself over is the best option for him

VIPIMO VYA UKIMWI VYA NYUMBANI VINATIA SHAKA.

Onyo juu ya vipimo vya Ukimwi

Moja ya aina ya kipimo cha nyumabani cha HIV.
Vipimo haramu vya nyumbani vya kupimia HIV vinawapa watu matokeo yasiyo sahihi, shirika la kudhibiti dawa na huduma za afya (MHRA) limeonya.
Limesema kuna matatizo mengine pia kwenye vipimo vya magonjwa ya zinaa ambayo ni halali lakini huenda pia vikawa si sahihi.
Chombo hicho kinaufanyia uchunguzi mtandao wa Uingereza unaouza vifaa hivyo.
Wakala wa kulinda afya umewaandikia baadhi ya walioathirika na kuwaeleza kuwa vipimo hivyo havikubaliki.

SIMU YA MKONONI YAMTAMBULISHA ALIYEKUFA KWENYE AJALI YA MOTO WA BASI.

Ajali ya basi iliyotokea juzi.

WAKATI mabaki ya miili ya watu 12 walioteketea kwa moto katika ajali ya basi la Deluxe yakizikwa jana, mmoja wa abiria waliokufa katika ajali hiyo, Salome Benjamin (24) alitoa simu yake itumike kutoa taarifa kwa ndugu zake.

Salome, mwanafunzi wa Chuo cha Mipango Dodoma, ameelezwa kuwa aliwapa mashuhuda hao simu hiyo na kuwataka wawasiliane na ndugu zake kwamba imeshindikana kwake kuokolewa hivyo wasihangaike.

Akisimulia jana jinsi mwanawe alivyokufa, baba mdogo wa Salome, Michael Isamuhyo alisema shuhuda aliyetumia simu ya mwanawe aliwaeleza kuwa, Salome kabla ya kufa, aliwataka wasihangaike.

Isamuhyo aliyezungumza na gazeti hili, alisema shuhuda huyo aliwaeleza kuwa Salome kabla ya kufa alitokea dirishani upande wa kulia na kupiga kelele ya kuomba msaada.

Shuhuda huyo kwa mujibu wa Isamuhyo, alisema walikwenda kumsaidia lakini walishindwa kwa kuwa alinasa sehemu ya miguu ndani ya basi hilo.

“Shuhuda alituambia kuwa, wakati wanamvuta, walibaini kuwa hawataweza kumuokoa kwa kuwa sehemu ya miguu ilinasa na alipoona hawezi kuokolewa, alirusha simu nje kwa shuhuda huyo.

“Baada ya kutoa simu hiyo, alimtaka atueleze sisi ndugu zake kuwa ameshindikana kuokolewa ili tusihangaike,” alieleza kwa uchungu Isamuhyo.

Baba wa Salome, Benjamin Magige akizungumzia msiba huo alisema; “Nimempoteza mtoto wangu wa pekee wa kike, nimebaki na mdogo wake wa kiume tu, walikuwa wawili pekee, nina uchungu sana.

“(Salome) alikuwa amalize chuo keshokutwa tu, ni maumivu makubwa kwa familia, mama yake kaja lakini hawezi kuzungumza, huu si wakati wa Serikali kufumbia macho ajali hizi, tuumie wote na tuhakikishe zinakoma,” alisema Magige huku akilia.

Maiti hao walizikwa katika makaburi yaliyochimbwa kwa kuambatana katika eneo la Air Msae walipozikwa abiria 25 waliokufa katika ajali ya basi ya Air Msae mwaka 1999, umbali wa kilometa takribani 10 kutoka ilipotokea ajali hiyo.

Alhamisi, 27 Oktoba 2011

ZITTO KABWE KALAZWA HOSPITALI MUHIMBILI.
























Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akiwa amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa kabla ya kuhamishiwa katika Hospitali ya Muhimbili. Kushoto ni rafiki wa yanke , Alex Kitumo. Picha na Venance Nestory

WALIOKUFA AJALI YA BASI JUZI KUZIKWA KABURI LA PAMOJA LEO

MIILI ya watu 12 walioteketea kwa moto katika ajali ya basi la Deluxe Coach iliyotokea Misugusugu mkoani Pwani juzi, watazikwa leo na Serikali kwa heshima zote katika kaburi moja katika eneo la Air Msae mjini Kibaha.
PICHA MBAYA
Maiti iliyoungua ikiondolewa.
Eneo hilo ndipo walipozikwa watu waliopata ajali ya basi la Air Msae lililokuwa likitokea Arusha kuja Dar es Salaam miaka ya 1990.


Uamuzi huo umefikiwa jana katika kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Pwani, iliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Mwantumu Mahiza kutokana na miili hiyo kuharibika vibaya na kushindwa kutambulika.
Gari iliyoteketea kwa moto.
Akizungumzia mazishi hayo jana, Mahiza alisema kabla ya maziko, miili ya watu hao itachukuliwa sampuli kwa ajili ya vipimo vya vinasaba (DNA) ili vifanikishe utambuzi wao.


Taarifa kutoka Hosptali Teule ya Tumbi, zilieleza kuwa hata wananchi waliokwenda kujaribu kutambua ndugu zao, walishindwa kufanya hivyo kutokana na kuharibika kwa miili hiyo ambayo baadhi imekuwa majivu.


Kutokana na hali hiyo, Mahiza aliwataka wananchi kutoa ushirikiano katika kufanikisha kuwatambua ndugu zao, kwa kupeleka vitu kama nguo ambazo ndugu zao walizitumia siku chache kabla ya ajali hiyo.


"Tunaomba wananchi walioondokewa na ndugu zao katika ajali hii watoe ushirikino kwa kuleta vitu kama soksi, shati, khanga au viatu alivyokuwa anatumia ndugu yao hivi karibuni ambavyo havijafuliwa ili visaidie kutambuliwa baada ya kupimwa kwa njia ya vinasaba,” alisema Mahiza.


Ofisa Habari wa Hosptali Teule ya Tumbi, Rose Mtei alisema kuwa majeruhi waliofikishwa katika hospitali hiyo ni 36 ambapo 35 waliruhusiwa na mmoja aliyelazwa anaendelea vizuri.

MWEKEZAJI ATOROKA NA BILIONI 1.8 ZA LAPF.

MFUKO wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF) umewachefua wabunge baada ya kubainika kupoteza Sh bilioni 1.8 kwa kukodisha hoteli ya Millenium Tower kwa kampuni ya kigeni ambayo hata anuani yake haijulikani.

Mwekezaji huyo kampuni ya GK Hotel and Resort, ambaye ametoweka bila kulipa fedha hizo, amebainika kuwa licha ya kukodishiwa hoteli, alipewa mkopo wa Sh milioni 500 za mtaji wa kuanzishia hoteli hiyo na LAPF.

Jengo la Millenium Tower linalomilikiwa na LAPF lililopo Kijitonyama.

Katika makubaliano yao, mwekezaji huyo aliahidi kurudisha mkopo na riba ya Sh milioni 721 ambazo nazo hakuzilipa hadi mkataba wake ulipovunjwa. Kana kwamba haitoshi, mwekezaji huyo hakulipa pango kwa kipindi chote ambacho aliendesha hoteli hiyo na hadi anaondoka, alikuwa anadaiwa Sh bilioni 1.1.

Fedha zote ambazo mwekezaji huyo anadaiwa na LAPF ni Sh bilioni 1.8 na sasa hivi mfuko huo unahaha kumpata huku akiwa ameshaondoka nchini na kurudi kwao Afrika Kusini.

Lakini LAPF jana ilikiri mbele ya Kamati ya Bunge, kuwa imeshindwa kupata anuani anazotumia Afrika Kusini.

Kashfa hiyo iliibuka wakati wa kikao cha Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na mbunge wa kwanza kuibua suala hilo, Esther Bulaya, alisema ana uhakika kuwa baada ya deni hilo, bodi ya wadhamini ya mfuko huo, imeamua kulifuta.

Mbunge huyo pia alikwenda mbali na kudai kuwa anatambua mwekezaji huyo ni kiini macho bali kashfa ni mpango maridadi ulioandaliwa miongoni mwa vigogo wa LAPF ambao wanatumia fedha za wanachama kwa manufaa binafsi.

“Hizi ni fedha za wananchi, hatuwezi kukaa kimya katika suala hili.”

Mkurugenzi Mkuu wa LAPF, Sanga Eliud, katika kujibu hoja ya Mbunge huyo, alikiri kuwa mwekezaji huyo ametoweka nchini na sasa hivi wanafanya juhudi za kumtafuta Afrika Kusini ili wamfungulie kesi nchini.

Alisema kwa vile Mfuko umeshindwa kumpata, wameomba msaada ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kupitia ubalozi wa Tanzania Afrika Kusini, ili watafute anuani ya mwekezaji huyo.

Jumatano, 26 Oktoba 2011

TEVE'Z APIGWA FAINI YA PAUNI 800,000. KWA KUKATAA KUCHEZA AKITOKEA BENCHI.

