Ijumaa, 30 Septemba 2011

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AWAJIBISHWE-PROF. LIPUMBA.

Siku moja baada ya Mahakama Kuu kusajili tuzo ya malipo ya Shilingi bilioni 111 kwa kampuni ya Dowans, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, amemshauri Rais Jakaya Kikwete kumwajibisha Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na watendaji wake kwa kuisababishia nchi hasara hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Profesa Lipumba alisema kwamba Ngeleja na watendaji walioko chini yake ndio waliosababisha hasara hiyo ambayo sasa Serikali inapaswa kulipa hivyo ni lazima wawajibishwe mara moja.

“Wakati huu ambao Serikali imeshindwa kutatua tatizo la umeme, tunaongezewa gharama za kesi. Hili ni ombwe la uongozi ndani ya Serikali ya CCM, tangu Rais, mawaziri na watendaji wake. Nashangaa bado viongozi waliosababisha yote haya wako madarakani,” alisema Profesa Lipumba.
Prof. Ibrahim Lipumba.


Profesa Lipumba alisema tukio hilo ni matokeo ya ufisadi ndani ya Serikali kwa sababu Dowans ilitokana na mkataba wa Richmond ambao tangu mwanzo, TANESCO waliupinga, lakini baadhi ya viongozi wa Serikali wakashinikiza.

Vilevile, Profesa Lipumba aliilaumu kampuni ya uwakili ya Rex Attorney ya jijini Dar es Salaam kwa kile alichoeleza kuwa ilicheza mchezo wa kimaslahi pale ilipoishauri TANESCO kuvunja mkataba na Dowans kwa madai kuwa haukuwa halali huku ikiisaidia kampuni hiyo kupata mkopo katika benki ya Stanbic.

“Tanesco waliitumia Rex Attorney kupata ushauri wa kuvunja mkataba wa Dowans na TANESCO, lakini Rex hao wakaandika tena barua kwa Benki ya Stanbic ikitaka Dowans ikopeshwe Dola Milioni 20 za Marekani. Hawa ndiyo waliosababisha tushindwe kesi,” alisema Profesa Lipumba.

Juzi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ilibariki malipo kwa Dowans baada ya kusajili tuzo iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC), dhidi ya Tanesco na kampuni hiyo ya kufua umeme. Kwa uamuzi huo, Tanesco sasa inatakiwa iilipe Dowans kiasi cha Sh 111 bilioni badala ya Sh 94 bilioni za awali kwani inatakiwa kuilipa fidia hiyo na riba ya asilimia 7.5


source: http://www.wavuti.com/

PICHA YA LEO; MREMBO WETU WA WIKI HUYU HAPA.

Mungu kaumba.

HELIKOPTA YA CCM YAPOTEA ANGANI IKIJARIBU KUTAFUTA VITUO VYA MIKUTANO YA KAMPENI.

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, helikopta inayotumiwa na  CCM katika kampeni za Igunga imeripotiwa kupotea ikiwa angani wakati ikijaribu kutafuta vituo vilivyopangwa kwa ajili ya kumnadi mgombea ubunge wa chama hicho, Dk Dalaly Kafumu.Taarifa za kupotea kwa helikopta hiyo zilianza kuzagaa jana majira ya saa tano asubuhi mjini Igunga na baadaye zilithibitishwa na mmoja wa maofisa wa CCM ambaye hakutaka jina lake litajwe kuwa walipotea mara kadhaa baada ya mtu wanayemtegemea kuwaongoza njia kupoteza ramani akiwa angani.
“Unajua tumemchukua mtu ambaye anaifahamu vizuri Igunga ili aweze kuielekeza helikopta mahala pa kwenda, lakini kwa bahati mbaya mtu huyo alipokuwa angani alishindwa kwa sababu ya kupoteza ramani,” alisema ofisa huyo.
Helikopta ya CCM.

Awali taarifa za kupotea kwa helikopta hiyo zilitolewa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe katika mkutano wa kampeni wa chama hicho uliofanyika katika Kata ya Nkinga jana asubuhi, akisema kuwa alipata habari kuwa helikopta ya CCM ilikuwa imepotea.Mmoja wa watu waliokuwa ndani ya helikopta hiyo alisema walipotea mara kadhaa na kwamba katika harakati hizo walitua kwenye kijiji kimojawapo cha Wilaya ya Igunga jana saa nne asubuhi, lakini walijikuta kwamba wamekosea, hivyo kuondoka kwani watu hawakuwa tayari kwa mkutano huo.
January Makamba ambaye ni Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (Siasa na Mambo ya Nje) alikanusha taarifa za kupotea kwa helikopta hiyo na kuziita kuwa ni “uzushi wa kisiasa”.
Helikopta ya CCM ambayo iliwasili juzi asubuhi na kuanza kutumika katika kampeni, inadaiwa kutumia mmoja wa wenyeji wa wilayani hapo katika ziara yake kutokana na kutokuwapo  kwa maandalizi ya ramani inayojulikana kama GPRS.
“Hatuna ramani ya kumwogoza rubani, hivyo tunafanya kazi hii kwa kutumia wenyeji wanaoifahamu vizuri Igunga, kama unavyojua huko angani wakati mwingine ni vigumu kutambua eneo na hili ni tatizo kwetu," alisema ofisa huyo.Helikopta hiyo ya CCM ilirejea mjini Igunga jana majira ya saa tisa alasiri na haikufahamika iwapo kurejea huko mapema kulitokana na matatizo hayo yaliyoelezwa.