MANCHESTER CITY'S STATEMENT IN FULL

'Manchester City Football Club can confirm that a disciplinary hearing has been concluded in relation to a charge of misconduct by Carlos Tevez.
The charge relates to events during the Champions League match against Bayern Munich on September 27, 2011.
Following a detailed investigation and associated hearing, a disciplinary panel has upheld the charge of misconduct. Five separate breaches of contract formed the basis of the decision by the panel.
As a result Carlos Tevez has been fined four weeks' wages and has been suspended for a period of two weeks (deemed to have already been served). He has received a written warning as to his future conduct.
All alone: Carlos Tevez
Carlos Tevez has been informed in writing of the decision of the disciplinary panel, and the club has written to the Professional Footballers Association for ratification of the fine.
The five contractual obligations found by the disciplinary panel to have been breached are:
1. An obligation to participate in any matches in which the player is selected to play for the club when directed by a club official.
2. An obligation to undertake such other duties and to participate in such other activities as are consistent with the performance of the player's duties and as are reasonably required of him.
3. An obligation to comply with and act in accordance with all lawful instructions of any authorised official of the club.
4. An obligation to observe the statutes and regulations of FIFA and UEFA, the FA Rules, the League Rules, the Code of Practice and the Club rules, including but not limited to breach of Rule E3(1) of the FA Rules (obligation on the player at all times to act in the best interests of the game and not act in any manner which is improper or which brings the game into disrepute).
5. An obligation not to knowingly or recklessly do anything or omit to do anything which is likely to bring the club or the game of football into disrepute or cause the player or the club to be in breach of the rules (as defined in the contract) or cause damage to the club.
Carlos Tevez has the right to appeal this decision to the board of the club. Any appeal must be made within 14 days.'


Read more: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/

POLISI WAKAMATA MABOMU NA BUNDUKI NAIROBI.

Usalama umeimarishwa

Mtu mmoja amekamatwa na polisi na silaha mbali mbali kunaswa katika mtaa mmoja mjini Nairobi,Kenya.
Katika nyumba hiyo polisi walinasa maguruneti 13 na bunduki kadhaa pamoja na risasi.
Kwa mujibu wa mkuu wa polisi nchini Kenya Mathew Iteere, mtu aliyekamatwa anashukiwa kuwa mwanachama wa kundi la kigaidi.
"Sina shaka kuwa tutapata habari muhimu kutoka kwake na kuweza kuwatia mbaroni wanachama wengine wa makundi ya kigaidi," alisema.
Majirani wanasema mtu huyo alihamia katika nyumba hiyo ya kupanga kama mwezi mmoja uliopita na kwamba hawajawahi kumuona mtu mwingine yeyote hapo.
Polisi wanasema walivamia nyumba hiyo kutokana na taarifa za kijasusi walizopata.
Hatua hiyo inakuja baada ya mashambulio mawili kutokea katika maeneo tofauti mjini Nairobi.Katika mashambulio hayo mtu mmoja alifariki dunia na wengine zaidi ishirini kujeruhiwa

Jumanne, 25 Oktoba 2011

ENZI HIZO, ASKARI POLISI WAKIWA KATIKA PATROL 1918 HUKO KEYSTONE URUSI.

Polisi wakifanya doria 1918

MWILI WA GADDAFI UMEZIKWA KWA SIRI JANGWANI

Kanali Gaddafi 'azikwa' kisiri Libya

Mazishi ya kanali Muammar Gaddafi, mwanae Mutassim na waziri wa ulinzi yamefanyika katika sehemu ya siri leo alfajiri.
Msemaji mmoja wa baraza la kitaifa la mpito (NTC) ameiambia BBC kuwa miili ya watu hao watatu imezikwa baada ya utata kuhusu pale watakapo zikwa.
mwili wa kanali Gaddafi
Gaddafi amezikwa

Jamaa wa kabila la Kanali Gaddafi waliomba wapewe mwili wa kiongozi huyo ili wauzike mjini Sirte, alipozaliwa lakini inasemekana kuwa viongozi wa baraza la kitaifa la mpito walipinga ombi hilo.
Taarifa zingine zinamnukuu msemaji wa NTC Ibrahim Beitalmal akisema jamaa wachache wa familia ya Gaddafi walishiriki katika mazishi hayo na dua zilisomwa kulingana na utaratibu wa Kiislamu.
Baadhi ya watu mjini Misrata wanasema miili ya watu hao watatu iliondolewa usiku kutoka sehemu ilipohifadhiwa katika harakati za kupanga mazishi hayo.
Raia wa Libya wamekuwa wakitembelea eneo hilo la Misrata kujionea mwili wa kiongozi huyo ili kuthibitisha ukweli kuwa ameuawa.
Viongozi wa NTC walikuwa wanahofia kuwa huenda Kanali Gaddafi akizikwa katika sehemu iliyowazi, kaburi lake huenda likabadilishwa kuwa pahali patakatifu na wafuasi wake.
Pamoja na hilo mashirika ya kutetea haki za binadamu yamekuwa yakishinikiza uchunguzi ufanyike kubainisha jinsi alivyouawa kanali Gaddafi, kwani picha za awali zilionyesha kuwa alikamatwa akiwa hai.
Kiongozi wa NTC Mustafa Abdul Jalil, ametangaza kuwa uchunguzi utafanyika kuhusu hilo. Hata hivyo, kuna wale wanaohoji ikiwa kweli uchunguzi huo utakuwa wa wazi ikiwa mashirika ya kujitegemea hayata husishwa

PICHA YA LEO;HAKI YA KIKATIBA, RAIS WA ZANZIBAR AAPISHWA ILI AINGIE KWENYE BARAZA LA MAWAZIRI JMT.

 



 Jaji Mkuu wa Tanzania, Othuman Chandeiakimwapisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed Shein kuwa mjumbe wa Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ikulu Dar es Salaam huku Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo (katikati) wakishuhudia. (Picha na Yusuf Badi).

Jumatatu, 24 Oktoba 2011

AGEUKA MWIZI KWA KUPENDA SANA PICHA ZA NGONO



NewsImages/6018254.jpg
Amanda Owens
Mwanamke mmoja wa nchini Marekani amejikuta akigeuka kuwa mwizi na kuwa mashakani kutupwa jela kwa wizi kutokana na tabia yake ya kupenda sana kuangalia video za ngono. Alikuwa akiiba ili apate pesa za kununulia video za ngono.
"Kila mtu na ugonjwa wake" msemo huu unaweza kuwa sahihi kabisa kwa kumaanisha kuwa kila mtu huwa kuna kitu anachokipenda zaidi kuliko vingine.

Amanda Owens mwenye umri wa miaka 18 tu, ugonjwa wake ulikuwa ni kupenda sana kuangalia video za ngono.

Amanda alikuwa akipenda sana kuangalia video za ngono kiasi cha kwamba alikuwa akinunua DVD za video za ngono karibia kila siku.

Pindi alipokuwa hana pesa za kununulia DVD hizo Amanda alikuwa akiiba vitu toka kwa jirani yake na kwenda kuviuza ili apate pesa za kununua DVD hizo.

Amanda mkazi wa St Paul, Minnesota aliajiriwa na jirani yake Darin Pake, 44, kama mlezi wa watoto wake. Lakini mbali ya ulezi, Amanda alianza kumuibia pesa na vitu mbalimbali jirani yake huyo ili aweze kupata pesa za kununua DVD za ngono.

Siku za mwizi zilitimia pale jirani yake huyo alipoamua kuweka kamera za ulinzi ili agundue ni nani aliyekuwa akiiba pesa na mali zake.

Siku mbili tu baada ya kamera hizo za ulinzi kuwekwa, Amanda alinaswa akiiba kamera, brifkesi na kisanduku cha pesa.

Amanda alitiwa mbaroni baada ya jirani yake huyo kuripoti polisi.

Amanda aliwaambia polisi kuwa ndani ya wiki moja alizamia kwenye nyumba ya jirani yake mara tatu na kuiba vitu mbalimbali.

Amanda alitoboa siri polisi kuwa alilazimika kuiba ili aweze kupata pesa za kulipa deni la DVD 30 za ngono ambazo alizinunua hivi karibuni kwa mkopo.

Amanda amefunguliwa mashtaka ya wizi na huenda akatupwa jela miaka 10 pamoja na kutozwa faini ya dola 20,000 iwapo atapatikana na hatia

RUSHWA YA NGONO YATUMIKA ILI KUPATA UONGOZI

 
Utafutaji wa vyeo kama ubunge na vingine vya maofisini miongoni mwa wanawake wasiojiamini, ni sababu kubwa ya kuendelea kuwepo kwa rushwa ya ngono nchini. 
Mh. Hilda Ngoye.

 Aidha, imeelezwa kuwa matumizi mabaya ya madaraka yanayofanywa na baadhi ya wanaume ni kichocheo kingine cha rushwa hiyo, inayochangia nchi kuwa na viongozi wasio na uwezo, maadili mema, kwa asilimia kubwa.

Akizungumza wakati wa mkutano wa Kamati ya Bunge ya masuala ya Ukimwi iliyokutana Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, kujielimisha kuhusu unyanyasaji wa jinsia nchini, Mbunge wa Viti Maalum, Hilda Ngoye (CCM) alisema rushwa hiyo ipo na inarindima hata kwa wabunge.

Huku akiungwa mkono na Waziri Kivuli wa Afya na Ustawi wa Jamii, ambaye pia ni Mbunge wa Biharamulo Magharibi (CHADEMA), Dk.Gervas Mbassa, Ngoye alisema anachokizungumza kinafanyika si tu katika kuutafuta ubunge, bali hata katika kutafuta vyeo maofisini.