Mratibu wa Kampeni za CCM Igunga, Mwigulu Nchemba hakupatikana kuzungumzia suala hilo na pale alipotafutwa kwa simu, ilikuwa ikiita bila majibu.
Masanduku ya Kura
Katika hatua nyingine, Chadema kimesema kuna njama za kuingiza kura bandia Igunga na kwamba tayari karatasi na masanduku ya kura yamefikishwa mjini Nzega kwa ajili ya kuingizwa Igunga siku ya uchaguzi.
Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika jana majira ya saa tano asubuhi katika Kata ya Nkinga, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe alisema Chadema kina taarifa za uhakika kwamba tayari karatasi hizo zimeshawasili wilyani Nzega.
“Ndugu waandishi mlioko katika mkutano huu, hii ni taarifa rasmi ya chama na kwamba tuna taarifa za uhakika kwamba karatasi hizo zimehifadhiwa nyumbani kwa ofisa mmoja wa Serikali,” alisema Mbowe.
Aliendelea kusema kuwa tayari karatasi hizo zimeshapigwa kura na kudumbukizwa kwenye maboksi ya kupigia kura tayari kwa kuyaingiza kwenye vituo vya kupiga kura.
Mbowe alisema kuwa tayari vijana wa Chadema wameshakwenda Nzega kuimarisha ulinzi ili kuhakikisha karatasi hizo haziingii Igunga.
Mbowe aliendelea kusema kuwa mpango huo wa CCM unatekelezwa kwa msaada mkubwa wa usalama wa taifa na kuonya kuwa iwapo zinaingia Igunga basi hapatakalika.
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Chadema zimedai kuwa karatasi hizo pamoja na maboksi hayo ya kura yamehifadhiwa nyumbani kwa mkuu wa wilaya hiyo, taarifa ambazo zimekanushwa vikali na kiongozi huyo.
Mwananchi lilizungumza kwa simu na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Florence Horombe ambaye alisema kwamba, hana taarifa za kuwapo kwa masanduku hayo ya kura katika wilaya yake.
“Sina taarifa yoyote kuhusiana na karatasi hizo au jambo lolote kama hilo,” alisema mkuu huyo wa wilaya.
Nahodha: Hatumchagui mfalme Igunga
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha amesema Jeshi la Polisi litatumia ikiwezekana fedha zote lilizo nazo kuhakikisha kwamba linawapata wahusika wa kitendo cha kumwagiwa tindikali kwa mmoja wa wakazi wa Igunga, Mussa Tesha.Alisema mjini Igunga jana kuwa “tutafanya kila tuwezalo, tutatumia fedha zetu zote polisi tulizonazo, kuhakikisha watuhumiwa hawa wote wanne wanakamatwa na wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria”.
Nahodha alisema hayo wakati akijibu hoja mbalimbali za viongozi wa vyama vya siasa mjini Igunga, mkutano ambao uliibua hoja kwamba mtuhumiwa aliyekamatwa kisha kufikishwa mahakamani George Salum, alionewa.
Nahodha alisema kwa kuwa suala hilo lipo mahakamani wahusika wawe na subira na kwamba ikiwa mahakama itabaini kutohusika kwa mtuhumiwa huyo, basi ataachiwa.
Nahodha aliweka bayana kwamba juzi alimtembelea mtuhumiwa huyo gerezani na kubaini kwamba miongoni mwa wanaosakwa ni mtuhumiwa George Ernest Nyati na kwamba kufanana kwa majina hayo ndiyo chanzo cha manung’uniko hayo.
“Nimeambiwa kwamba yule mgonjwa (Tesha), anapata nafuu, sasa nami namuombea akipata nafuu hiyo hasa ya macho, tutaitisha gwaride la utambulisho na yeye atawatambua hata kama asipoweza kuwaona basi hata kwa sauti zao maana ni watu ambao aliwazoea na alikuwa akiwafahamu,”alisema Nahodha.
Katika mazungumzo yake waziri huyo alisema uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Igunga keshokutwa si wa kumchagua mfalme wala mwakilishi wa wananchi peponi, bali ni wa mbunge pekee.
Kutokana na hali hiyo, Nahodha ambaye yuko Igunga tangu Jumanne wiki hii alisema hakuna haja ya vyama vya siasa kuwa na uhasama na badala yake zifanyike siasa za kistaarabu ambazo zinawezesha wananchi wa Igunga kupata mwakilishi wanayemtaka.
“Ninachotaka kuwaeleza wenzangu hapa, ni kwamba hatuchagui mwakilishi wetu peponi, la hasha, ila tunamtafuta mbunge tu, hivyo kadhia hii yote haina maana, sidhani kama ni sahihi sana kuwa na mvutano mkubwa katika jimbo dogo tu la uchaguzi,”alisema Nahodha muda mfupi kabla ya kuingia katika mkutano na viongozi wa vyama vya siasa.
Nahodha alirudia kauli hiyo wakati alipozungumza na viongozi hao pale alipowaambia kwamba: “Hatumchagui mfalme wa Igunga”, hivyo kuwataka viongozi hao kuhakikisha wafuasi hao wanaendesha siasa za kistaarabu zisizo na uhasama.
Waitara wa Chadema alizungumzia suala la madai ya kutaka kutekwa kwa mbunge wa Viti Maalumu Ester Bulaya (CCM) na kurushiwa risasi ambapo baadaye kesi hiyo ilibadilishwa na yeye (Waitara) kutuhumiwa kurusha risasi huku polisi wakionekana kuegemea upande wa CCM."Ninachosema hapa kuwe na usawa wa kushughulikiwa matukio ya uhalifu na mtu anapofanya kosa, ashughulikiwe kama yeye na chama kisihusishwe, kwa sasa hakuna ugomvi na polisi bali ugomvi uliopo ni wa makada wa CCM na Chadema,  hapa kuna uhasama nasema ukweli," alisema.
Waitara alitaka kuhakikishiwa juu ya ushiriki wa polisi katika mchakato wa kuchakachua kura kwa kuwa katika chaguzi zingine polisi wamekuwa wakihusishwa.Kada wa CCM, Shaibu Akwilombe alitaka kuwapo kwa utaratibu mzuri kwa ajili ya watu wanaosubiri matokeo utakaoepusha vurugu kwa kuwa sheria iliyopo inasema mtu akipiga kura akae umbali wa mita 200 kutoka kituo cha kupiga kura jambo ambalo alisema ni hatari iwapo watajikusanya wengi wakiwa na itikadi tofauti.
Kwa upande wake, Katibu wa CCM Wilaya ya Igunga, Neema Adam, alikiri kutokea kwa mfululizo wa matukio ya kujeruhiana, kuchaniana picha na mabango, lakini alikanusha matukio hayo kuhusishwa na CCM ambapo aliitupia shutuma nzito Chadema kuwa ndio imekuwa ikitajwa mara kwa mara kuhusika na matukio hayo.
Polisi: Hatutapendelea chama chochote Igunga
Wakati huo huo, uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga mkoani Tabora ukitarajiwa kufanyika keshokutwa Jumapili, Jeshi la Polisi nchini limeweka wazi msimamo wake kwa kusema: "Tutahakikisha hatutumiki kwa maslahi ya chama chochote cha siasa".Kadhalika Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kupitia kwa Mwenyekiti wake wa muda, Profesa Amon Chaligha imesema, itahakikisha uchaguzi wa Igunga unakuwa huru na wa haki na kwamba mshindi halali ndiye atakayetangazwa.
Polisi katika tamko lililotolewa na Kamishna wake wa Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja imesema itahakikisha upigaji kura unafanyika kwa amani, bila vikwazo wala bughudha, kulinda usalama wa vifaa vya kupigia kura na kuhakikisha mchakato wa kupiga, kuhesabu kura na kutangaza matokeo unakuwa wazi, huru na wa haki.Chagonja aliwaambia waandishi wa habari jana mjini Igunga kuwa chombo cha umma, polisi watasimamia sheria, kanuni na taratibu zote za uchaguzi "bila upendeleo wowote" na kwamba usalama utaimarishwa kabla, wakati na baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa.
"Jeshi la polisi litaendelea kusimamia sheria, kanuni na taratibu zote bila upendeleo wowote. Kama chombo cha Umma, litahakikisha halitumiki kwa maslahi ya chama chochote cha siasa," alisema Chagonja.
Uchaguzi mdogo wa Igunga unatarajiwa kufanyika keshokutwa Jumapili, Oktoba 2, 2011 na vyama vinane vimesimamisha wagombea wakiwania kurithi nafasi iliyoachwa wazi na mbunge aliyejiuzulu, Rostam Aziz kutoka CCM.

Habari hii imeandikwa na Neville Meena, Geofrey Nyang'oro na Daniel Mjema, Igunga

CREDITS; Gazeti la Mwananchi.

NYUMBA ZABOMOLEWA KUNDUCHI MTONGANI JANA.

Nyumba Kunduchi Zabomolewa


Thursday, September 29, 2011 10:41 AMJESHI la Polisi limebomoa nyumba za wakazi eneo la Kunduchi Mtongani kwa kile kilichodaiwa kuwa zimejengwa ndani ya eneo la Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ).


">Majira ya alfajiri jana ubomoaji huo ulianza na nyumba ambazo idadi yake haijafahamika kamili lakini zilizomolewa katika taarifa ya awali zimedaiwa ni zaidi ya 30
Ubomoaji huo uliendelea kwa kusimamiwa na Kikosi cha Askari wa Kutuliza Ghasia (FFU) waliokuwa na mabomu ya machozi, silaha za moto na magari ya maji ya kuwasha.

Sababu za awali zinadai nyumba hizo zimezidi mita 50 kuingia sehemu zinapohifadhiwa silaha za jeshi kwa mujibu wa Taarifa kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni

Alhamisi, 29 Septemba 2011

AJALI YAUA TISA HUKO MBEYA

AJALI sasa ni shetani aliyeukumbatia mkoa wa Mbeya, baada ya siku chache kupita tangu watu 14 wapoteza maisha kwa ajali ya Fuso la mnadani, watu wengine tisa wamekufa na wengine 12 kujeruhiwa katika ajali nyingine.

Watu hao wamepoteza maisha katika ajali iliyohusisha basi dogo la abiria aina ya Toyota Hiace namba T 219 ASQ na gari aina ya Prado namba T 155 ACQ yaliyogongana uso kwa uso katika barabara ya Mbeya - Tunduma.

Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Gabriel Kimolo amesema leo kuwa, ajali hiyo ilitokea jana saa 1.30 usiku katika Kijiji cha Chimbuya, Mbozi mkoani Mbeya.

Kimolo amesema, dereva aliyekuwa akiendesha basi hilo, alishindwa kulimudu kutokana na mwendo wa kasi na kuyumba kutoka upande wake hadi upande wa pili na kugongana na gari hilo lililokuwa likienda Tunduma kutoka Mbeya.

Kwa mujibu wa Kimolo, waliokufa na miili yao kutambuliwa na ndugu zao ni pamoja na wanafamilia Anna Mbembela na mwanawe Mariam Mrema na Rahabu Mwaijumba na mwanawe Leah Said.

Wengine ni Binaisa Mwashiuya, Baraka Mwansite na dereva wa Hiace ambaye hajafahamika jina lake, wakati Agness Mpoli alifia njiani wakati akikimbizwa katika hospitali ya Rufaa Mbeya kwa matibabu zaidi.

Mkuu wa Wilaya aliwataja majeruhi wa ajali hiyo waliolazwa katika hospitali ya wilaya ya Mbozi iliyopo katika mji mdogo wa Vwawa kuwa ni Frank Simbeye (25) mkazi wa Chimbuya, Emmanuel Sanga (16) wa Mlowo, Agness Anthony (28) wa Mbeya na wanawe Jacqueline na Victor Christopher.

Majeruhi wengine ni mkazi wa mji mdogo wa Tunduma Anastazia Mtumbo (19), Richard Ezekiel (miezi 10) na Chenny Mwembe (25) wa Chimbuya.

Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo walisema basi hilo lilikuwa likiendeshwa na Charles Kumbi wakati Prado lilikuwa likiendeshwa na mmiliki wake, Emmanuel Kaila ambaye amelazwa katika hosptali ya Sifika mjini Vwawa akipata matibabu kutokana na kujeruhiwa vibaya.

Hata hivyo, mashuhuda hao walisema huenda ajali hiyo ilisababishwa na trekta lililokuwa eneo la tukio likiwa limebeba tangi la maji bila taa na dereva wa Hiace akitaka kulipita.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Advocate Nyombi, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kutoa mwito kwa wadau kutambua kuwa usalama barabarani unaoweza kupunguza matukio ya ajali kama hizo ni jukumu la wote

YANGA YAITUNGUA COASTAL UNION 5-0

Mchezaji wa Yanga Kenneth Assamoah akishangilia bao jana.
Davies Mwape akiruka vikwazo vya mabeki wa Coastal.

Jumatano, 28 Septemba 2011

HELIKOPTA YA CHADEMA YATIKISA IGUNGA, YA CCM BADO KITENDAWILI.CUF NAO KURUSHA KWA MARA YA KWANZA LEO.

<>  WAKATI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilitikisa anga la Igunga baada ya kuanza kutumia helikopta kufanya kampeni zake, zile mbili za wapinzani wao, CCM zikishindwa kuwasili jimboni humo na kubaki Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kutokana na sababu za kiufundi.Wakati Chadema ikipasua anga na mbili za CCM zikibaki KIA, helikopta ya Chama cha Wananchi (CUF) nayo imeshindwa kutua Igunga jana na sasa inatarajiwa hapa leo.

Helikopta ya Chadema ilianza kuonekana katika anga la Igunga saa 10:40 jioni ikiwa na maandishi makubwa ya chama hicho na rangi ya bluu.Ujio wa helikopta hiyo ulivuta kwa muda idadi kubwa ya wananchi waliokuwa kwenye Viwanja vya Sabasaba wakisubiri ujio wa helikopta mbili za CCM, ambazo awali, ilielezwa kuwa zingewasili saa 8:00 mchana.

Baadaye ilielezwa kwamba helikopta hizo za CCM zingetua Igunga saa 11:30 jioni zikiwa na makada wa chama hicho akiwamo Katibu wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Bumbuli, January Makamba.

Hata hivyo, ilipofika saa 12:00 jioni, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akitumia gari la matangazo la Bendi ya muziki ya ToT Plus alitangaza kwamba helikopta hizo zisingeweza kutua Igunga kutokana na sababu za kiufundi.
Alisema zilichelewa kupata vibali kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam na kwamba baada ya kutua KIA ilishauriwa kuwa ni vyema zilale hapo.

Alisema kama helikopta hizo zingeondoka KIA jana jioni na kufika hapa usiku wakati tayari kungekuwa na giza kitu ambacho kisingekuwa kizuri kiusalama. Alisema helikopta hizo sasa zitawasili leo saa 4:00 asubuhi.

Matumizi hayo ya helikopta yanawafanya wananchi wa Igunga kushuhudia kampeni nzito na za aina yake tangu kufanyika kwa uchaguzi wa kwanza wa vyama hivyo mwaka 1994 na Rostam Aziz kushinda.Jimbo hilo lenye wapiga kura 170,000 katika vijiji 96, halijawahi kushuhudia kampeni nzito kiasi hicho zinazohanikizwa na magari yenye vifaa vya kisasa vya muziki.

Habari kutoka ndani ya CCM, zinaeleza kuwa katika kujihakikishia kura katika kipindi hiki cha lala salama, chama hicho kitawatumia makada wake, Makamba na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli wanaoelezwa kuwa na ushawishi mkubwa.

Kulingana na vyanzo mbalimbali vya habari, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa aliyekuwa mgeni rasmi katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za CCM anatarajiwa kurudi tena hapa keshokutwa.Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe naye aliwasili hapa jana kuongeza nguvu kwa viongozi wa chama hicho ambacho idadi kubwa ya wabunge wake wameweka kambi hapa.

Helikopta ya CUF
Kwa upande wake, CUF kinatarajiwa kuanza kutumia helikopta yake kuanzia leo huku Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Juma Duni Haji akitarajiwa kufunga pazia la kampeni za chama hicho ambazo, awali zilitarajiwa kufungwa na Katibu Mkuu wake ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad.

Akizungumzia na waandishi wa habari jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Julius Mtatiro alisema kampeni hizo sasa zitafungwa na Haji anayetarajia kuwasili wakati wowote katika kipindi hiki cha mwisho wa kampeni.Mtatiro alisema tayari wabunge wa chama hicho  akiwamo Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Zanzibar) Ismail Jussa wanaendelea na kampeni jimboni humo.

Chanzo; Mwananchi

KUMBE MATUNDA NI BORA KULIKO CHIPS MAYAI

Matunda mchanganyiko.

Mchanganyiko wa mboga na mtunda.


Chips Mayai, chakula kinachopendwa na Watanzania wengi hasa wakazi wa mijini.
WATAALAMU wa Kilimo na Afya wamesema kuwa vifo vingi husababishwa na ulaji hafifu wa matunda na mboga za majani huku wakihadharishwa kuwa ulaji wa chipsi mayai unachangia unene unaosababisha vifo vya ghafla.

Katika mkutano wa kwanza wa uhamasishaji matumizi ya bidhaa za matunda na mboga unaofanyika mjini Arusha, wataalamu hao walisema inapotokea vifo vya namna hiyo, baadhi ya watu kusingizia sababu mbalimbali hususani uchawi.

Wamebainisha kwamba watu wengi wanakula matunda na mboga chini ya kiwango cha gramu 400 kilichowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), jambo ambalo ni hatari kwa afya.

Mtaalamu kutoka WHO, Godfrey Xuereb alisema jana kwamba takribani watu milioni mbili hufa kila mwaka kutokana na maradhi yanayosababishwa ukosefu wa lishe za matunda na mboga.

Mwenyekiti wa Baraza la kuendeleza Kilimo cha Matunda na Mboga (Hodect), Felix Mosha alisema viazi vilivyochomwa kwenye mafuta na kuchanganywa na mayai ya kukaanga maarufu kama Chipsi Mayai unaonesha kushika hatamu katika lishe za wakazi wa mijini hasa vijana na wanawake.

Akielezea chakula hicho kama mlo ‘mchafu’, Mosha Alisema: “Matokeo yake taifa sasa limekumbwa na tatizo la unene uliokithiri hasa miongoni mwa watoto na akina mama na kuchangia vifo vingi isivyotarajiwa.” Ofisa kutoka Wizara ya Kilimo na Chakula, Geoffrey Kirenga Alisema:

“Na mara nyingi mtu akionekana mnene huchukuliwa kuwa na afya lakini ukweli wengi huwa na utapiamlo na wanapofariki ghafla wanakuwa chanzo cha uvumi, tetesi na hisia za ajabu wakati chanzo hasa huwa ni ukosefu wa vitamini na madini yatokanayo na matunda na mboga”.

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe akifungua mkutano huo, alisema wastani wa mtanzania mmoja hula gramu 80 pekee za matunda na mboga kwa siku.

“Hii ni asilimia 20 tu ya kiwango kilichowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) ambacho ni gramu 400 kwa mtu mmoja kwa siku.”

Alisema Maghembe na kuongeza kuwa asilimia kubwa ya Watanzania humaliza hadi miezi miwili bila kugusa hata tunda moja.

“Na hii ni aibu maana hapa nchini kuna matunda ya kila aina ambayo pia hupatikana kwa bei ya chini sana, lakini bado watu hawana mwamko wa kuyatumia kiafya na hata katika mila zingine matunda na mboga huonekana kuwa ni vyakula vya watoto,” alisema Waziri Maghembe

WANAZUONI WALAANI CHADEMA KUSHINDWA KUOMBA RADHI KWA KUMVUA HIJAB BI. KIMARIO.


Katibu wa Sekretarieti ya Wanazuoni, Sherally Huseein (kulia) akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)kukataa kuomba radhi kwa Waislamu kufuatia udhalilishaji wa kumvua hijabu Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Mkoani Tabora, Fatma Kimario hivi karibuni. (Picha na Mwanakombo Jumaa- Maelezo

Jumanne, 27 Septemba 2011

MAMBO YA MFALME MSWATI HAYO, MSIMU WA KUCHAGUA MKE UMEWADIA.

Warembo katika pozi mbalimbali ili wachaguliwe kuolewa na mfalme huko Swaziland.
Inasemekana wote huwa ni mabikira.

MBUNGE NA MADIWANI CHADEMA WACHUKUA POSHO YA VIKAO VYA BARAZA LA MADIWANI ARUSHA.

MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema amekiri kusaini na kuchukua posho ya kikao cha Baraza la Madiwani mwishoni mwa wiki, lakini akatetea uamuzi huo akisema alikwenda kuzima
njama za kufukuzana.
Mh. Godbless Lema


Lema na madiwani wenzake watatu wa Chadema, walishiriki katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Arusha, kinyume cha msimamo wao wa kutohudhuria vikao hivyo.