Wakati akisema hayo, Mbunge wa Viti Maalu, Margret Mkanga (CCM) alishtuka kwa mshangao ulioashiria kuisikia habari hiyo kwa mara ya kwaza na ndipo Ngoye alipomwambia, “Usishangae! It is a practical example, akimaanisha kuwa alichokizungumza ni mfano hai uliopo.

Kwa upande wake, Mbassa aliliambia gazeti hili kuwa hali hiyo ipo kweli na kwamba inatokana na kukosa utu miongoni mwa wanaoomba na wanaotoa rushwa ya ngono.

Alisema, wengi wanaojihusisha na rushwa hiyo na kushindwa kupata wanachokitaka huishia kuaibika au kupata maambukizi ya VVU huku walioigawa na kuupata uongozi wakiiharibu nchi kwa njia tofauti kutokana na kukosa maadili ya uongozi pamoja na uwezo wa kazi, “Alichokisema Ngoye ni sahihi kabisa, rushwa ya ngono ipo hata kwa wabunge. Lakini pia ipo katika nyanja zingine ambazo si za siasa. Watu wanataka uongozi wakati wanajua hawana uwezo na matokeo yake wanaamua kutumia miili yao. “Ufike wakati Watanzania tuikatae na kuthamini utu vinginevyo nchi itajaa viongozi watakaotusababishia matokeo mabaya,” Ndassa alisema.

Wakati huo huo, baadhi ya wabunge wanaounda kamati hiyo wamewataka wanafunzi wanaoombwa rushwa ya ngono kutoa taarifa kwa maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili wahusika wakamatwe na kushitakiwa, kwa sababu kitendo hicho, licha ya kuwa kosa la jinai, kinatumiwa na wengi kusambaza VVU.

Mbunge wa Viti Maalum, Rosweeta Kasikila (CCM) na Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo (CCM), walisema hayo kwa nyakati tofauti wakati wakitoa michango yao, kuhusu unyanyasaji wa kijinsia, unaohusisha ngono nchini.

Kasikila ambaye ni Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, alisema kuwa wanafunzi ni waathirika wakubwa wa rushwa ya ngono na kwamba wanahitaji kupewa elimu zaidi juu ya athari za rushwa hiyo ya ngono kwa watu mbalimbali wanaowarubuni ili waikatae na kuwaripoti wanaowashawishi kuishiriki, “Wapo wasichana na hata wavulana jasiri wanaowaeleza maofisa wa Takukuru kuhusu kuombwa rushwa ya ngono na hivyo kuandaa mitego inayowezesha kunaswa kwa wengi wao na kushitakiwa.

Hiyo ni njia mojawapo inayoweza kusaidia kupunguza kuenea kwa maambukizi ya VVU ambayo wengi wao huyapata wanaposhiriki kujamiiana huko”, Kasikila alisema.

Naye Shelukindo alisema kuwa wanafunzi wanastahili kujengewa ujasiri wa kuwaeleza wakubwa wao na taasisi zinazoshughulikia masuala ya haki zao ili kukomesha vitendo vya unyanyasaji vinavyofanywa dhidi yao, kama vile kuhisishwa katika masuala ya kujamiiana kwa kurubuniwa kupata wanachokihitaji.

Alisema, rushwa ya ngono haistahili kuwepo mahali popote pale kwa kuwa ni njia mojawapo inayochochea maambukizi kutokana na ukweli kuwa mara nyingi wahusika wanaoishiriki hawapati muda au kukumbuka kutumia kinga kama kondomu.


source: http://www.wavuti.com/

SERIKALI IWE MAKINI, ALBINO WAMEANZA KUUAWA TENA.

MLEMAVU wa ngozi aliyekatwa mkono wake wa kulia na watu wasiojulikana, Kulwa Lusana (16), amesimulia alivyojikuta akiwafukuza wavamizi hao, huku akilia na kuwaomba wamrudishie mkono wake.

Kulwa ametoa maelezo hyao Polisi jana na kuongeza kuwa juhudi hizo za kudai kurudishiwa mkono wake, hazikuzaa matunda, kwani wakataji hao walizidi kutokomea gizani na kumuacha akitapatapa.

Baada ya kupoteza matumaini ya kuupata mkono wake, Kulwa alisimulia kwamba akiwa anagugumia kwa maumivu makali, alikimbilia kwenye nyumba ya baba yake ambapo aligongana naye mlangoni na wote kuanguka chini.

Mlemavu huo alifanyiwa unyama huo juzi saa 7 usiku katika Kijiji cha Mbizi, Kata ya Segese wilayani Kahama katika Mkoa wa Shinyanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Diwani Athumani alisema watuhumiwa hao walivunja mlango na kuingia ndani kwa albino huyo na kuanza kumshambulia na kumjeruhi sikio na baadaye wakakata mkono wake wa kulia na kuondoka nao.

Kwa mujibu wa Kamanda Athumani, albino huyo alipiga kelele ya kuomba msaada kwa baba yake, Lusana Nkola ambaye hata hivyo wakati akitoka katika harakati za kumuokoa mtoto wake huyo, alipigwa jiwe kichwani akaanguka chini.

Alisema baada ya kufanyiwa unyama huo, watu hao waliufunga mkono huo kwenye mfuko na kuanza kukimbia nao na kutokomea pasipo julikana na kumuacha albino huyo akigugumia kwa maumivu makali.

Kutokana na tukio hilo, Polisi inamshikilia Petro Nkola mkazi wa kijiji cha Mtukula Runzewe wilayani Bukombe ambaye ni baba mdogo wa mlemavu wa ngozi, Kulwa Lusana (16).

Hata hivyo, Kamanda Athumani hakutaka kueleza kwa undani sababu za kumshikilia baba huyo zaidi ya kufafanua kuwa ni kwa mahojiano zaidi na uwezekano wa kuwapata watuhumiwa wengine waliotoroka na mkono wa mlemavu huyo.

Kulwa kwa sasa yupo katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama akiuguza jeraha lake na hali yake inaendelea vizuri.

Kamanda Athumani aliwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa watu wote watakaowadhani kuwa ni washiriki wa tukio hilo la kinyama alilofanyiwa mtoto huyo.

Tukio hilo limetokea ikiwa ni siku chache tu baada ya mlemavu mwingine wa ngozi, Adam Robert (14) kujeruhiwa kwa kukatwa na sime mkono wa kushoto na kunyofolewa vidole vya mkono wa kulia huko katika Kijiji cha Nyaruguguna wilayani Geita, mkoani Mwanza.

Katika tukio hilo la Geita, baba mzazi na mama wa kambo wa mtoto huyo, wanashikiliwa kwa tuhuma hizo.

SIMU YA MKONONI ILIMPONZA GADDAFFI NA KUFANYA NATO WAJUE KAJIFICHA WAPI?

Katika muda wote wa vita nchini Libya, Gaddafi alijitahidi kutoacha alama yoyote ambayo ingepelekea ajulikane sehemu aliyokuwa amejificha.

Kosa kubwa sana ambalo lilipelekea kifo chake alilifanya siku moja kabla ya kukamatwa kwake na baadae kuuliwa.

Gaddafi baada ya kuzidiwa na mashambulizi ya majeshi ya baraza la mpito na yale ya NATO, Gaddafi alitumia simu ya satelite kuwapigia wafuasi wake kusini mwa Libya akiwaomba wamtumie wanajeshi 12,000 ili kumsaidia kupigana vita na ndipo NATO ilipoidaka simu hiyo na kugundua sehemu ambayo Gaddafi alikuwa amejificha.

Baada ya kugundua amegundulika sehemu aliyokuwa amejificha, Gaddafi akiwa na msafara wa magari 80 alijaribu kutoroka mji wa Sirte lakini alikumbana na mashambulizi ya angani ya NATO ambayo yalitumia ndege za kivita za Ufaransa za Mirage 2000D pamoja na ndege za kivita za Marekani ambazo hazibebi mtu zinazoitwa, Predator.

Wakati huo huo, majeshi ya NTC yalitaarifiwa sehemu alipo Gaddafi na hivyo kupelekea Gaddafi awe kwenye mashambulizi makali ya angani na ardhini.

Gaddafi alilazimika kurudi kwenye mji wa Sirte ambako baadae alikutwa akiwa amejificha chini ya mfereji wa maji taka akiwa anavuja damu usoni.

Kijana mwenye umri wa miaka 21, Mohammed al-Bibi ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kumuona Gaddafi akiwa amejificha kwenye mfereji wa maji taka. Mohamed alimtaarifu kamanda wa kikosi chake ambaye aliwaongoza wenzake kumtia mikononi Gaddafi. Tangu wakati huo, Mohamed amekuwa akionekana kama shujaa wa Libya.

Gaddafi alijisalimisha mwenyewe kwa waasi huku akiwaomba wasimuue huku akiwaambia "Haya mnayonifanyia ni haramu, mnatenda dhambi".

Hali hiyo ilipelekea baadhi ya wanajeshi wa NTC wamtandike na viatu usoni huku mwingine akiiba pete yake ya ndoa na mkewe iliyokuwa na maandishi "Safia 1970".

Baada ya purukushani ya kumtembeza mtaani, Gaddafi aliuliwa na mwili wake ulionekana baadae ukiwa na majeraha ya risasi kichwani na tumboni.