Mapema mwaka jana, Lema na madiwani wote wa Chadema wa Jiji la Arusha waliweka msimamo wa kutomtambua Meya wa Jiji hilo, Gaudence Lyimo na kutohudhuria vikao vyote vya Baraza la Madiwani kwa madai kuwa Meya huyo hakuchaguliwa kwa mujibu wa sheria na kanuni na kuhudhuria vikao ni kumtambua.

Lakini Ijumaa iliyopita, Lema na madiwani Isaya Doita (Ngarenaro), Crispin Tarimo (Sekei) na Sabina Francis (Viti Maalumu), walihudhuria kikao hicho na kupokea posho kwa malipo ya kuhudhuria kikao.

Lema alikiri alisaini posho hiyo yeye na wenzake na kudai kulikuwa na njama za kutaka kuwafukuza madiwani wa Chadema kwa kukosa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo bila ya kuwa na taarifa yoyote na kwa mujibu wa sheria na kanuni wangetimuliwa.

Alisema kwa kufanya hivyo siyo kama wamebadilisha msimamo wao wa kutomtambua Meya
Lyimo na Naibu wake, Estomii Mallah, isipokuwa ilibidi wafanye hivyo kutegua mtego wao wa madai ya kufukuzwa madiwani.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Estomii Chang’a alisema madiwani wa Chadema walipewa posho baada ya kuhudhuria kikao hicho na wala hakukuwa na njama za kutaka kuwafukuza kama alivyodai Lema

WIKI YA LALA SALAMA IGUNGA, WASHINDANI NI CUF, CCM NA CHADEMA.

Daniel Mjema, Igunga
KAMPENI za uchaguzi mdogo jimbo la Igunga, leo zinaingia katika wiki ya lala salama huku tathmini ikionyesha kuwa mchuano mkali ni baina ya vyama vitatu, licha ya vyama nane kusimamisha wagombea wake.

Vyama vyenye ushawishi mkubwa kisiasa jimboni humo katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2, ni CCM kilichomsimamisha Dk Dalaly Kafumu, CUF kilichomsimamisha Leopard Mahona na Chadema ambacho kimemsimaisha, Joseph Kashindye.

Uchaguzi huo pia unavishirikisha vyama vya SAU, UPDP, DP, AFP na Chausta, lakini baadhi yake kampeni zake zinaendeshwa kwa kusuasua, huku vingine vikishindwa kabisa kufanya kampeni hizo.

Katika muda wa wiki mbili za kampeni Igunga, kumekuwa na matukio baadhi ya vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo kutuhumiana kwa matukio ya uhalifu, ukiwamokampeni chafu, ubakaji, kumwagiwa tindikali, udhalilishaji na hata vitisho vya kutumia silaha za moto kama bastola.

Mvutano mkali zaidi upo baina ya CCM na Chadema, ambavyo makada wake wamekuwa wakipiga kambi za muda mrefu, ikiwa ni pamoja na kulala katika maeneo yenye idadi kubwa ya wapigakura.

Juzi Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe ambaye ni miongoni mwa wanasiasa wenye ushawishi alitua kukiongezea nguvu chama chake, lakini tayari CCM kilikwishaongeza wapiga kampeni wake wakiwamo, Katibu Mkuu mstaafu wa chama hicho Philip Mangula. Kwa upande wake CUF kinajivunia mtaji wa kura 11,000 ilizopata katika uchaguzi wa mwaka jana. 

Mbinu nyingine ambayo imekuwa ikitumiwa katika kampeni hizo ni wagombea kujinadi kwa lugha ya kisukuma kutokana na wapigakura wengi wa jimbo hilo kuzungumza lugha hiyo ikilinganishwa na Kiswahili.

Hali hiyo imekuwa ikiwapa wakati mgumu wanahabari kufuatilia mikutano hiyo kutokana na wengi kutofahamu lugha hiyo, isipokuwa pale anapokuwapo mkalimani wa kutafsiri maneno husika Kiswahili.

Katika wiki ya mwisho iyaoanza leo, viongozi wa kitaifa wa vyama vyenye ushindani, wanatarajiwa kuhamia Igunga, ili kunadi sera za wagombea wao ili kujihakikikisha ushindi.

Inachojivunia CCM
CCM ambacho kinadai kuwa na mtaji wa kura 39,000 ilizozipata katika uchaguzi mkuu uliomalizika Oktoba mwaka jana, kimekuwa kikijivunia mfumo wa uongozi kuanzia ngazi ya mabalozi, shina, kata hadi wilaya.

Chama hicho kinaamini kuwa kama viongozi wao hao hawatakisaliti basi kina uhakika wa kutetea kiti hicho kilichoachwa wazi na Rostam Aziz aliyejiuzulu huku kikiamini kushinda kwa zaidi ya asilimia 60.

Mbali na uongozi huo, lakini chama hicho kina madiwani 24 kati ya 26 na kinaamini kuwa madiwani hao pia wana ushawishi mkubwa kwa vile walichaguliwa na wananchi kwa kura.

Katibu Mkuu wa CCM, Willison Mukama wiki iliyopita alisema chama chake pia kinajivunia sera nzuri kwenye huduma za jamii ikiwamo mradi mkubwa wa maji wa Shinyanga-Nzega-Igunga ambao utafanya tatizo sugu la maji Igunga kuwa historia.

CCM kimejenga imani kwamba tuhuma dhidi ya Chadema kwamba wanafanya vurugu, zinaweza kukisadia kuendelea kuliongoza jimbo hilo ambalo halijapata kuwa na mwakilishi wa upinzani.

Baadhi ya makada wa CCM wanaweka wazi kwamba Chadema ambacho ni chama kikii cha upinzani nchini, kimejikuta kikisigana na CUF ambao pia ni wapinzani na kwamba CCM wanaweza kunufaishwa na hali hiyo.

Kwa mtizamo huo, CCM kinaamini CUF kitasaidia kupunguza kura za Chadema ambacho hakina mizizi jimboni humo ikilinganisha na CUF ambacho kilishiriki uchaguzi mkuu 2010 na kunyakua kura 11,000.

Hivyo ipo imani kwamba Chadema na CUF vinaweza kujikuta vikigawana kura za wale wanaounga mkono upinzani, hivyo CCM kushinda kwa urahisi. Vijana kuwabeba Chadema
Kwa upande wake Chadema ambacho ni chama kipya katika siasa za Igunga, kinaamini kitashinda uchaguzi huo kwa kile kinachodai ni kufanikiwa kujipenyeza katika kundi la vijana ambao ni wengi.

Hakuna ubishi kwamba katika mikutano ya chama hicho, kundi kubwa linaloonekana kukiunga mkono ni vijana ambao wanaamini matatizo makubwa ya ajira na maisha magumu yamesababishwa na CCM.

Jambo jingine, Chadema kinaamini mgawanyiko ndani ya CCM uliosababishwa na kujiuzulu kwa Rostam, pia utapunguza kura za chama tawala na kuwanufaisha wapinzani.

Wafuasi wa Rostam wanadaiwa ‘kununa’ na kufanya kampeni za chinichini ili kuhakikisha CCM hakishindi uchaguzi huo.

Jambo lingine ambalo Chadema kinaamini litapunguza kura za CCM ni hatua ya kumsimamisha Dk Kafumu katika wakati ambao kuna kelele nyingi kuhusu ufisadi katika sekta ya madini ambayo yanadaiwa kutowanufaisha Watanzania.

Kabla ya kuteuliwa kwake kupeperusha bendera ya CCM, Dk Kafumu alikuwa kamishina wa madini na Chadema na CUF vinatumia hilo kama silaha ya kummaliza mgombea huyo kwamba alishiriki ufisadi.

CUF na mtaji wa kura 11,000
CUF kwa upande wao wanaamini kuwa kura 11,000 kilizozipata 2010, mgawanyiko ndani ya CCM unaotokana na kundi la Rostam na vurugu zinazotokea jimboni humo zitasaidia kukivusha na kushinda.

Mbali na hayo lakini CUF kinaamini kuwa ndicho pekee kimeendesha kampeni za kistaarabu kulinganisha na vyama vingine na kutokana na hulka ya wenyeji kutoshabikia vurugu basi watakipa kura.

Pia CUF kinaamini kwamba mchuano mkali kati ya Chadema na CCM kutavifanya vyama hivyo viwili kugawana kura hivyo wao kupata ushindi kutokana na ushawishi walioufanya kwenye kampeni.

CUF kinaamini mgombea wake ndiye mwenye nguvu na anayekubalika zaidi na kwamba hata 2010 angeweza kuibuka mshindi lakini kutokana na ‘nguvu’ kubwa aliyoitumia Rostam ndio iliyochangia kumwangusha.