Baada ya habari za kukamatwa na kuuliwa kwa Gaddafi kusambaa duniani, mtoto wa kike wa Gaddafi, Aisha Gaddafi mwenye umri wa miaka 34 alijaribu kumpigia baba yake simu mara kadhaa lakini simu hiyo ilipokelewa na wanajeshi wa NTC.

Ripoti za televisheni nchini Jordan na Dubai zilisema kuwa Aisha aliwavurumishia matusi waasi kwenye simu akiwaita "Panya" jina ambalo baba yake alipenda kuwaita waasi wakati wote wa vita vya kuipindua serikali yake.

Wakati huohuo, familia ya Gaddafi imetaka ikabidhiwe mwili wake ili iweze kumuandalia mazishi ya heshima.

Wakati huohuo pia, majeshi ya NATO yametangaza kuwa yatasitisha harakati zao za kivita nchini Libya ifikapo oktoba 31


Marehemu Kanali Gaddaffi

MANCHESTER CITY WAIAIBISHA MANCHESTER UNITED KWA KUIFUNGA 6-1

Manchester United: De Gea, Smalling, Ferdinand, Evans, Evra, Nani (Hernandez 65), Fletcher, Anderson (Jones 66), Young, Rooney, Welbeck.
Substitutes: Lindegaard, Berbatov, Park, Fabio Da Silva, Valencia.
Booked: Evra, Anderson, Smalling, Welbeck
Sent off: EvansGoals:
 Fletcher 81

Seeing red: United defender Jonny Evans (right) is sent off by Mark Clattenburg after fouling Balotelli
John Evans akitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea faulo Balloteli.



Manchester City: Hart, Richards, Kompany, Lescott, Clichy, Toure Yaya, Barry, Milner (Kolarov 89), Silva, Balotelli (Dzeko 70), Aguero.
Substitutes: Pantilimon, Zabaleta, Nasri, Toure, De Jong.
Goals: Balotelli 22, 60, Aguero 68, Dzeko 90, 90+3, Silva 90+1
Booked: Kompany, Balotelli, Richards
Referee: Mark Clattenburg (Tyne & Wear)
Attendance: 75,487

 Read all about it: Balotelli (left) celebrates by revealing a t-shirt that read 'why always me?'
Mario akisheherekea kufunga bao.

Ijumaa, 21 Oktoba 2011

MAISHA YA GADDAFFI, ATIMIZA AHADI YA KUFIA LIBYA, AUWAWA BAADA YA KUKAMATWA.

Taarifa za kuuawa kwake zilitolewa huku zikiambatanishwa na picha zinazoonyesha sura inayoonekana kuwa ni ya kiongozi huyo, katika muonekano wa nywele zake laini na ndefu wastani na uso uliotapakaa damu na majeraha.

Kanali Gaddafi anakuwa kiongozi wa kwanza kuuawa tangu kuanza vuguvugu la mageuzi katika mataifa ya kiarabu mwanzoni mwa mwaka huu, yaliyowaondoa madarakani Rais Ben Ali wa Tunisia na Hosni Mubarak wa Misri.

Kifo hicho kimetangazwa ikiwa ni miezi tisa tangu kuanza kwa upinzani mkali dhidi ya Serikali yake Februari mwaka huu, ambapo aliapa kwamba asingeondoka nchini Libya na kwamba yeye na wafuasi wake wangepambana hadi tone la mwisho la damu.

Kanali Gaddafi ambaye wakati wa utawala wake aliwahi kujipa wadhifa wa “mfalme wa wafalme wa Afrika” alikuwa akisifika kwa ukali wa sauti yake na maneno makali ya kuhamasisha na kueleza misimamo yake katika hotuba zake.

Mapambano hayo yameishia katika mji wa nyumbani kwake, Sirte ambao umekuwa na upinzani mkali kwa vikosi vya wapiganaji wa NTC ambavyo vililazimika kupambana kwa miezi kadhaa hadi waasi walipofanikiwa kuuteka jana.

Kanali Bani alisema mtoto wa Kanali Gaddafi, Mutassim ambaye walikuwa pamoja katika mji wa Sirte aliuawa na wapiganaji hao wa NTC.

Msemaji huyo aliwaambia waandishi wa habari kuwa kiongozi huyo alifariki dunia baada ya kujeruhiwa vibaya katika miguu yake yote na kichwani.

“Aliuawa katika mapambano na wapiganaji wetu. Kuna picha zinazoonyesha hayo,”alisema.

Alijificha kwenye karavati

Kwa mujibu wa taarifa za vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa, Kanali Gaddafi alidhibitiwa baada ya kukutwa  amejificha katika karavati la barabarani, yeye pamoja na baadhi ya walinzi wake.

Kwa upande wake, kamanda wa wapiganaji wa baraza hilo, Abdul Hakim Belhaj pia alithibitisha kuwa Kanali Gaddafi alifariki dunia kutokana na majeraha aliyoyapata baada ya kukamatwa.

Makamu Mwenyekiti wa NTC, Abdul Hafiz Ghoga alithibitisha mbele ya waandishi wa habari kuwa Gaddafi aliuawa katika mji wa Sirte.

“Tunatangaza kwa dunia kuwa Muammar Gaddafi aliuawa katika mikono ya wanamapinduzi,” alisema Ghoga.

Katika mtiririko wa matukio yaliyokuwa yakirushwa katika vituo mbalimbali vya televisheni, kituo cha televisheni cha al-Jazeera kilionyesha picha za mwili wa Kanali Gaddafi ukiburuzwa katika eneo alilouawa.

Filamu za video zilizochukuliwa kwa simu za mkono zilionyesha kile kilichoonekana kuwa maiti ya Gaddafi iliyolowa damu. Mwili wake baadaye uliburuzwa na wapiganaji na kupakiwa nyuma ya gari aina ya pick-up.


 Nato na Marekani zilieleza kuwa haziwezi kuthibitisha taarifa za kuuwawa kwa kiongozi huyo ambaye hajaonekana tangu NTC ilipoikamata Tripoli.

Watu washangilia mitaani

Wakati huohuo, katika mji wa  Benghazi na miji mingine nchini humo, watu walionekana kukusanyika mitaani na kushangilia taarifa hizo za kuuawa kwa Gaddafi.

Viongozi mbalimbali duniani pia wamezungumzia kuhusu taarifa hizo za kuuawa kwa Kanali Gaddafi ambaye amewahi kuwa mpinzani mkubwa wa mataifa ya Ulaya na Marekani kutokana na misimamo yake dhidi ya mataifa hayo.

Miongoni mwa viongozi hao ni Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameroon ambaye alisema ni siku maalum ya kukumbuka maovu yote yaliyofanywa na Gaddafi.

Alisema watu wa Libya wako katika nafasi nzuri ya kujenga nchi imara na yenye demokrasia.

“Ninafurahi kazi ambayo Uingereza imesaidia katika kuuondoa utawala wa Gaddafi,”alisema.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Alain Juppe amepongeza kufikiwa mwisho kwa utawala wa miaka 42 ya Gaddafi.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon pia alisema kwamba kifo cha Kanali Gaddafi kinatoa mwanya wa “historia mpya kwa Libya”.

“Watu wanatakiwa watambue kuwa huu ni mwisho wa mwanzo. Sasa ni wakati wa Walibya wote kushikamana na kuwa kitu kimoja. Ni wakati wa kuponya majeraha na kujenga upya taifa. Si wakati wa visasi,” alisema Ki-Moon.

Balozi wa Libya nchini Uingereza, Mahmud Nacua alisema kuwa kuawa kwa Gaddafi kunamaanisha Libya inaelekea kwenye mustakhabali bora wa baadaye.

Wasifu wa Kanali Muammar Gaddafi

Alikuwa mtoto wa wafugaji wa Kibedui, mwenye maisha ya utata, lakini ambaye alitukuzwa sana, huku mataifa ya Magharibi yakimuona mtu wa hatari wakati wote.

Muammar Muhammad Gaddafi aliitawala Libya kwa zaidi ya miaka 40. Hadi mwanzoni mwa Machi 2011, alikuwa akiamini ndani ya moyo wake kwamba watu wake walikuwa wakimpenda na kwamba walikuwa tayari kumlinda hadi kufa kwa ajili yake.

Lakini wakati huo, tayari Gaddafi alikuwa ameshatumia njia za kikatili kuyazima maandamano dhidi yake, maandamano ambayo baadaye yaligeuka vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Kwa mujibu wa taarifa, watu zaidi ya 30,000 waliuawa kwenye vita hivyo. Mara nyingi sana, Gaddafi alitoa matamko makali wakati wa vita hivyo, ila linalojuilikana zaidi ni lile la kuwaita wapinzani wake kuwa ni panya.

Kwa kila hali, yaliyotokea ni mambo ambayo Gaddafi hakuyatarajia asilani. Mtoto huyu wa wafugaji wa Kibedui aliyezaliwa mwaka 1942, alikuja kuibuka kama mkombozi wa Walibya, alipompindua Mfalme Idriss hapo mwaka 1969.

Kuanzia hapo akaanza kujenga kile alichokiona mwenyewe kuwa ni mfumo wa kidemokrasia wa moja kwa moja. Alianzisha kamati za umma zilizoamua juu ya mustakabali wa umma na wa Serikali. Aliuita mfumo wake wa kisiasa na kiuchumi kuwa ni wa kisoshalisti, alioufafanua kwenye kijitabu chake cha Kijani.

Historia yake kiufupi

Alizaliwa mwaka 1942 katika eneo la Jangwa, kwenye mji wa Sirte, katika familia ya baba Mohamed Abdulsalama Abuminiar na mama Aisha Ben Niran. Alijiunga na Jeshi la Libya  mwaka 1965.
Alifanya mapinduzi ya Serikali yasiyo ya umwagaji damu na kumuondoa mfalme Idris katika utawala wake mwaka 1969 na kuwa mtawala wa Libya akiwa na umri wa miaka 27.

Alikuwa maarufu kwa nguo anazopenda kuvaa na walinzi wa kike wenye kubeba silaha, kiongozi huyo wa Libya pia anadhaniwa kuwa na mbinu nzuri za kisiasa kwa kuweza kuirejesha Libya kutokana na kutengwa kidiplomasia duniani.
Baada ya miongo miwili ya kutengwa katika jamii ya kimataifa, mwaka 2003, Tripoli ilikiri kuwa walifanya shambulio la Lockerbie kwa kuiangamiza kwa mabomu ndege ya Pam Am. Umoja wa Mataifa (UN) ulikubali kuondoa vikwazo dhidi ya Libya.

Baada ya miezi kadhaa, Serikali ya Kanali Gaddafi ilisitisha mipango yake ya kuunda silaha za maangamizi na hii ikarejesha ushirikiano na nchi za Magharibi.

Gaddafi ni mtu wa kipekee katika kauli zake, mienendo yake, tabia zake na mikakati yake, kwa mujibu wa Saas Djebbar, mtaalam wa siasa za Libya.
Alipokuwa kijana alivutiwa na kiongozi mzalendo wa Misri, Gamal Abdel Nasser, alipokuwa akishiriki katika maandamano dhidi ya Israel wakati wa mtafaruku wa Suez mwaka 1956.

Alipanga njama ya kupindua utawala wa kifalme alipokuwa mwanafunzi wa kijeshi alipokuwa mafunzoni Uingereza kabla ya kurejea nyumbani Libya. Alipanga mapinduzi ya Septemba 1, 1969 akiwa katika mji wa Benghazi.

Alianza kujenga itikadi zake za kisiasa mwaka 1970 na kuziandika katika kitabu chake cha kijani kibichi.
Alikitumia kitabu chake kuanzisha mfumo wa kisiasa uliojumuisha kanuni za Kiislamu na mfumo ulio tofauti na siasa za ujamaa au ubepari.
Mwaka1977 aliasisi mfumo ujulikanao kama 'Jamahiriya' au 'Taifa la Umma' ambapo raia ndio wanaoendesha uongozi wa nchi yao kupitia 'kamati za umma'.

Mfumo huo wa Gaddafi umevuka mipaka na hauhusishi mambo ya siasa tu, bali pia mambo mengine.
Akiwa safarini ng'ambo, alikuwa akitumia makazi maalum kwenye kambi iliyojengwa na hema yake ya kifahari ya Kibeduwi akiwa amefuatana na walinzi wanawake ambao, inasemekana, huwa hawapotezi umakini kazini kama walinzi wanaume.Hema hiyo pia ilitumiwa kuwalaki wageni wa Libya na Kanali Gaddafi huendesha mikutano na mahojiano yake humo humo akipepea usinga au tawi la mitende.

Rais wa zamani wa Marekani Ronald Reagan alimwita Gaddafi 'mad dog' yaani 'mbwa kichaa' na Marekani ililipiza kisasi dhidi ya Libya kwa madai ya kuhusika na mashambulio ya anga barani Ulaya kwa kuvamia miji ya Tripoli na Benghazi mwaka 1986.Aliposhindwa katika jitihada zake za kuzipatanisha nchi za Uarabuni katika miaka ya 90, Kanali Gaddafi alielekeza nguvu zake barani Afrika na kupendekeza 'Muungano wa Nchi' za bara la Afrika.

Alianza kuvaa mavazi yake binafsi, sare za michezo zilizo na ngao za Bara la Afrika au picha za viongozi kutoka bara hilo.Aliwahi kuvunja na kufuta Wizara za nchi hiyo pamoja na bajeti zao, isipokuwa Wizara chache ikiwemo ya Ulinzi, Fedha na Mambo ya Nje.Licha ya uchumi wa Libya kutoa fursa kwa wawekezaji wa nje, mabadiliko bado yanakwenda taratibu.

Vuguvugu la mageuzi dhidi yake lilipoanza mwanzoni mwa mwaka huu, aliapa kuwafuata wanaompinga nyumba hadi nyumba, mlango kwa mlango, hatua iliyoibua hasira na kuchochea harakati za kijeshi dhidi yake.

Baada ya baadhi ya askari kutangaza kujitoa katika jeshi lake na kuanzisha uasi, aliapa kwamba atapambana hadi tone la mwisho la damu litakapomwagika. Alisisitiza kwamba kamwe hatakimbia kutoka katika ardhi ya Libya, atafia katika ardhi ya mababu zake.

Taarifa zilieleza jana kwamba aliuawa baada ya kukutwa akiwa amejificha katika daraja dogo kwa ajili ya kupitisha maji barabarani (karavati).
Mara baada ya kuuawa, wapiganaji wa Baraza la Mpito waliokuwa katika mapambano dhidi yake walibaini kwamba alikuwa na bastola iliyotengenezwa kwa dhahabu tupu.
Credits; Gazeti la Mwananchi

YANGA YAPANDA NGAZI MOJA KUELEKEA KILELENI.

 Image






YANGA ya Dar es Salaam imezidi kunogesha mbio za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya jana kuifunga Toto African mabao 4-2.

Kutokana na matokeo ya mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga sasa imefikisha pointi 18 na kupanda kutoka nafasi ya nne hadi ya tatu kwenye msimamo.

Azam FC iliyokuwa ikishika nafasi ya tatu imeshuka kwa ngazi moja, ambapo Azam pia ina pointi 18, lakini inazidiwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa. Yanga ipo mbele mchezo mmoja zaidi ya Azam.

JKT Oljoro inaendelea kushika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 19, huku Simba yenyewe ikiongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 24, ambapo zote zimecheza mechi kumi.

Katika mchezo wa jana, Yanga ambayo ina udugu wa kihistoria na Toto African ya Mwanza
ilienda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 3-0.

Mabao hayo yalifungwa na Haruna Niyonzima dakika ya nane, Kenneth Asamoah dakika ya 12 na Jerry Tegete dakika ya 21 yote yakifungwa kwa mashuti.

Toto iliyokuwa ikionekana kuzidiwa kipindi cha kwanza ilicharuka dakika za mwisho na kupata
bao dakika ya 82 mfungaji akiwa Mohammed Soud.

Wakati mashabiki wakiamini mchezo huo ungemalizika kwa matokeo hayo ya mabao 3-1, Asamoah aliongezea Yanga bao la nne dakika ya 85 kabla ya Soud naye kupachika la pili dakika
ya 89.

Yanga ingeweza kupata mabao mengi zaidi lakini umaliziaji haukuwa mzuri kwa kushindwa
kulenga lango kila walipokaribia golini.

Hali hiyo pia iliikumba Toto Africans ambayo kwa nyakati tofauti wachezaji wake Soud,
Phabian James na Bakari Kigodeko walishikwa na kigugumizi cha miguu walipomkaribia kipa
Yaw Berko

ICC YAISHUTUMU MALAWI KWA KUTOMKAMATA AL-BASHIR.

Rais Omar al-Bashir

Mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC imeitaka Malawi kueleza kwanini ilishindwa kumkamata Rais wa Sudan Omar al-Bashir katika ziara yake ya hivi karibuni.
ICC imetoa hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa Bw Bashir kwa mashtaka ya mauaji ya kimbari na uhalifu wa kivita wakati wa mgogoro huko Darfur.
Malawi ni moja ya nchi zilizotia saini makubaliano ya kuridhia mahakama ya ICC lakini imesema "si kazi yake" kumkamata Bashir.
Bw Bashir amekana mashtaka hayo, akisema yamechochewa na masuala ya kisiasa.
Umoja wa Afrika ulishawishi hati hiyo ya kukamatwa iahirishwe, ikiishutumu ICC kwa kuchunguza tu madai ya uhalifu wa kivita barani Afrika na kukamatwa kwa rais wa Sudan kutazuia utafutaji wa amani Drafur.
Bw Bashir alilakiwa na gwaride la heshima alipowasili kwenye mji mkuu, Lilongwe, katika mkutano wa masuala ya biashara mwishoni mwa juma.
Umoja wa Ulaya na makundi ya kutetea haki za binadamu yaliisihi Malawi kumkamata Bw Bashir.
Lakini waziri wa habari Patricia Kaliati aliiambia BBC kwamba wasingeweza kumkamata Bw Bashir kwani alikuwa akihudhuria mkutano wa wakuu wa nchi wa soko la pamoja la mashariki na kusini mwa Afrika (comesa).
Alisema, " Anakuja kikazi na kukamatwa kwa Rais Bashiri hakutuhusu."
Kenya na Chad, ambao wote nao wametia saini mkataba huo wa ICC, wamemruhusu Bw Bashir kutembelea nchi zao.
ICC imeiandikia Malawi kuiomba kufanya "uangalizi" wa ziara ya Bw Bashir kabla ya Novemba 11.
Rais wa Malawi Bingu wa Mutharika ni miongoni mwa viongozi wengi wa Afrika wanaoishutumu ICC kwa kuchunguza madai ya uhalifu wa kivita barani Afrika tu na si maeneo mengine.
Bw Bashir alikuwa rais wa kwanza kushtakiwa na ICC, iliyomshutumu kwa mauaji ya kimbari na uhalifu wa kivita Darfur

RAIS JAKAYA KIKWETE ATUNUKIWA UDAKTARI WA SHERIA NA UDSM.