Kinachotarajiwa

Kutokana na hali ilivyo na ushindani mkubwa baina ya vyama vya Chadema, CUF na CCM, wadadisi wa siasa wanasema lolote linaweza kutokea katika jimbo hilo.

Wiki ya mwisho ya kampeni hizi inaweza kutoa mwelekeo wa nani atakuwa mshindi lakini kwa mtizamo wa kidadisi, hadi sasa hakuna chama chochote chenye uhakika wa ushindi.

Uchaguzi huo mdogo unatarajiwa kufanyika Oktoba 2 huku wapiga kura waliojiandikisha wakiwa 170,000 lakini wanaweza wasijitokeze wote kama ilivyotokea mwaka jana ambapo ni asilimia 40 waliojitokeza

MTOTO MWENYE SURA MBLI AZALIWA PAKISTAN, MUNGU MKUBWA.


NewsImages/5968126.jpg
Mtoto mwenye sura mbili aliyezaliwa nchini Pakistan
Mamia ya watu wamekuwa wakimiminika kwenye wadi ya wazazi ya hospitali moja nchini Pakistan ili kumshuhudia mtoto mwenye kichwa chenye sura mbili aliyezaliwa juzi nchini humo.
Mtoto huyo alizaliwa usiku wa kuamkia ijumaa akiwa na kichwa kimoja chenye sura mbili tofauti.

Mtoto huyo aliyezaliwa kwa njia ya kawaida bila ya operesheni alikuwa na uzito wa kilo 3.2. Alizaliwa kwenye mji wa Palandri uliopo Azad Kashmir nchini Pakistan.

Hali aliyo nayo mtoto huyo inajulikana kitaalamu kama "Craniofacial duplication" ambapo kichwa chake kilikuwa na sura mbili ambapo alikuwa na midomo miwili, macho manne, pua mbili isipokuwa tu alikuwa na masikio mawili tu.

Ana ubongo mmoja na kwajinsi maumbile yake yalivyoungana madaktari wanasema kuwa ni vigumu sana kumfanyia operesheni ya kurekebisha sura yake ili awe sawa na watoto wengine.

Daktari wa hospitali ya HFH aliyozaliwa mtoto huyo aliyejitambulisha kama daktari Nasira, alisema kuwa wana matumaini madogo sana mtoto huyo ataishi muda mrefu kwani hadi sasa anashindwa kupumua vizuri na analishwa kwa kutumia mrija.

"Tuna matumaini madogo ya kunusuru maisha ya mtoto huyu", alisema daktari Nasira.

Mtoto huyo alizaliwa katika familia ya bwana Khalil Ahmed na mkewe Shahida Perveen ambao wana watoto watatu waliozaliwa bila ya kuwa na dosari yoyote kwenye maumbile yao.

Mama wa mtoto huyo bado amelazwa hospitali pamoja na mtoto wake ambaye amelazwa kwenye kitengo maalumu akipatiwa matibabu maalumu ya kunusuru maisha yake

Jumatatu, 26 Septemba 2011

KARIBU TANZANIA, PRIDE OF SIMBA

Simba hawa walikutwa wanacheza, watalii toka Kenya na Tanzania wakiangalia huko Serengeti.

PICHA YA LEO; TUJIKUMBUSHE SIKU MBWA WA POLISI ALIVYOKATA KAMBA NA KUINGIA UWANJA WA MPIRA.

Polisi akiwa amemdhibiti mbwa wake akisimamia foleni siku ya mechi ya ligi kuu ya Vodacom kati ya Simba na Toto Africa ya Mwanza huko CCM Kirumba juma lililopita.

Hapa mbwa amekata kamba na kuingia uwanjani, hapa inasemekana alikuwa anamkimbiza mchezaji wa Simba Haruna Moshi 'Boban', sijui kwa nini amuandame yeye tu.

Wachezaji wakiwa wametahayari wasijue lakufanya, je huu ni uzembe au bahati mbaya kwa polisi huyu!!?

PROFESA WANGARI MAATHAI WA KENYA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUUGUA KANSA.

Wangari Maathai
Wangari Maathai - R.I.P (photo: takingrootfilm.com)
Kenya's Nobel laureate and conservation heroine Professor Wangari Muta Maathai (aged 71), has died in Nairobi while undergoing cancer treatment.

"It is with great sadness that the Green Belt Movement announces the passing of its founder and chair, Professor Wangari Muta Maathai, after a long illness bravely borne," her organization said.

The environmentalist, activist and politician died at the Nairobi Hospital at around 10pm on Sunday (September 25th, 2011), according to officials at her Green Belt Movement organisation.

She was born on 1 April 1940 in Ihithe village, Tetu division, Nyeri District in Kenya. She was educated in the United States at Mount St. Scholastica and the University of Pittsburgh, as well as the University of Nairobi in Kenya.

Prof. Maathai won the Nobel Peace Prize in 2004 for promoting conservation, women's rights and transparent government - the first African woman to get the award.

She was elected as a Member of the Kenyan Parliament in 2002 and served as Assistant Minister for Environment and Natural Resources in the government of President Mwai Kibaki between January 2003 and November 2005.

In the 1970s, Maathai founded the Green Belt Movement, an environmental non-governmental organization focused on the planting of trees which has planted 20-30 million trees in Africa., environmental conservation, and women's rights. In 1984, she was awarded the Right Livelihood Award, and in 2004, she became the first African woman to receive the Nobel Peace Prize for “her contribution to sustainable development, democracy and peace.”
The organisation also campaigned on education, nutrition and other issues important to women.

Ms Maathai had been arrested several times for campaigning against deforestation in Africa

Ijumaa, 23 Septemba 2011

HAINA NAMNA LAZIMA TUMKUBALI!!!!! KIKWETE USO KWA USO NA KIONGOZI WA WAASI WA LIBYA.

Picture
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na kiongozi wa kiongozi wa Serikali ya mpito ya Libya, Mustafa Abdel-Jalil
Picture
Rais Kikwete katika maongezi mafupi na Mustafa Abdel-Jalil
Picture
Rais Kikwete akimtabulisha Balozi wa Kudumu wa Tanzania Umoja wa Mataifa, Ombeni Sefue kwa Mustafa Abdel-Jalil


source: http://www.wavuti.com/

AJALI MBAYA YA LORI KUGONGANA NA GARI DOGO MBALIZI MBEYA JANA

Polisi wakiangalia gari aina ya roli lenye namba IT.9518, lililopata ajali baada yakugongana na gari jingine na hivyo kupinduka na kusababisha vifo vya watu watatu watembea kwa miguu na kuvunja nyumba.
Gari iliyogongana na lori.


Chanzo;globalpublishers.info

PATRIOTIC FRONT ZAMBIA YASHINDA UCHAGUZI

Kiongozi wa Upinzani aliyeshinda Uchaguzi Zambia, Michael Satta

Mpinzani ashinda uchaguzi Zambia

Kiongozi wa chama cha Patriotic Front, MichaEl Sata ametangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais nchini Zambia
Bw Sata alipata asilimia 43 ya kura zilizopigwa na kumshinda Rais Rupiah Banda wa chama tawala cha MMD ambacho kimekuwa mamlakani kwa muda wa miaka 20.
Michael Sata
Kiongozi wa Patriotic Front ameshinda uchaguzi wa urais Zambia


Tangazo hilo lilitolewa na Jaji Mkuu wa Zambia Ernest Sakala.
Awali watu wawili waliuawa kufuatia ghasia katika maeneo ambayo ni ngome ya upinzani.
Mkuu wa Polisi wa jimbo hilo maafuru kwa uzalishaji Shaba ameliambia shirika la habari la Reuters watu wamejitokeza katika barabara za mji wa Kitwe na Ndola wakivurumisha mawe.
Mwandishi wa BBC anasema ghadhabu hizi zimechochewa na agizo la serikali kupiga marufuku vyombo vya habari kutangaza matokeo bila ya idhini ya tume ya uchaguzi ya nchi hiyo.
Mwandishi wa BBC Mutuna Chanda akiwa Lusaka kilomita 300 kusini mwa Kitwe, anasema huko Kitwe, waandamanaji waliteketeza soko moja usiku na Polisi wameweka vizuwizi katika mji wa Wusaikile.
Rais Banda alimshinda Bw Sata kwa kura 35,000 katika uchaguzi wa mwaka 2008, matokeo yaliozusha ghasia kutoka upande wa upinzani katika ngome zao za mijini.
Tangu uchaguzi wa mwaka 2008, watu wengine milioni moja wamejiandikisha kuwa wapiga kura,wengi wao vijana wasio na ajira

Alhamisi, 22 Septemba 2011

ANTI-CORRUPTION WEBSITE IS DUE ONLINE, HONGERA FREDRICK FUSSI NA WENZIO.