CHUO KUKUU CHA DAR ES SALAAM JANA KILIMTUNUKIA SHAHADA YA UDAKTARI WA SHERIA RAIS KIKWETE KWENYE HAFLA ILIYOFANYIKA UKUMBI WA NKRUMAH UDSM, MWENYEWE ASHANGAA, PIA RAIS MUSEVENI WA UGANDA ALITUNUKIWA SHAHADA YA UDAKTARI WA FASIHI TOKA CHUO HICHO.

Alhamisi, 20 Oktoba 2011

INASEMEKANA GADDAFFI KAKAMATWA AU KAUWAWA!!!!!!!

Picha ya video ya simu ambayo imesambaa karibia Duniani kote na vyombo kadhaa vya habari vimetangaza habari hii, tusubiri kidogo tutajua ukweli kamili, hali ni mbaya Siirte, tuombe vita iishe.

BAADA YA UKAME WA MAGOLI, TORRES AIFUNGIA CHELSEA CHAMPIONS LEAGUE,GENK YACHAPWA 5-0.

Fernando Torres's prayers were answered as he scored his first Champions League goals for Chelsea in a thrashing of Genk.
The Spain striker, who was pictured before the game joining Brazilian team-mate David Luiz in apparent meditation, scored twice as Andre Villas-Boas’ team brushed aside their Belgian opponents to spark songs of praise at Stamford Bridge.
Contented manager Villas-Boas believes he now has Europe’s top strikeforce, declaring: ‘We are able to choose from the best up front. The choice fell with Torres and he responded pretty well.’

Blessed: Fernando Torres and David Luiz before Chelsea's win
Torres had not scored in 875 minutes in the competition since netting for Liverpool against Chelsea more than two years ago.
Raul Meireles, Branislav Ivanovic and Salomon Kalou scored Chelsea’s other goals as Villas-Boas’ side continued their unbeaten start and equalled their biggest home win in the competition.
The Chelsea manager admitted he is spoilt for choice with Torres, Didier Drogba, Nicolas Anelka, Daniel Sturridge and Romelu Lukaku to pick from.
‘I’m pretty pleased with the way the team played,’ said the Portuguese coach, who was able to select Torres for the first time since the striker’s sending-off against Swansea three weeks ago. 
‘It would have been a long period off (if Torres hadn’t played). It’s important players feel confident.
Villas-Boas, who has seen his side score 13 times in their last three matches, was happy to come through a match that he feels could have been a potential banana skin.
'To score two goals in the first 15 minutes, this put us in a very comfortable position," he said.
"It was a good display from everybody. I'm very happy with the performance, not only the way we played but the commitment of the team.
"This was a game that everyone expected us to win, and that's when surprises lie just round the corner. But we had the focus and put in a good performance.'
Another three points in Belgium next month would all but guarantee the club's qualification, but Villas-Boas is not getting carried away with talk of his team challenging for the Champions League trophy that Blues owner Roman Abramovich craves.
He said: 'With seven points, we go to Genk and the three over there would put us in a good position to qualify but this group could become very tight depending on what happens in Leverkusen with Valencia.
Doubling up: Torres (left) heads home his second goal at Stamford Bridge
Doubling up: Torres (left) heads home his second goal at Stamford Bridge
'The most important months for us will be the last three of the season, when you finally win or don't win trophies.
'For now, we're just aiming at our objectives. We want the best results as possible to get qualification through, and keep on track for going as far as we can in the competition.'
Genk boss Mario Been admitted Chelsea were a class apart from what his team could offer.
'They were on totally another level,' Been said.
'We gave them the goals too easily. We needed to keep a clean sheet for the first 20 minutes, but we were two down after 10 minutes.'
Meanwhile, goalkeeper Petr Cech hailed Chelsea's 'brilliant mentality'.
Cech told Sky Sports: 'We were very good, we put them under pressure, created chances and converted them clinically.

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU UINGEREZA AFA KATIKA UKUMBI WA DISCO BAADA YA VURUGU ZA KUTOKA NJE KUWAHI MABASI.

Killed: Northampton University student Nabila Nanfuka died in the nightclub

Killed: Northampton University student Nabila Nanfuka died in the nightclub
A university student was killed in a nightclub stampede as revellers were told their coaches home were about to leave without them.
Nabila Nanfuka, 22, is believed  to have suffered a heart attack after being crushed on a landing area halfway down a staircase as bodies piled on top of her.
Two others were critically injured in the tragedy, which happened at an ‘urban music’ night attended by students from all over the country.
Yesterday there were claims that the event at the Lava & Ignite club in Northampton was overcrowded and tickets had been oversold.
The stampede followed an announcement that students had ‘ten minutes to get on the coaches or they will go without you’ at around 3.30am yesterday.
A fire alarm was then also triggered, which caused the crowd surge to escalate further.
One 19-year-old who passed out in the crush said that when she regained consciousness, she saw the lifeless body of a woman trapped under other fallen clubbers.
The student, who travelled to the ‘Wickedestwickedest’ event from London, said: ‘People were pushing, pushing, pushing to get out. A lot of us just couldn’t breathe.
‘I ended up on my front, trying to find a gap to breathe through, but there were so many people on top of me.
‘Every time somebody was pulled out of the pile of bodies, more people fell forward on top of us. It was awful. I thought I was going to die.
‘I’m sure I passed out for a few minutes. When I came around, I saw a girl’s body below me, to my left.
‘Her eyes were closed and she had people lying on top of her. Everybody else was trying to move or screaming, but she was motionless.’
The event was attended by students from universities as far away as Canterbury, as well as others across Bedfordshire, Hertfordshire, Birmingham and the East Midlands.


Read more: http://www.dailymail.co.uk/

JK AONJA ADHA YA KUKATIKA KWA UMEME.


Aziza Masoud
RAIS Jakaya Kikwete juzi usiku alionja adha ya kukatika kwa umeme alipokuwa akiendesha hafla ya kuchangia ujenzi wa kituo cha wanafunzi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwenye ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.  Tukio hilo lilitokea majira ya saa 5:43 usiku takriban saa nne tangu hafla hiyo ianze.
Rais Kikwete alifika ukumbini hapo saa 2:33 muda mfupi akitanguliwa na viongozi wengine wa Serikali.  Baadhi ya viongozi hao ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk Shukuru Kawambwa, Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki.  Kukatika huko kwa umeme, kuliwafanya wageni waliokuwapo ukumbini kuanza kupiga kelele za: “Ngeleja... Dowans... Ngeleja... Dowans... Ngeleja... Dowans.”

Tukio hilo lilidumu kwa dakika mbili kabla uongozi wa Mlimani City kuwasha genereta. Katika hafla hiyo, Rais Kikwete alichangisha Sh720 milioni kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho kinachotarajiwa kujengwa katika Kampasi ya Mlimani katika kumbukizi ya Miaka 50 ya Uhuru.  Kituo hicho kitakuwa na maeneo ya kupumzika wanafunzi, hosteli, sehemu za michezo, maktaba, huduma za vyakula, benki, ofisi za serikali ya wanafunzi na kituo cha intaneti.

Akizungumza kabla ya uchangishaji huo, Rais  Kikwete alisema lengo la kuchangisha fedha hizo za kujenga kituo cha wanafunzi ni kuboresha mahitaji ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambayo kwa sasa  yamekuwa changamoto kubwa inayosababisha wanafunzi kupata elimu katika mazingira magumu.

 “Mara  nyingi ukipita katika maeneo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, unakuta wanafunzi wamezagaa katika maeneo mbalimbali na wengine chini ya miti. Hii yote inatokana na kukosa eneo maalumu la kujisomea na kupumzika mara wanapomaliza au kusubiri kuingia katika vipindi,” alisema Kikwete.

  Alisema kutokana na ongezeko la watu na shughuli za kimaendeleo, chuo hicho kwa sasa kinakadiriwa kuchukua wanafunzi 20,000 kwa mwaka, tofauti na miaka ya nyuma   kilipokuwa kinachukua wanafunzi 14,000.  Alisema kutokana na hali hiyo, wahitimu wanapaswa kuchangia maendeleo ya chuo hicho kwa kuwapatia wanafunzi nafasi za malazi ambazo kwa sasa hazitoshi na kuwalazimu wengine kulala nje ya eneo la chuo.

Credits; Gazeti la Mwananchi.

Jumatano, 19 Oktoba 2011

GARI LA GHARAMA LAZINDULIWA HUKO AUSTRIA, LINAGHARIMU PAUNDI 1.9 MILLIONI, LINA KILA KITU KAMA NYUMBA YA KIFAHARI.


LINAITWA ELEMMENTE, LINA VYOO VIWILI MASTER BEDROOM NA TV YA INCH 40.
Austrian company Marchi Mobile is behind the 40ft-long palace on wheels called the eleMMent palazzo, which comes complete with a roof terrace. The bizarre-looking vehicle has a huge master bedroom with 40-inch TV, an en suite bathroom, separate toilet, lounge and driver's cab complete with bunk-bed. But the most impressive touch is the machine's 'sky lounge' which opens at the touch of a button and features underfloor heating and a bar.

MKAO WA BAADHI YA ABIRIA NDANI YA DALADALA MMHM.....

BABA NA MAMA WAKAMATWA KWA KUMSHAMBULIA MTOTO WAO ALBINO GEITA.

Mbunge wa Viti Maalumu, Al-Shaymaa Kwegyir akitokwa machozi baada ya kumuona kijana Robert Tangawizi (14) ambaye ni mlemavu wa ngozi (albino) alivyojeruhiwa mkono wa kushoto na kisha kunyofolewa vidole vitatu vya mkono wa kushoto, wakati alipomtembelea hospitalini Geita mkoani Mwanza. (Picha na David Azaria)

.WATU watano wakiwemo baba mzazi na mama wa kambo wa kijana mlemavu wa ngozi, Adam Robert, wamekamatwa na Polisi wilayani Geita Mkoa wa Mwanza, kwa tuhuma za kumjeruhi
kwa kumkata mapanga na kumnyofoa vidole vitatu kijana huyo, mkazi wa Kijiji cha Nyaruguguna.

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Liberatus Barlow, amethibitisha kukamatwa kwa
watuhumiwa hao, lakini alikataa kuwataja majina.

Hata hivyo, taarifa zilizopatikana kutoka Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Geita, zimeeleza kuwa miongoni mwa wanaoshikiliwa ni pamoja na mganga maarufu wa jadi, Rumanyika Yesu (49).

Wengine kwa mujibu wa taarifa hizo ni pamoja na baba mzazi wa Adam, Robert Tangawizi (36),
mama wa kambo wa majeruhi huyo ambaye amekuwa akimlea kwa siku nyingi, Agnes Majala (29).

Pia baba mkubwa wa Adam, Andrew Tangawizi (52) na mkazi wa kijiji hicho, Machibya Alphonce (30). Taarifa hizo zimeeleza kuwa baba mzazi amekamatwa kutokana na maelezo ya mtoto na mazingira ya tukio hilo.

Adam anadaiwa kueleza kuwa siku ya tukio, mtuhumiwa ambaye ametoroka na anatafutwa na Polisi, alitaka kufanya kitendo hicho machungani, lakini mtoto huyo alimzidi ujanja.

Katika maelezo hayo, Adam alieleza kuwa mtuhumiwa huyo alimdanganyia kofia, lakini alikataa kabla ya kumtaka kuwapeleka ng’ombe kwenye nyasi nyingi ambapo kulikuwa na kichaka, lakini pia alikataa.

“Siku hiyo hiyo jioni mtuhumiwa huyo alifika nyumbani kwao na mtoto na kisha
akakaribishwa na baba mzazi na kuketi naye mahali walipokuwa wakiota moto (Kikome).

BUSHA LA KILO 45 LAMTESA JAMAA.


NewsImages/6008614.jpg
Wesley Warren Jr
Mwanaume mmoja wa nchini Marekani ana busha lenye uzito wa kilo 45, busha hilo linamtesa sana kiasi cha kushindwa kutembea na hata kwenda chooni.
Wesley Warren Jr anateseka sana kutokana na busha linalomnyima raha na kumfanya ashindwe kuendelea na maisha yake ya kawaida.

Wesley ameanzisha kampuni ya kuchangisha watu pesa ili aweze kupata dola milioni moja ambazo ameambiwa azipeleke hospitali kwaajili ya gharama za operesheni ya kuliondoa busha hilo.

Wesley anasumbuliwa na ugonjwa unaoitwa scrotal elephantiasis. Busha lake ni kubwa sana lenye uzito wa kilo 45 kiasi cha kumfanya ashindwe kutembea na kupata tabu kwenda haja.

"Ni vigumu sana kutembea, kutwa nashinda ndani", alisema Wesley.

Wesley mwenye umri wa miaka 47, anasema kuwa ingawa baadhi ya watu wanamcheka kutokana na hali yake, hajakata tamaa na aliamua kujitokeza kwenye vipindi vya televisheni na redio kuelezea hali yake ili kuomba msaada wa kuchangisha fedha za operesheni yake.

Hali aliyo nayo Wesley ni nadra sana kuiona kwenye nchi ambazo si za Tropiki zaidi ya Afrika na Asia, ambako ugonjwa huo husababishwa na maambukizi yanayosambazwa na mbu.

Wesley anasema kuwa hajawahi kusafiri kwenye nchi za tropiki na anaamini kuwa hali aliyo nayo inasababishwa na tukio lililotokea mwaka 2008 wakati alipozibana korodani zake katikati ya miguu yake wakati alipokuwa akijigeuza kitandani.

Wesley aliongeza kuwa siku iliyofuatia korodani zake zilivimba na kufikia ukubwa sawa na mpira wa soka

Jumanne, 18 Oktoba 2011

SABABU 6 MBOVU ZA KWA NINI UINGIE KATIKA NDOA.

Watu wengi tumewaona kwenye ndoa wakiishi katika hali tofauti za maisha, wako wenye fedha na wasionazo, wako wenye furaha na wasio na wasionao.

Yote hii huweza kuchangiwa na sababu nyingi ikiwemo wanandoa hawa kujikuta wanaingia katika ndoa wakisukumwa na sababu zilizo mbovu na zisizo na msingi
Ziko sababu njema na nzuri za ndoa zinazoongelewa sana na wengi maeneo mbalimbali. Mimi nimejaribu kuzitafuta zile sababu zisizo nzuri ambazo wengine pasipokuwa makini wamezishikilia na kusiruhusu sababu hizi ziwasindikize katika ndoa na hivyo kujikuta wenajuta na kulia katika muda mwingi wa maisha.

Hii pia ni sababu ya ukweli kwamba siku hizi idadi ya ndoa zinazovunjika ni kubwa sana kuliko zamani. Hali ya kiwango cha kudhamiria (commitment) kwa wanandoa ni kidogo sana na hivyo kushusha uthamani wa ndoa zenyewe.

Sababu hizi zitakuwezesha kuubadili mtazamo ulionao juu ya ndoa na kukupelekea kubadili namna  unavyo sema au kuwaza au kutenda kuhusiana na suala zima la ndoa.

SABABU MBOVU

  1. Kuingia katika ndoa kwa lengo la kusaidiwa au kuongeza  kiwango cha kiuchumi ulicho nacho. Hapa wengine wamewageuza wapenzi wao kuwa mitaji au rasilimali ya kuwaondoa wao pamoja na ndugu zao kutoka kwenye umasikini.  Kwa kuthibitisha hili wengine  wamepewa majina kama BUZI, ATM n.k. Katika penzi la namna hii hakuna mguso au muunganiko wa kuhisia baina ya wapenzi, bali kinachowaunganisha pekee ni kile kilicho mfukoni. Athari za penzi la aina hii lina fungua milango mingi kwa wanandoa  kutokuwa  waaminifu na hata kujihusisha na mapenzi  nje ya ndoa.
  2. Hofu ya umri kupita na kuzeeka. Wako wengi sana, hususani watu wa wajinsia ya kike ambao wamejikuta wakiwakubali wanaume wa aina yoyote ili mradi tu nao waolewe maana umri wao ulionekana kusonga sana na hofu ya kutoolewa kutanda. Mwanaume anayehusiana na mwanamke mwenye tabia hii huulizwa au kulazimishwa kila siku kwenda kujitambulisha kwa wazazi wa binti au kutangaza ndoa.  Ndoa nyingi za aina hii zimeishia kenye talaka na kutengana. Wako wengine ambao, kwasababu wanakiu sana ya kupata watoto na wameogopeshwa sana habari kwamba wana weza wasipate watoto kwa sababu ya umri wao, basi watacheka  na kaka yeyote yule ilimradi tu waolewe au wazae naye  Wengine wajinsi hii wamejuta sana baada ya kujikuta kuwa waliyezaa naye hakuwa BABA wa kweli bali kirukanjia tu na kwahiyo wameishia kulea mtoto au watoto wao wenyewe pasipo mzazi wa pili, jambo ambalo kwa kiasi kikubwa  linawaathiri watoto wengi.  Kwa wale wanaokimbilia kuolewa ili wakazae watoto, kukumbuka kuwa hata huko kwenye ndoa kuna waliokosa watoto.
  3. Kuingia kwenye ndoa sababu ya mimba au mtoto aliyepatikana kabla ndoa. Lazima kutofautisha kuwa sababu iliyowapelekea kuzaa mtoto siyo itakayowapelekea kuoana.  Acha sababu ya kuoana kwenu iwe penzi lenu la dhati na sio mimba au mtoto. Suala hili linahitaji pia wazazi wajue kwamba kitendo cha watoto  kupeana mimba au kupata mtoto hakitoshi kuwa sababu ya kuwalazimisha kuoana, maranyingi wazazi wamewalazimisha watoto wao kuingia katika ndoa sababu ya mimba au mtoto na kujikuta wanawaharibia maisha yao mazima.  
  4. Kulazimika kuingia kwenye ndoa au mahusiano ya kudumu kwa sababu ya upweke, (Loneliness). Mara nyingi mtu anapokuwa peke yake (single) huwaza kuwa ndoa ndiyo inayoweza kuwa utatuzi mkubwa wa matatizo yake.  Nakubaliana na ukweli wa maandiko kwamba “Sio vema mtu awe peke yake…” lakini ni vizuri tukijua tofauti iliyopo baina ya kuwa peke yako na upweke.  Hivi ni vitu tofauti: kuwa peke yako inamaanisha kukosa mawasiliano au ukaribu na watu wengine, unakuwa kama uliyetengwa, wakati upweke (loneliness) inahusisha nafsi,  akili na hisia kuwa pweke au kujihisi kutengwa na hii ni ngumu kuishuhulikia.  Ni heri kuwa peke yako (single) kuliko kuwa  kwenye ndoa na bado ukajisikia upweke (lonely).  Wako wengine waliodhani ndoa ni suluhisho la upweke waliokuwa nao na mara walipoolewa au kuoa, mawasiliano baina yao yakayumba na hivyo kukomaza  upweke kwa wote wawili.
  5. Kuolewa au kuoa kwa sababu ya shinikizo kutoka kwa wazazi, ndugu au marafiki. Shinikizo hizi zaweza kuwa za kihisia au hata kihalisia.  Kihisia ni pale ndugu au wazazi wanapokushawishi mara kwa mara kuoa sababu umri wako una pita na wako wazazi wengine husema wanataka wajukuu.  Hata kama huhisi  kulazimishwa lakini kwa kule kurudia rudia kwa kukumbushwa kila siku kunaathiri hisia zako na kuweza kukupelekea kuingia katika ndoa isiyopangiliwa.  Shinikizo ya kimwili au kihalisia ni pale wazazi wanopolazimisha watoto wao kuoa au kuolewa na watu fulani kwa sababu tu ni marafiki zao (family friends) au kwa sababu ya kulinda utajiri na matarajio yoyote binafsi.  Ndoa nyingi za aina hii zimekuwa kero na dimbwi la maumivu na machozi, baada ya muda kidogo mna jikuta mali mnazo, wazazi wenu wanapatana,  lakini nyie kama wapenzi ni maadui wakubwa.
  6. Kuamua kuoa au kuolewa ili kupata uhuru. Hii hutokea sana kwa wale waliozoea kubanwa sana na wazazi katika kila wafanyacho hususani katika maamuzi. Wengine huzikimbia familia zao maana hazieleweki, hazina mpangilio na hivyo kutamani kutoka ili wakaanzishe zakwao wenyewe. Kinadada na kinakaka wanachoka kuamuliwa na kuwekewa masharti ya kuvaa, kula, kufanya mambo, kutoka na kurudi kwa muda kwahiyo wanadhani ndoa ndio itawachomoa kifungoni hapo.