Kijana mwanzilishi wa mtandao huo, Fredrick Fussi.

 
ripoti rushwa
Unaweza kuripoti vitendo vya rushwa kupitia / report corruption via: ripotirushwa.or.tz
----

Corruption in the health sector in Tanzania has been a stumbling block upon accessing services, something that has culminated loss of lives, especially people with meager income.

In a move towards finding the lasting solution on the vice which has been increasing at alarming rate, Tanzania Youth Vision Association (TYVA) launched anti-graft awareness community campaign in September10, this year in all secondary schools of Dar es Salaam region, aimed at creating awareness and sensitization.

The campaign, sponsored by the World Bank (WB) through the British Council, is part of Anti Corruption Journalism for Health (ACJH) project which kicked off in the mid of August this year, to fight and combat corruption in the health sector.

The campaign is colored by various testimonies from different students who adduced before the public the scenarios in which they were forced by officials from the health sector to give bribes in exchange of the service. It was held at Azania Secondary School in Dar es Salaam.

“I once bribed a doctor when I was undergoing medical examination to fill in the form for joining Azania Secondary school so that I could ease the exercise when I realized that it was very hard to be examined without bribing the doctor on duty’’, said Mbwana Msangula.

Msangula says that a doctor at Amana hospital in Ilala district solicited 3,000/- from him. He had no other alternative than to give him, simply because he was in a great need to proceed with his studies.

According to ACJH Project Manager Mr Fredrick Fussi this campaign dubbed ‘Ripoti Rushwa Community Campaign’’ started with secondary schools in Dar es Salaam and Cost regions, after which it would involve the community at large in both regions



source: http://www.wavuti.com/

WAKILI FELIX MKONGWA KIZIMBANI KWA KUGHUSHI

Wakili wa kujitegemea Felix Mkongwa amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka ya kughushi na kujipatia kiwanja kwa njia za udanganyifu.

Wakili wa Serikali Leonard Shayo alidai jana mbele ya Hakimu Mkazi Rita Tarimo kwamba Mkongwa alitenda makosa hayo Juni 3, 2005 jijini Dar es Salaam.

Katika shitaka la kwanza, anadaiwa kuwa alighushi mkataba wa kuuziana kiwanja namba 600 block G Tegeta jijini Dar es Salaam ikionesha kwamba imesainiwa na mmiliki halali George Kimwaga akijua sio kweli.

Mkongwa anadaiwa katika shitaka la pili kwamba alijipatia mali kwa njia za udanganyifu na kwamba tarehe hiyo alijipatia kiwanja hicho akionesha kwamba ameuziwa na Kimwaga.

Wakili Mkongwa amekana mashitaka hayo na yuko nje kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya dhamana yaliyomtaka kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika na kusaini hati ya dhamana ya Shilingi milioni 10. Kesi hiyo itatajwa Oktoba 24 mwaka huu.


source: http://www.wavuti.com/

Jumatano, 21 Septemba 2011

WANAZUONI WAKIISLAMU WALAANI KITENDO CHA DC IGUNGA KUVULIWA HIJAB

WANAZUONI wa Kiislamu nchini wameipa siku tatu Chadema Taifa kulaani kitendo cha wafuasi na viongozi wake kulidhalilisha vazi tukufu la hijab na kumwomba radhi Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Fatuma Kimario, kwa kumvua sitara yake.

Wamesema iwapo chama hicho kitapuuza kufanya hivyo na kupita muda huo wanazuoni hao na Waislamu wataiona Chadema kama chama chenye sera na madhumuni ya kuhujumu Uislamu na Waislamu wa Tanzania na kuhimiza Waislamu kukiepuka kama ukoma.


Kauli hiyo iko kwenye tamko la Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania (HAY-AT) lililosomwa jana na Naibu Katibu Mkuu wa Sekretarieti Kuu ya Umoja huo, Shehe Sherali Hussein Sherali na kusema siku tatu hizo zilianza jana.

Wanazuoni hao zaidi ya 10 wakiongozwa na Mwenyekiti wao, Shehe Suleimani Kilemile, walitoa tamko hilo mbele ya waandishi wa habari na kusema baada ya hapo umoja huo utakaa na kutafakari hatua stahiki za kukabiliana na dharau hizo na kuelekeza Waislamu cha kufanya.

Sherali alisema ifahamike, kwamba shambulio lolote dhidi ya hijab ni dhidi ya Uislamu na Waislamu wote, haliwezi kuvumilika na watakabiliana na yeyote anayetaka kuidhalilisha amri ya hijab iliyo katika Quran sura ya 33:59.

“Tunataka ifahamike, kwamba yeyote atakayelidharau vazi la hijab kwa kauli au vitendo, atakuwa amewachokoza Waislamu na sisi kamwe hatukubali hilo liendelee na kukaa kimya, tutachukua hatua stahiki na ikibidi tutalazimika kuondoa munkari kwa mikono yetu wenyewe, kama dini yetu inavyotuelekeza,” alisema.

Aliongeza kuwa wanalaani na kupinga kitendo kilichofanywa na wanaodaiwa kuwa wafuasi na viongozi wa Chadema kumvua nguo Mkuu huyo wa Wilaya na kumwacha bila sitara.

Alisema Kimario ni Mwislamu anayefuata mafundisho ya Uislamu yanayomtaka kila
mwanamke ajisitiri kwa vazi la hijab, hivyo kumvua ni kumdhalilisha kwa wanajamii kama mwanamke wa Kiislamu, mama mwenye watoto na kiongozi wa Serikali.

Tumetafakari tukio hili kwa undani na tunalichukulia kama shambulio la wazi na la makusudi dhidi ya mafundisho yetu na dini ya Kiislamu, yanayomtaka kila mwanamke aliyevunja ungo, kujisitiri kwa kuvaa vazi la hijab,” alisema Sherali.

Aliwaomba Watanzania wote, wanaharakati wa asasi za kijamii na wa haki za binadamu, viongozi wa vyama vya siasa na wa dini zote, kulaani na kupinga unyanyasaji huo wa kijinsia na kidini unaokwenda kinyume na Katiba ya nchi na utamaduni wa Watanzania wa kuheshimiana.

“Tumesikitishwa na ukimya wa asasi za kijamii zinazodai kutetea haki za binadamu na za wanawake, kutolaani kitendo hiki cha mwenzao kudhalilishwa kijinsia, kuendelea kukaa kimya kunatulazimisha kuwaona wanafiki na ndumilakuwili juu ya madai yao ya kutetea wanawake,” alisisitiza.

Alisema wanaitaka Serikali ilitafakari kwa kina tukio hili la kudhalilishwa mwanamke Mwislamu, akilitumikia Taifa kama mmoja wa viongozi wake, kukaa kimya kutatoa tafsiri hasi juu ya jinsi inavyolichukulia tukio hilo na kuitaka kuwachukulia hatua kali wahusika.

Wanawake Waislamu Katika hatua nyingine, kikao cha wanawake Waislamu kilichofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee Jumapili, wanawake walilaani tukio hilo.

Kikao hicho chini ya Mwenyekiti wake Fatma Juma, kiliwataka wanawake na wapenda amani wote kulaani kitendo hicho cha udhalilishaji wanawake.

Walisema kitendo hicho kimeonesha dharau, si tu kwa Uislamu, bali hata kwa madhehebu mengine na kinaweza kuvuruga amani na utulivu uliopo nchini hivi sasa.

Tamko la kikao hicho, lilisema litaanza kusambazwa katika misikiti yote Ijumaa, ili Waislamu waelewe namna walivyoguswa na kusononeshwa na tukio hilo.

Shura ya Maimamu
Habari zaidi zilizopatikana zilisema Shura ya Maimamu nayo itakutana hivi karibuni kujadili tukio hilo la mwanamke wa Kiislamu kuvuliwa hijab.

Mbali ya kukutana huko, Shura hiyo itaandaa maandamano ya kupinga kitendo hicho ambacho wamekitafsiri kuwa ni matusi dhidi ya Uislamu.


Katibu wa Shura ya Maimam, Shehe Ponda Issa Ponda, jana alithibitisha kuwapo kwa ajenda hiyo.

Akizungumza na gazeti hili jana alisema kitendo kilichofanywa na wafuasi wa Chadema kimekosa utu, ustaarabu, uungwana na maadili mema na kinapaswa kukemewa na wapenda amani wote nchini, bila kujali itikadi zao, kwani kikiachwa kitazidi kukomaa na kuonekana ni
jambo la kawaida katika jamii.

Akizungumzia kadhia hiyo, Katibu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini (Baraza Kuu), Shehe Ramadhan Sanze, naye alisema taasisi yake inaungana na wanaolaani tukio hilo .

“Mtazame DC Fatuma namna alivyokuwa akivutwa, akivuliwa nguo na akitukanwa na vijana wale wa Chadema ambao baadhi yao ni sawa na watoto wake wa kuzaa, hakika inatia uchungu,” alisema Shehe Sanze kwa masikitiko na kuongeza kuwa wanawake kote nchini wamedhalilishwa kwa uhuni ule.

Nao baadhi ya Waislamu ndani ya Chadema wameeleza kukasirishwa na kitendo hicho cha wenzao kumvua kwa nguvu hijab Mkuu wa Wilaya.

Waislamu hao ambao hawakutaka kutajwa majina, walisema watakutana hivi karibuni kujadiliana juu ya hatua za kuchukua kutokana na tukio hilo la kudhalilisha dini yao.

Kwa karibu wiki nzima baada ya tukio hilo la Igunga watu mbalimbali wametuma salamu zao za kulaani tukio hilo kupitia Radio Imani ya Morogoro na Radio Kheri na Radio Quran.

Viongozi watatu wa Chadema wakiwamo wabunge wawili wamefikishwa mahakamani Tabora, wakikabiliwa na mashitaka manne ya wizi wa simu, shambulio, matusi ya nguoni na utekaji
nyara. Kesi yao iliahirishwa juzi hadi Oktoba 10.

Chadema wang’aka
Akizungumzia tuhuma hizo jana, Mwanasheria wa Chama cha Chadema Tundu Lissu alisema hawajapata taarifa ya suala hilo na kuwataka wanazuoni hao kufahamu kuwa Mkuu wa Wilaya hakuvuliwa hijab na wala hakudhalilishwa kama inavyodaiwa.

Alisema ushahidi wa suala hilo unaonekana katika kesi waliyofunguliwa wanachama hao na hakuna tuhuma za kumdhalilisha kijinsia wala shambulio la aibu.

“Hatuna chochote cha kuomba msamaha kutokana na hali halisi ilivyokuwa, labda kama ingekuwa kweli alivaa hijab,” alisema Lissu.

Aliongeza kuwa kwa mujibu wa picha, Mkuu huyo wa Wilaya alikuwa amevaa mtandio, gauni linaloishia magotini na lenye mikono mifupi wakati hijab anavyoelewa yeye ni nguo inayofunika mwili mzima isipokuwa uso

MAHITA AKUBALI AMRI YA MAHAKAMA

Bw. Omari Mahita.

 
Hatimaye, aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Omar Mahita amekubali kutekeleza hukumu ya Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam kuhusu mtoto aliyekuwa akimkataa kwamba si wake, ambaye alizaa na mtumishi wake wa ndani, Rehema Shabani.

Jana Mahita alilipa gharama za malimbikizo ya matunzo ya kumhudumia mtoto huyo kuanzia mwaka 2003 hadi siku ya hukumu ilipotolewa Septemba mwaka juzi, ambapo alilipa Shilingi milioni 9 kupitia kwa wakili wake, Charles Semgalawe kwa kampuni ya udalali ya Nasm Auction Mart ambayo ilipewa jukumu na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni kufuatilia fedha hizo, na kuahidi kulipa Shilingi milioni 3 zilizobaki baada ya siku 30 kuanzia jana.
Mtoto Juma na mama yake.


Mahakama hiyo pia ilimtaka Mahita kulipa Sh 100,000 kila mwezi kwa ajili ya matunzo ya mtoto huyo baada ya kulipa Sh milioni 12 hizo.

Uamuzi wa Mahakama ulitokana na Mahita kugoma na hivyo mama wa mtoto kurudi mahakamani na kutoa taarifa. Mtoto wao, Juma Mahita kwa sasa anasoma kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari ya Hananasif Kinondoni.

Kampuni ya Nasm Auction Mart  ilitoa notisi ya siku 14 kwa Mahita awe amelipa fedha hizo, vinginevyo hatua ya kutumia nguvu kukamata mali zake ingetumika.  Notisi hiyo ilikuwa inamalizika jana na kwa kuwa sehemu ya fedha hizo ilitolewa na kuhidi kumaliza kiasi kilichobakia ndani ya siku 30, hatua ya kutumia nguvu iliondolewa.

Katika kesi hiyo, Mahakama ya Kinondoni ilijiridhisha kuwa mtoto huyo ni wa Mahita kutokana na ushahidi wa upande wa mlalamikaji uliowasilishwa mahakamani hapo, ukiwapo wa vipimo vya vinasaba (DNA).

Hata hivyo, Mahita alikata rufaa kupinga hukumu hiyo, rufaa ambayo nayo ilitupiliwa mbali na Mahakama Kuu.

Katika uamuzi wa rufaa hiyo, Jaji Dk. Fauz Twaib wa Mahakama Kuu, aliunga mkono hoja za wakili wa mlalamikaji  kuwa ingawa sheria inatamka fidia ya Shilingi 100/- lakini mahakama inaweza kuangalia hali ya maisha na uwezo wa mlalamikiwa na hivyo kuweza kuongeza kiwango hicho.  Alisisitiza kuwa katika shauri husika, kiwango kilichoamuriwa na Mahakama ya chini kilizingatia hali ya kiuchumi hususan gharama za maisha na uwezo wa mrufani kuweza kulipa na kwa mujibu wa barua kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwenda kwa Mahakama, mrufani hakuweza kufika kwa ajili ya uchunguzi mara sita kwa nyakati tofauti.

Jaji Twaib akasema Mahakama ya Kinondoni ilikuwa sahihi na hivyo kumtaka Mahita kulipa pia gharama za kesi hiyo

WAKOREA WAPATIKANA NA HATIA YA KUTOA RUSHWA.

Boss wa Takukuru, Bw. Edward Hosea.

 Raia wawili wa Korea waliokuwa wakikabiliwa na makosa ya kutoa rushwa, wamehukumiwa kwenda jela miaka mitano kila mmoja baada ya kukiri kosa mahakamani.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)  mkoani Dodoma iliwafikisha mahakamani raia wawili wa Korea kwa kosa la kutoa hongo ya Shilingi 100,000 kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Waliofikishwa mahakani ni Yun Yong Sim na Kim Song Hul ambao wanakabiliwa na kosa la kutoa rushwa kwa ajili ya kumshawishi Mganga Mkuu, Godfrey Mtey ili aweze kuwapa kibali cha Zahanati yao ambayo ilifungiwa kutokana na kutokukidhi vigezo.

Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Dodoma, Hassan Momba, aliwahukumu washtakiwa kwa kosa la kutoa rushwa ya Shilingi 100,000 kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Kaimu Kamanda wa TAKUKURU mkoani Dodoma, Sostenes Kibwengu alisema kuwa raia hao waliwekewa mtego baada ya kupokea taarifa za jambo hilo ambapo walifanikiwa kuwatia mbaroni na kuwafungulia mashtaka ya kutoa rushwa mahakamani.

Kibwengu alisema kikosi chake chini ya Kamanda wa Mkoa, Eunice Mmari kilianza kutilia shaka nyendo za raia hao baada ya kupewa taarifa za siri na raia wema na viongozi wenyewe waliotaka kuhongwa.
Walifungiwa kutoa huduma katika Zahanati yao ambayo ipo eneo la Area C’ Manispaa ya Dodoma baada ya Wizara ya Afyana Ustawi wa Jamii  kubaini ilikuwa imejengwa na kutoa huduma chini ya kiwango, “Walifungiwa  ili warekebishe baadhi ya mambo yakiwamo mazingira pamoja na kuzuiwa kuuza dawa za asili ambazo hazikuwa na vibali ndipo walipoanza kuhaha kwa ajili ya kuweka mambo sawa kwa wakubwa,’’alisema mmoja wa watu wanaoishi karibu na eneo hilo.

Taarifa zinaonyesha kuwa mbali na kufungiwa kituo hicho, lakini raia hao walikamatwa na kuwekwa korokoroni ingawa siku mbili baadaye walionekana mitaani wakitafuta namna ya kunusuru biashara yao.

Kwa mujibu wa vyanzo kutoka Uhamiaji Mkoa wa Dodoma, raia hao hata vibali vyao si halali na kwamba wanaishi kwa kutumia ujanja ujanja kutoka kwa baadhi ya watu, “Ni kweli ningekuambia kikamilifu lakini msemaji hayupo hapa isipokuwa hata mimi naweza kusema uhalali wa wao kuishi hapa nchini ni wa mashaka mashaka lakini usinitaje,’’alisema mmoja wa wafanyakazi wa Uhamiaji.

Momba alisema ametoa hukumu hiyo mapema, kutokana na washtakiwa hao kutosumbua mahakama, baada ya kukiri kutenda kosa hilo, “Mahakama imeridhika pasipo na shaka yoyote, baada ya watuhumiwa wenyewe kukiri kosa lao, kuwa walikuwa wametenda kosa hilo, hivyo watatumikia kifungo cha miaka mitano kila mmoja gerezani au watatakiwa kulipa faini ya Shilingi 500,000 kwa kila mmoja, kwa maana hiyo wote wawili watatakiwa kulipa ni Shilingi 1 milioni,’’ alisema Momba.