MATOKEO YA KUINGIA KATIKA NDOA KWA SABABU MBOVU

Lengo la kuingia kwenye ndoa, liwe zuri au liwe baya ndilo litakalotegemeza aina ya maisha yenu katika ndoa hiyo kuwa ya furaha au ya machungu. Baada tu ya kuoana na huyo mtu wako kwa sababu zisizo za msingi, siku, miezi au miaka siyo mingi utaanza kuchoka na kutamani kutoka nje ya hiyo ndoa kwa maana baina yenu hakuna muunganiko wa kindani ya ndoa ya jinsi hii.  Na mara nyingi hali hii hupelekea msongo wa mawazo, mfadhaiko na kukosa furaha ndani ya ndoa.  Na matokeo ya hali hii kumfanya mwanandoa mmoja au wote wawili kuanza kutafuta kutoshelezwa na kuliwazwa nje ya ndoa na hapa vinazaliwa vitu kama uzinzi, kutengana na talaka.

Kwanini ndoa nyingi hushindwa?


Kwa sababu ya kukosa maarifa.

Wanandoa wengi hawajui nini wafanye, nini waelewe ili kufanya ndoa yao zifanikiwe. Thamani ya ndoa na jinsi ndoa inavyochukuliwa siku hizi ni tofauti sana na nyakati za wazazi wetu, na hii imewafanya wengine kujikuta wako wenye ndoa kwa sababu mbovu na hivyo ndoa nyingi kuvunjika au kuyumba baada ya muda mfupi tu. Vitu kama kudhamiria, heshima na uaminifu sio vya maana tena siku hizi, sababu watu wanaogopa kuonekana wa zamani na washamba. Mtazamo wa ulimengu juu ya ndoa umeharibiwa na magazeti, luninga na vitabu mbali mbali.

Siku hizi kuishi bila ndoa ni kitu cha kawaida, kuwa na mpenzi nje ya ndoa sio kitu cha kutisha tena,  mapenzi nje ya ndoa sio ya kushangaza hata kidogo.  Kinyume chake ukionekana kuyashangaa haya, jamii itakushangaa wewe kwa jinsi ulivyo nyuma ya wakati.

Mambo yamebadilika sana. Zamani binti akikutwa bikira wakati anaolewa ilikuwa sifa kwake na familia nzima, siku hizi binti akikutwa bikira atachekwa, na watu kumshangaa wakihisi ana matatizo fulani. Hali kadhalika kwa kijana wa kiume aliyejitunza. Kwa bahati mbaya sana  tunaishi katika jamii ya ajabu isiyoamini katika kujitoa kwa kweli na kudhamiria katika ndoa. Jamii isiyoamini katika uaminifu, na ndiyo maana magomvi mengi hutokea pale simu ya mmoja inapoguswa.  Kuwindana na kuchunguzana kumekuwa kawaida, maadili sio jambo la kuzingatiwa tena.  Wanandoa wengi ni wale wenye majeraha ya moyoni na walio umizwa, kwa hiyo hutoka nje ya ndoa zao wakitafutatafuta mwingine aliyeumizwa kama wao ili  waliwazane.

Kwa haraka tuangalie sababu za msingi zinazoweza kukufanya uingie katika ndoa na usijute:-

-  Ndoa ni mpango wa Mungu kwa mwanamke na mwanaume kuwa pamoja
-  Ni nafasi ya wawili hawa kuonyeshana mapenzi  yao
-  Nafasi ya kutimiziana mahitaji ya mwili kupitia tendo la ndoa kwa muda sahihi, na mtu sahihi, kwa maadili.
-  Hamu na kiu ya kutengeneza familia yenu.
-  Kutimiza kiu ya kuwa pamoja kwa umoja (companionship)
-  Nia au kusudi la kushiriki vyote kwa pamoja . Kufanya kutenda kwa pamoja ili kutimiza mahitaji yetu wote.
-  Nafasi ya kutumia kwa manufaa kila uwezo na vipawa mlivyokuwa navyo.
-  Kuchangiana katika makuzi yenu ya ujumla, makuzi ya kimwili, kiriho, kihisia n.k

Imeandikwa na:
Chris Mauki
Counselor and Social Psychologist
University of Dar es Salaam
0777 407182, chriss@udsm.ac.tz

[cross-posted toka SamSasali. "Papaa" blog]



source: http://www.wavuti.com/

Jumatatu, 17 Oktoba 2011

SUKARI YA MAGENDO YAKAMATWA HIMO MOSHI.

Daniel Mjema, Moshi
MAGARI 23 yakiwamo malori na mabasi ya abiria, yamekamatwa katika Mji mdogo wa Himo wilayani Moshi Vijijini, yakiwa yamesheheni sukari na mahindi yaliyokuwa yakivushwa kimagendo kwenda Kenya.Mkoa wa Kilimanjaro umekuwa kinara wa biashara ya magendo ya sukari na mahindi na hivi karibuni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alitaka nguvu zaidi kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) kukabiliana na biashara hiyo inayosababisha uhaba wa bidhaa hizo katika soko la ndani. 

Jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Absolom Mwakyoma alisema magari hayo yalikamatwa katika maeneo mbalimbali ya mpakani katika Mji wa Himo ambako kumekuwa na operesheni maalumu ya wiki moja.

Mwakyoma alisema kukamatwa kwa malori hayo kulitokana na ushirikiano wa karibu kati ya wananchi na kikosi kazi kilichoundwa na Serikali kikiwashirikisha polisi.

Kamanda Mwakyoma alisema Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kilimanjaro, inatarajiwa kukutana wakati wowote kuanzia leo kuzungumzia hatima ya malori hayo na magari mengine yaliyokamatwa.

Kamanda Abasalom Mwakyoma.

“Hatuwezi kusema yatataifishwa au la, hilo ni mpaka kamati ya ulinzi na usalama ikae na kupata pia ushauri wa kisheria kwa sababu sheria ya kutaifisha mali ya mtu ina mlolongo mwingi,” alisema Mwakyoma.

Hata hivyo, sukari yote iliyokamatwa itauzwa kwa bei elekezi ya Serikali ambayo ni kati ya Sh1,700 na Sh1,900 kwa kilo.

Agizo la RC
Wiki iliyopita, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama aliamuru kukamatwa kwa malori yote yatakayoonekana yameegeshwa katika Mji mdogo wa Himo ambao umekithiri kwa biashara ya magendo.

Mji huo unaonekana kuwa na malori mengi kupita kiasi na muda wote wa mchana yamekuwa yameegeshwa lakini usiku wa manane ndiyo yanayotumika kuvusha sukari na mahindi kwenda Kenya.

Pamoja na jitihada hizo za Serikali na vyombo vyake vya ulinzi na usalama kudhibiti uvushaji wa sukari kwenda nje ya nchi, lakini bado bei ya sukari haijashuka kwani bado inauzwa hadi Sh2,600 kwa kilo