Hata hivyo, watuhumiwa hao kwa pamoja walilipa faini na kukwepa kwenda gerezani.

Hukumu ya watumiwa hao imekuja ikiwa ni siku moja tangu TAKUKURU waliposhinda kesi dhidi ya Ofisi Utamaduni wa zamani Manispaa ya Dodoma, Stansalaus Kobelo, baada ya kutiwa hatiani kwa kosa kama hilo. Kobelo alihukumiwa juzi na mahakama hiyo kwa kosa la kutaka rushwa kutoka kwa mmoja wa wanafunzi wa Sekondari ya Jamhuri, ili kumsaidia mambo yake. Alilipa faini ya Shilingi 500,000/=

Jumanne, 20 Septemba 2011

PICHA YA LEO; UNAIKUMBUKA ENZI YA TANCUT ALMASI BENDI YA IRINGA.

Wanamuziki mapacha wa Tancut Almasi enzi hizo, walioshika vibuyu ni mapacha Kasaloo Kyanga na Kyanga Songa ambao wote ni marehemu kwa sasa, Mungu awalaze mahala pema, Amina.
Tancut Almas wakitumbuiza, unavikumbuka vibao kama "Kumbe nilimkaribisha nyoka"(masafa marefu) na vinginevyo vilivyotamba!? Bendi hii nayo haipo tena katika Ulimwengu wa burudani.

Marehemu Kasaloo Kyanga ambaye ametutoka duniani mwezi huu mwanzoni na kuzikwa makaburi ya Sinza, Mungu amrehemu-Amia.

VIONGOZI WA CHADEMA WAWATETEA WAFUASI WAO WALIOMDHIBITI MKUU WA WILAYA YA IGUNGA KUWA WALIKUWA SAHIHI.!!!!!!

Mh. Tundu Lissu akiongea na Waandishi wa habari jana huko Igunga akilaani kitendo cha Wabunge wawili na mfuasi mmoja wa CHADEMA kufikishwa mahakamani Tabora juzi kwa kosa la kumshambulia Mkuu wa Wilaya ya Igunga aliyedaiwa kuingilia mkutano wao wa kampeni, alitaja pia nia yao ya kufanya lolote linalowezekana ili washinde kesi hiyo. Alisema watuhumiwa hao hawana kosa lolote walilotenda zaidi walikuwa wanalinda maslahi ya Chama chao.

Hivi ndio mambo yalivyokuwa hadi kupelekea Lissu kutetea waliopelekwa mahakamani, haya tusubiri tuone mahakama ikionesha haki imetendeka. Nasikia Lissu nae ni mwanasheria.

Jumatatu, 19 Septemba 2011

SHUKURANI KWA WASAMARIA WEMA


Ndugu Watanzania,



Shukrani za pekee ziwaendee wale wote aliojitolea kwa hali na mali kumchangia mtoto Sesilia Edward ambaye anahitaji msaada wa haraka wa operesheni ya moyo.


Tunapenda kuwataarifu kuwa fedha za operesheni zimekwishapatikana, na tayari tiketi mbili (ya kwake na mlezi wake Peter Nyambaliko) zimekwisha patikana.



Kwa sasa, motto Sesilia amelazwa katika hopsitali ya Regency chini ya uangalizi mkubwa wa Daktari Bingwa Dr. Kanabar na timu yake tayari kupunguza maji yalioyojaa tumboni kabla ya yeye kusafiri siku ya Jumatano.



Dola 6,100 tayari zimekwishalipwa kwa ajili ya matibabu India, na tiketi mbili zimekwishalipiwa. Tayari tumelipa shilingi 200,000 kama admission fee katika hospitali ya Regency ambapo tunatemegemea mtoto Sesilia atalazwa hadi Jumanne tarehe 20, kabla ya kusafiri Jumatano. Gharama zilizobaki za Regency zitagaramiwa na hospitali ya Regency. Yote hii ni katika kuiweka hali yake sawia kabla ya safari ndefu kuelekea India.



Bado tunahitaji msaada wa fedha za kununua madawa ambapo kwa wiki mtoto Sesilia hutumia madawa zaidi ya shilingi 50,000. Tunahitaji nguo kubwa kubwa za kuvaa kwani tumbo linaongezeka sentimeta moja kila baada ya masaa 72.  



Unaweza kumtemebelea mtoto Sesilia katika hospitali ya Regency kwa  leo jumatatu na kesho jumanne



Kama una msaada wa haraka kama nguo, chakula peleka katika kituo cha Chanel Ten – Dar es Salaam.

Na weka pesa katika account zuatazo:



Tigo Pesa:-  0715 095797

MPESA:  –  0762 962467

NMB Account: 2072517079



Kwa maelezo zaidi, piga simu 0767-262625



Watanzania tumeweza, tunamuombea mtoto Sesilia aende salama na arudi salama.

Shukrani za dhati kwenu wote kwa niaba ya Africa Media Group Limited



Hoyce Temu
Mtangazaji  - Mimi na Tanzania

Jumapili, 18 Septemba 2011

NIALL MCCANN BINGWA WA KUPAMBANA NA NYOKA, AMKAMATA ANACONDA WA UREFU WA FUTI 18.

 
Most people trekking through the jungle would turn tail and run a mile the opposite direction if they came face to face with a giant anaconda. But not Niall McCann (pictured right). Like a real-life Indiana Jones he decided instead to do battle with the beast - something he said was a lifetime's ambition. The 29-year-old biologist from Cardiff had been exploring the tropical rainforests of Guyana when he happened across the 18ft-long snake on a bank of the Rewa River.

KONDOMU ZA KIKE ZA CHINA NI NDOGO KWA WAAFRIKA KUSINI

'Kondomu za Wanawake Toka China ni Ndogo Sana'

NewsImages/5952702.jpg
Mahakama nchini Afrika Kusini imezuia uamuzi wa serikali kununua kondomu za wanawake toka China kwa kuwa kondomu hizo ni ndogo na haziwafiti vizuri wanawake wa nchini Afrika Kusini.
Mahakama ya nchini Afrika Kusini imeizuia serikali ya Afrika Kusini Kuendelea na mpango wake wa kununua kondomu za wanawake milioni 11 toka nchini China kwa kuwa kondomu hizo ni ndogo sana kwa wanawake wa Afrika Kusini.

Wizara ya fedha ya Afrika Kusini iliingia mkataba na kampuni ya Siqamba Medical, kununua kondomu za wanawake zinazoitwa Phoenurse toka China, gazeti la Beeld liliripoti.

Kampuni nyingine inayoitwa Sekunjalo Investments Corporation, ambayo ilinyimwa mkataba huo na serikali iliamua kwenda mahakamani mjini Pretoria kupinga rufaa uamuzi huo wa serikali ikisema kuwa kampuni hiyo ya nchini Afrika Kusini inatengeneza kondomu zenye ukubwa wa asilimia 20 zaidi ya kondomu zinazotengenezwa nchini China.

Jaji wa mahakama hiyo ya Pretoria alitoa uamuzi wa kuuzuia uamuzi wa serikali akisema kuwa kondomu toka China ni ndogo sana kwa wanawake wa Afrika Kusini na pia zimetengenezwa kwa vifaa ambavyo havijathibitishwa na shirika la afya la dunia (WHO).

Afrika Kusini inaongoza duniani kwa idadi kubwa ya watu walioathirika na HIV duniani.

Jumla ya watu milioni 5.38 kati ya milioni 50 waliopo nchini Afrika Kusini ni waathirika wa HIV

Jumamosi, 17 Septemba 2011

RAIS KIKWETE AWAAPISHA WAKUU WAPYA WA MIKOA IKULU LEO ASUBUHI


 Rais Dkt. Jakaya Kikwete , akimwapisha Mwantum Bakari Mahiza, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika leo asubuhi katika Viwanja vya Ikulu Dar. Katikati ni Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo.



Rais Dkt. Jakaya Kikwete, Makamu wake, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiteta jambo baada ya kuwaapisha wakuu wa mikoa Ikulu,jijini Dar es Salaam leo.



Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete amewaapisha wakuu wa mikoa aliowateua hivi karibuni.Sherehe za kuwaapisha wakuu hao wapya wa mikoa imefanyika leo asubuhi katika viwanja vya ikulu jijini Dar es Salaam.Pichani ni Mkuu mpya wa Mkoa wa Tabora. Bi.Fatuma Mwassa akila kiapo mbele ya Rais Dkt. Jakaya Kikwete na kukabidhiwa miongozo ya kazi. 
Rais Dkt. Jakaya Kikwete, akimwapisha Leonidas Tutubert Gama, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro
 
Rais Dkt. Jakaya Kikwete, akimwapisha Fabian Inyasi Massawe, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, Makamu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Mikoa walioteuliwa kushika nyadhfa hizo baada ya kuwaapisha katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo, asubuhi.